Posts

VIDEO: Magufuli "Nimechoka kuwa Rais, ni Mateso"

Image
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amesisitiza kuwa chama hicho ni kiwanda kinachopika viongozi bora, hivyo hana mpango wa kuongeza muda wa kukaa madarakani kinyume na Katiba ya chama hicho na Katiba ya nchi. TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI:

Vazi La Hijabu La Kiislamu

Image
Wanaume na wanawake, licha ya kwamba wanavyo vipengele vingi vinavyofanana, pia wanazo tabia za pekee. Mojawapo ya tabia hizi ni kwamba wanawake ni viumbe wa kuvutia, wazuri, na wanaopendwa. Ni wachangamfu, wanavutia na wanapendwa; ambapo wanaume huchangamshwa, huvutiwa na huwapenda wanawake kwa sifa zao. Mwanaume anapomuoa mwanamke, hutamani uzuri wote na mapenzi yote ya mke wake visitiriwe kwa ajili yake tu. Hutumaini kuwa ni yeye peke yake ndiye anayefaidi uchangamfu, mapenzi, kujishaua, uzuri, ukunjufu na kadhalika na kuwaepuka wanaume wengine kabisa. Mwanaume kimaumbile yu moto moto sana na hamvumilii mwanaume mwingine kumtazama mke wake au kuanzisha aina fulani ya uhusiano naye. Mwanaume ataona uhusiano wa karibu na mke wake na wanaume wengine kuwa ni kukiukwa kwa haki yake ya kisheria. Mume anatarajia mkewe kufuata kanuni ya vazi la kiislamu la Hijab na kwa kuwa mwepesi wa kubadilika kufuatana na tabia na maadili ya Kiislamu atashiriki katika kutunza haki yake ya kisheria. ...

Kubenea AJITOA Kugombea Uongozi Chadema Kisu Tundu Lissu

Image
Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea amesema Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Tundu Lissu anafaa kuwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, hivyo amejitoa kugombania nafasi hiyo katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Desemba 18, 2019 Amesema Lissu ataweza kufanya kazi ambazo yeye angeweza kuzifanya Endapo watateuliwa na Baraza, Mbunge wa Viti Maalumu wa (CHADEMA), Sophia Mwakagenda atachuana na Tundu Lissu kuwania nafasi ya Makamu Mwenyekiti Bara

Heshima Ya Mume

Image
Hamu ya kuheshimiwa ni jambo la asili, lakini si kila mtu yupo tayari kuitoa. Mumeo hukutana na watu wengi katika shughuli zake wakati hayupo nyumbani. Baadhi ya watu hao wanaweza kuwa hawana staha na kumfedhehesha hali ambayo hatimaye humtibua mtu. Wewe kama mke wake, anakutarajia wewe kuonesha heshima na ari akiwa nyumbani na kwa hali hiyo unaipandisha hadhi ya nafsi yake iliyokanyagwa. Kumstahi na kumheshimu mume wako hakukudhalilishi wewe, lakini huongeza nguvu na mwelekeo kwenye harakati za kuyafanya maisha kuwa bora. Kila mara unatakiwa umsalimie na kwa hayo maamkizi yako mfanye ahisi unamjali. Usiingilie kati mazungumzo yake. Uwe na adabu na mpole unapozungumza naye na usimpigie makelele. Inapotokea wote wawili mnakwenda kwenye mkutano ngoja mumeo aingie kwanza. Msifie mbele ya watu wengine. Waambie watoto wenu kumheshimu baba yao na uwakaripie kama hawaoneshi adabu kwake. Mheshimu mbele ya wageni na uwe makini kwa mahitaji yake, na yale ya wageni. Anapogonga mlango jar...

UHAKIKA WA KUFA NA UHAI

Image
Allah ametuumba na kutuweka katika dunia hii ili atujaribu na kutupa mitihani, kama alivyosema kuwa: «Yeye ndiye aliyeumba kifo na uhai ili akujaribuni; Ni nani miongoni mwenu mwenye matendo mazuri sana?». (Sura Almulk, aya 2). Mwenye kuamini na akawa mwenye kumuogopa Allah ataingia peponi, na atakaye chagua upotevu na upotokaji ataingia motoni. Uhai wa binadamu katika maisha haya vyovyote utakavyokuwa mrefu utafikia kikomo na utaondoka. Uhai wa milele na wa kudumu ni wa Akhera, kama Allah alivyosema kuwa: «Na kwa yakini, nyumba ya Akhera ndio maisha hasa laiti wangekuwa wanajua». (Sura Al-ankabuut, aya 64). Kiumbe bora zaidi kwa Allah ni Mtume, swallahlahu alayhi wasalam. Allah amemuambia kuwa: Utakufa kama wanavyo kufa watu wengine, na watu wote watakusanywa mbele ya Allah Siku ya Kiama ili awahukumu. «Kwa yakini, wewe utakufa na wao watakufa. Kisha nyinyi Siku ya Kiama mtashitakiana mbele ya Mola wenu». (Sura Azzumar, aya 31). Mtume, swallahlahu alayhi wasalam,  ametuelez...

WATU Wengi Hawamuelewi NYOKA Ndio Maana Wanapanic ,Chukua Tahadhari Hizi Pindi Uking'atwa

Image
Wengi wakimuona nyoka wanaanza kukimbia ,kupiga makelele.Nani kakuambia kuna nyoka ambaye akimuona mtu anaanza kumkimbiza. Nyoka sio simba au chui ambao tabia zao wakimuona mtu ambaye ni kitoweo kwao wanaanza kumkimbiza kwa nia ya kumla.Kwa nyoka la hasha hakuna nyoka wa aina hiyo awe venomous au non venoumous.Nyoka huwakimbiza rodents tu kama panya sababu ni kitoweo chao. WATCH SUBSCRIBE ON YOUTUBE Watu hawamtizami nyoka kama kiumbe wa porini Bali humtizama kama vile kitu kibaya hilo ndio tatizo. Nyoka pekee ni kiumbe namba moja ambaye watu humuelewa sivyo ndivyo Africa,hivyo ni mnyama anayeongoza kuuliwa kikatili Nyoka hupata attention mbaya sababu ya stori ambazo watu husikia pale mtu anapong'atwa Kung'atwa kwingi panatokea pale mtu anapojaribu kumzuru nyoka na kiumbe huyo anajaribu kujitetea Majira ya kiangazi nyoka hujificha sana chini ya mawe,miamba majani au kwenye miti kukaa mbali na joto la jua Mida ya jioni hujitokeza kwa wingi na usiku waka...

NAMNA YA KUSWALI

Image
Nia: Nia ni sharti la swala kuwa sahihi, kwa maana ya mtu kukusudia kwa moyo wake kumuabudu Allah kwa kuswali, huku akijua kwamba swala anayoswali ni Magharibi kwa mfano au Isha. Haitakiwi na sheria kuitamka hii nia, bali makusudio ya moyoni na akilini ndio yanayotakiwa. Kuitamka Nia ni jambo ambalo hilo halikuthibiti kunukuliwa kwa Mtume,swallalahu alayhi wasalam, wala maswahaba wake watukufu. Atasimama wima kwa ajili ya swala na kusema:  (Allahu Akbar). Atanyanyua mikono yake mpaka usawa wa mabega yake au juu yake huku matumbo ya viganja vya mikono akiyaelekeza upande wa Kibla. Takbira haiwi sahihi isipokuwa tu kwa tamko hili la (Allahu Akbar). Maana yake ni kumtukuza na kumuadhimisha Allah. Allah ni mkubwa zaidi kuliko kila kisichokuwa yeye. Ni mkubwa zaidi kuliko dunia pamoja na starehe zote na matamanio yote yaliyomo humo. Tunaziweka kando starehe zote hizo na tunaelekea kwa Allah mkubwa, mtukufu katika swala kwa nyoyo zetu na akili zetu huku tukiwa wanyenyekevu...