Posts

Showing posts from September, 2019

HAKIKA YA DUA

Image
Dua ni hakika ya kuabudu na kuonesha dalili mahususi za kuabudu ambazo ni kukimbilia na kujisalimisha kwa Allah Mtukufu. Allah amesema kuwa: «Na Mola wenu amesema kuwa: Niombeni nitakujibuni. Kwa yakini, wale wanaofanya kiburi cha kuacha kuniabudu (kuniomba) wataingia motoni wakiwa dhalili». (Sura Ghaafir, aya 60)     Allah Mtukufu ni Mkarimu zaidi ya Wakarimu. Kwa hiyo, mja anapojipeleka kwake hujibu maombi yake na kumpa kwa sababu ya kujinyongesha kwake. Mtume amesema kuwa: «Kwa yakini, Mola wenu ni mwenye haya, mkarimu. Anaona haya mja wake anaponyanyua mikono yake kwake kuirudisha ikiwa sifuri (mitupu)». (Abudaudi 1488 )    Je, Allah anawajibu wote waombao? Allah amemuahidi anaye omba kwa njia sahihi bila ya dhuluma au kuwaonea wengine kwamba atamjibu. Amesema kuwa: «Na wanapo kuuliza waja wangu kuhusu mimi, kwa yakini kabisa mimi niko karibu, ninajibu dua ya mwenye kuomba aniombapo». (Sura Albaqara, aya 186) Lakini kujibu huku kuna aina kadhaa ambazo Mt...

NYIRADI KATIKA MAZINGIRA TAFAUTI

Image
Nyiradi za asubuhi na jioni Aya Kursiy. Tazama uk.271 Sura za kinga. Tazama ukurasa 273 Kwa jina la Allah ambaye pamoja na jina lake hakiwezi kuleta madhara kitu chochote ardhini wala mbinguni na yeye ndiye tu Msikivu, Mjuzi. Mtume amefahamisha kwamba hakuna mja yeyote anaye isoma aya hii asubuhi na jioni ya kila siku mara tatu halafu akadhuriwa na kitu. (Tirmidhiy 3388) Nimeridhia kwamba Allah ndiye Mola na Uislamu ndio dini na Muhammad, swallalahu alayhi wasalam, ndiye Nabii. Mtume amesema kuwa: «Hakuna mja yeyote Muislamu anayesema wakati wa asubuhi na wakati wa jioni mara tatu kwamba: Nimeridhia kwamba Allah ndiye Mola na Uislamu ndio dini na Muhammad, swallalahu alayhi wasalam, ndiye Nabii isipokuwa kwamba ni haki kwa Allah kumridhisha mja huyo Siku ya Kiyama». (Ahmad 18967).  Ewe Mola wangu, wewe ni Mlezi wangu. Hakuna anayestahiki kuabudiwa ila wewe tu. Umeniumba na mimi ni mja wako. Na mimi niko katika ahadi yako kadiri niwezavyo. Ninaomba hifadhi kwak...

KUMUOSHA MAITI

Image
Nani anamuosha maiti?  Kama marehemu alitoa Wasia kwamba mtu fulani amuoshe, Wasia wake utekelezwe.  Wanaume na wanawake wenye umri chini ya miaka 7. Hawa wanaweza kuoshwa na wanaume au wanawake, japokuwa  jambo bora zaidi ni mtoto wa kiume aoshwe na wanaume na mtoto wa kike aoshwe na wanawake. Marehemu akiwa na umri wa zaidi ya miaka saba,wanaume tu ndio wamuoshe mwanaume na wanawake tu ndio wamuoshe mwanamke. Inafaa kwa mume kumuosha mkewe na mke kumuosha muemewe. Ali Bin Abitwalib, Allah amuwiye radhi, alimuosha mkewe Fatma, Allah amuwiye radhi. Aisha, swallahlahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Lau kama ningejua yatakayo tokea, wasingumuosha Mtume wa Allah isipokuwa  wake zake tu». (Abudaudi, Hadithi Na. 3141. Ibnumaja, Hadithi Na.1464). Kumvalisha sanda maiti Kumvalisha sanda maiti ni katika haki za lazima kwake ambazo ndungu zake na Waislamu wana wajibu wa kumfanyia.  Gharama za sanda zitachukuliwa kutoka katika mali yake aliyoacha kama anayo...

BAADA YA KUFA

Image
Mauti yakithibitika na mwili ukatengana roho, inapendekezwa yafanyike mambo kadhaa. Miongoni mwa hayo ni haya yafuatayo: Kuyafumba macho ya maiti kwa upole kwa kuonesha heshima kwake. Kuwa na subira, kujidhibiti na kutojachia kwa kupaza sauti za vilio na kuomboleza na kuwahimiza familia na ndugu wa marehemu wawe na subira. Mtume, swallahlahu alayhi wasalam, alimuamrisha mmoja wa binti zake pale mtoto wake alipokufa kwamba awe na subira na kutegemea malipo kwa Allah. (Bukhari, Hadithi Na.1284. Muslim, Hadithi Na. 923) Kumuombea marehemu rehema na kusamehewa dhambi, na kuwaombea ndugu zake subira na faraja Mtume, swallahlahu alayhi wasalam, alifanya hivyo pale alipohudhuria kifo cha Abuusalama, Allah amuwiye radhi, mmoja wa Maswahaba watukufu. Aliingia nyumbani kwake huku Abuusalama akiwa ameshakufa na macho yake yakiwa wazi. Aliyafumba kisha akasema: «Hakika, inapotolewa roho macho yanaifuatilia». Sauti za familia yake zikalipuka kwa kilio na kulalama. Mtume akasema: «Msijiombee i...

UHAKIKA WA KUFA NA UHAI

Image
Allah ametuumba na kutuweka katika dunia hii ili atujaribu na kutupa mitihani, kama alivyosema kuwa: «Yeye ndiye aliyeumba kifo na uhai ili akujaribuni; Ni nani miongoni mwenu mwenye matendo mazuri sana?». (Sura Almulk, aya 2). Mwenye kuamini na akawa mwenye kumuogopa Allah ataingia peponi, na atakaye chagua upotevu na upotokaji ataingia motoni. Uhai wa binadamu katika maisha haya vyovyote utakavyokuwa mrefu utafikia kikomo na utaondoka. Uhai wa milele na wa kudumu ni wa Akhera, kama Allah alivyosema kuwa: «Na kwa yakini, nyumba ya Akhera ndio maisha hasa laiti wangekuwa wanajua». (Sura Al-ankabuut, aya 64). Kiumbe bora zaidi kwa Allah ni Mtume, swallahlahu alayhi wasalam. Allah amemuambia kuwa: Utakufa kama wanavyo kufa watu wengine, na watu wote watakusanywa mbele ya Allah Siku ya Kiama ili awahukumu. «Kwa yakini, wewe utakufa na wao watakufa. Kisha nyinyi Siku ya Kiama mtashitakiana mbele ya Mola wenu». (Sura Azzumar, aya 31). Mtume, swallahlahu alayhi wasalam,  ametuelez...

KUFA NA KUZIKA

Image
Kifo sio mwisho wa mambo, lakini ni hatua mpya kwa mwanadamu na ni mwanzo wa maisha kamili ya Akhera. Uislamu kama ulivyo fanya hima kubwa ya kuzilinda haki tangu wakati wa binadamu kuzaliwa ndivyo pia ulivyo weka mkazo wa sheria ambazo zinalinda haki za maiti na kuangalia hali za familia yake na ndugu zake. Uhakika wa kufa na uhai Wakati wa kuwa mahututi Kumuosha maiti Nani anamuosha maiti? Kumswalia maiti Sehemu ya kuswalia swala ya jeneza Kuzuru makaburi Wasia Mirathi

DAWA DAWA DAWA KIBAMIA KWISHA OKOA NDOA YAKO LEO

Image
WASILIANA NA DOKTA 0673160865 Kwa ufupi Makala ya juma lililopita ni mojawapo ya makala niliyopokea maelfu ya maswali kutoka kwa wasomaji, naamini kama tutakuwa pamoja mtapata majibu ya maswali yenu katika mfululizo wa makala tatu zijazo. Juma lililopita tuliona sababu za wanaume kuwa na maumbile madogo ya uume. Leo tunaendelea sehemu ya pili, tutaona dondoo za kitafiti zenye kueleza ukweli wa maumbile ya uume. Makala ya juma lililopita ni mojawapo ya makala niliyopokea maelfu ya maswali kutoka kwa wasomaji, naamini kama tutakuwa pamoja mtapata majibu ya maswali yenu katika mfululizo wa makala tatu zijazo. Wanasayansi wengi wa tiba wametoa machapisho mengi ya kitafiti kuhusu urefu na upana wa uume nia na madhumuni ni kujibu swali juu ya wastani wa uume kwa wanaume wengi duniani ni upi. Baadhi ya wanaume wamekuwa wakiishi kwa hofu na kukosa kujiamini katika uhusiano wao wakihisi kuwa wana uume ambao ni mdogo usioweza kumridhisha mwenza wa ki...

Tukio la Israa Na Mi'iraaj na mafundisho yake

Image
Kutoka katika Vitabu "Zaad Al-Ma’ad" na "Ar-Rahiyq Al-Makhtuwm" بسم الله الرحمن الرحيم Kutokana na umuhimu wa tukio hili ambalo Allaah  سبحانه وتعالى  Kalielezea katika Kitabu Chake Kitukufu pale Aliposema: “ Subhaanah!   (Utakasifu ni wa) Ambaye Amemchukua mja Wake (sehemu ya) usiku kutoka  Al-Masjid Al-Haraam  mpaka  Al-Masjid Al-Aqswaa  ambao Tumevibariki vilivyoko pembezoni mwake (amechukuliwa) ili Tumuonyeshe baadhi ya  Aayaat  (miujiza, ishara, dalili)   Zetu. Hakika Yeye (Allaah) ni Mwenye kusikia yote daima, Mwenye kuona yote daim). ”  [Al-Israa: 1] Ni Mu’ujizah mkubwa kabisa wa Nabii yetu kipenzi  صلى الله عليه وآله وسلم    baada ya Mu’ujizah wa Qur-aan Tukufu, kuna haja ya kukieleza tena japo kimekwishaelezwa na kuandikwa na wengi. Tukio hili adhimu, limeelezwa na wanahistoria kwa kauli mbalimbali wakati hasa lilipotukia: 1.        Inasemekana Isr...