NYIRADI KATIKA MAZINGIRA TAFAUTI

Nyiradi za asubuhi na jioni

Aya Kursiy. Tazama uk.271
Sura za kinga. Tazama ukurasa 273
Kwa jina la Allah ambaye pamoja na jina lake hakiwezi kuleta madhara kitu chochote ardhini wala mbinguni na yeye ndiye tu Msikivu, Mjuzi.
Mtume amefahamisha kwamba hakuna mja yeyote anaye isoma aya hii asubuhi na jioni ya kila siku mara tatu halafu akadhuriwa na kitu. (Tirmidhiy 3388)
Nimeridhia kwamba Allah ndiye Mola na Uislamu ndio dini na Muhammad, swallalahu alayhi wasalam, ndiye Nabii.
Mtume amesema kuwa: «Hakuna mja yeyote Muislamu anayesema wakati wa asubuhi na wakati wa jioni mara tatu kwamba: Nimeridhia kwamba Allah ndiye Mola na Uislamu ndio dini na Muhammad, swallalahu alayhi wasalam, ndiye Nabii isipokuwa kwamba ni haki kwa Allah kumridhisha mja huyo Siku ya Kiyama». (Ahmad 18967). 
Ewe Mola wangu, wewe ni Mlezi wangu. Hakuna anayestahiki kuabudiwa ila wewe tu. Umeniumba na mimi ni mja wako. Na mimi niko katika ahadi yako kadiri niwezavyo. Ninaomba hifadhi kwako unikinge na uovu wa niliyoyafanya. Ninakiri neema zako kwangu, na ninakiri dhambi zangu kwako. Kwa hiyo, nisamehe kwa sababu hakuna anayesamehe dhambi ila wewe tu. 
Mtume amesema kuwa: «Na mwenye kuisema dua hiyo mchana akiwa na imani nayo na akafa katika mchana wake huo kabla hajafika jioni, basi yeye ni miongoni mwa watu wa peponi. Na mwenye kuisema wakati wa usiku akiwa na imani nayo na akafa kabla ya kufika asubuhi, basi yeye ni miongoni mwa watu wa peponi». (Bukhariy 5947)
Tumefika asubuhi na ufalme ni wa Allah, na shukurani anazistahiki Allah. Hakuna mwenye haki ya kuabudiwa isipokuwa Allah tu peke yake, akiwa hana mshirika. Ni wake yeye tu ufalme, na ni zake yeye tu shukurani, na yeye ni mwenye uwezo wa kila kitu. Ewe Mola wangu, ninakuomba kheri za yaliyomo katika mchana huu na kheri za yaliyomo baada yake. Na ninakuomba hifadhi unikinge na uovu wa yaliyomo katika mchana huu na uovu wa yaliyomo baada yake. Ewe Mola wangu, ninaomba hifadhi kwako unikinge dhidi ya uvivu na uzee mbaya. Ewe Mola wangu, ninaomba hifadhi kwako unikinge dhidi ya adhabu ya moto na adhabu ya kaburini. (Muslim 2723)
Na akifika jioni atabadilisha maneno ya asubuhi kwa jioni.

Dua wakati wa kula

Kabla ya kula

«Anapokula chakula mmoja wenu aseme Bismillaah. Akisahau kusema hivyo mwanzo wa kula kwake aseme Bismillaahi Fii Awwalihii Wa-aakhirihii». (Tirmidhiy 1858, 3264)

 Wakati wa kumaliza kula

«Ambaye amekula chakula na akasema Shukrani anazistahiki Allah ambaye amenipa chakula hiki na kuniruzuku bila ya mbinu zangu wala nguvu (zangu) zitasamehewa dhambi zake za zamani». (Tirmidhiy 3458, Abudaudi 4023)

Dua za nyumbani

Wakati wa kuingia nyumbani

«Mmoja wenu anapoingia nyumbani kwake aseme: Ewe Mola wangu, kwa yakini mimi ninakuomba uingiaji wa kheri na utokaji wa kheri. Kwa jina la Allah tumeingia na kwa jina la Allah tumetoka na Allah mola wetu tunamtegemea. Halafu aisalimie familia yake». (Abudaudi 5096)

 Wakati wa kutoka nyumbani

«Kwa jina la Allah. Namtegemea Allah. Hakuna mbinu wala nguvu isipokuwa kwa msaada wa Allah. Ewe Mola wangu,  ninaomba hifadhi kwako unikinge nisipotee au kupoteza, na nisipotoke au kupotosha, na nisidhulumu au kudhulumiwa, na nisiwe mjinga au kufanywa mjinga». (Abudaudi 5094, 5095)

Dua wakati wa kulala

Dua kabla ya kulala

“Bismikallaahumma amuutu wa ahyaah (Kwa jina lako ewe Mola wangu ninakufa na ninakuwa hai)”. (Bukhari, Hadithi Na. 5953 – Muslim, Hadithi Na. 2711)

Adhana na msikiti

Sheria inamtaka Muislamu kuiga anayoyasema Muadhini isipokuwa tu pale Muadhini anaposema «Hayya alasw-swalaah» au «Hayya Alalfalaah» yeye atasema: «Laa Hawla Walaa Quwwata Illaa Billaah»..
Halafu baada ya Adhana kumalizika atasema: «Ewe Mola wangu, Mlezi wa huu wito uliotmia na swala iliyo simama, mpe Muhammad Wasila na Fadhila na mfikishe kwenye hadhi ya kusifika ambayo umemuahidi». Mtume amempa habari njema mwenye kusema hayo kwamba: «utakuwa halali kwake uombezi wangu». (Bukhariy 589)    

Wakati wa kuingia msikitini

Kwa jina la Allah, na rehema na amani zimfikie Mtume wa Allah. Ewe Mola wangu, nisamehe dhambi zangu na nifungulie milango ya rehema zako. Na akitoka atasema: Kwa jina la Allah na rehema na amani zimfikie Mtume wa Allah. Ewe Mola wangu, nifungulie milango ya fadhila zako.

Baada ya swala ya faradhi

Astaghfirullaah Atayasema haya mara tatu
Ewe Mola wangu, wewe ni amani na amani inatoka kwako. Umetukuka ewe mwenye utukufu na ukarimu. (Muslim 591)
Halafu atamtakasa Allah mara 33 akisema «Subhaanallaah» na atamshukuru Allah mara 33 akisema «Alhamdu Lillaah» na atamtukuza Allah mara 33 akisema «Allaahu Akbar» na atahitimisha mara mia moja kwa kusema «Laa Ilaaha Illallaah. Wahdahuu Laa Shariika Lah. Lahulmulk Walahulhamd. Wahuwa Alaa Kulli Shay-in Qadiir». (Muslim 597) Mtume amempa habari njema mwenye kusoma uradi huu kwamba dhambi zake zitasamehewa hata kama zilikuwa (nyingi) kama povu la bahari. (Muslim 597)
Kusoma Aya Kursiy (Tazama Uk.271 )
Kusoma sura za kinga (Tazama Uk.273 )

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

Kisa Cha Nabii Ibraahiym عليه السلام - Sehemu Ya 1