Kumridhisha Mume Wako Na Si Mama Yako
Msichana anapokuwa nyumbani kwa wazazi wake anawajibika kuwaridhisha. hata hivyo, mara aolewapo, wajibu wake hubadilika. Anapokuwa nyumbani kwa mume wake, mwanamke lazima ayapatie kipaumbele mahitaji ya mume wake. Hata hapo ambapo matakwa ya mume wake na wazazi wake yanatofautiana lazima amtii mume wake, hata kama wazazi wake hawakuridhika. Kutomtii mume ni kitendo ambacho kinaweza kuharibu uhusiano wa ndoa ya mtu, na kinyume chake. Aidha, kinamama wengi hawafaidi ilmu sahihi na busara. Mama wengine, hawajatambua kwamba wanatakiwa kuwaacha mabinti zao wafikie maelewano na wanaume zao wenyewe. Wanandoa lazima waachwe wapange mambo yao wenyewe na kama wakipata tatizo lolote walitatue wao kwa kutumia uwezo wao. Kwa kuwa mama wa wake hawajui jambo hili, basi wao katika akili zao hujaribu kumfanya mkwe wao afuate wanavyotaka wao. Hujaribu kufanya hivyo moja kwa moja au kwa kuzunguka, kuingilia mambo yao ya familia. Wanawatumia mabinti zao ambao hawajapata uzoefu na hawafahamu viz...