Kumridhisha Mume Wako Na Si Mama Yako
Msichana anapokuwa nyumbani kwa wazazi wake anawajibika kuwaridhisha. hata hivyo, mara aolewapo, wajibu wake hubadilika.
Anapokuwa nyumbani kwa mume wake, mwanamke lazima ayapatie kipaumbele mahitaji ya mume wake. Hata hapo ambapo matakwa ya mume wake na wazazi wake yanatofautiana lazima amtii mume wake, hata kama wazazi wake hawakuridhika. Kutomtii mume ni kitendo ambacho kinaweza kuharibu uhusiano wa ndoa ya mtu, na kinyume chake. Aidha, kinamama wengi hawafaidi ilmu sahihi na busara.
Mama wengine, hawajatambua kwamba wanatakiwa kuwaacha mabinti zao wafikie maelewano na wanaume zao wenyewe.
Wanandoa lazima waachwe wapange mambo yao wenyewe na kama wakipata tatizo lolote walitatue wao kwa kutumia uwezo wao.
Kwa kuwa mama wa wake hawajui jambo hili, basi wao katika akili zao hujaribu kumfanya mkwe wao afuate wanavyotaka wao. Hujaribu kufanya hivyo moja kwa moja au kwa kuzunguka, kuingilia mambo yao ya familia. Wanawatumia mabinti zao ambao hawajapata uzoefu na hawafahamu vizuri hali yao, kwa lengo la kumvuta mkwe wao. Mama wakwe huwaambia mabinti zao kila wakati jinsi ya kutekeleza nini cha kufanya, kusema na asichotakiwa kusema.
Binti ambaye anamuona mama yake kama mwenye huruma na mwenye uzoefu anamtii na anajiingiza mwenyewe kwenye matamanio ya mama yake pia.
Kutakuwa hakuna matatizo yoyote kama mume atakubali matakwa ya mama mkwe wake. Hata hivyo, akionesha kukataa, basi ugomvi huanza kutokea. Kwa sababu ya ujinga wa mama mkwe anaweza kuwa jeuri ambayo inaweza kuharibu familia mabinti yake. Mama mjinga, badala ya kumpa matumaini binti yake kujitolea maisha yake kwa mume wake, anamfanya ampinge mume wake. Mama anaweza kumwabia binti yake: “Umeharibu maisha yako. Mume gani mbaya hivi! Wanaume wazuri kiasi gani walikuwa tayari kukuoa! maisha mazuri yalioje anayoishi binamu yako!
Bahati iliyoje ya dada yako! ni nini walicho nacho ambacho nyinyi hamnacho! Kwa nini uendeshe maisha ya namna hii? Binti yangu masikini!”
Mama ambaye maneno yake yanafikiriwa kama yenye huruma, husababisha ugomvi na ubishi baina ya binti yake na mume wake. Binti anawekwa katika hali ya kuanzisha ugomvi na mume wake. Wazazi wake binti watakuwa upande wake ili hatimaye washinde ugomvi, huonesha kuwa wako tayari mtoto wao apewe talaka.
“Mwanamke wa miaka thelathini alimshambulia mama yake mwenye umri wa miaka hamsini kwa sababu alisababisha kuvunjika kwa ndoa yake. Mwanamke alisema; ‘mama yangu alimsengenya mume wangu sana hivyo kwamba alisababisha mabishano mengi sana kati yangu na yeye. Hatimaye nikaachika lakini nilijuta baada ya muda mfupi. Lakini nilichelewa sana kwa sababu saa sita baada ya kutalikiana aliyekuwa mume wangu akamchumbia binamu yangu. Nilikasirika sana hivyo kamba niliamua kumpiga mama yangu.’ ”
“Mwanaume wa miaka thelathini na tisa alimkimbia mke wake na mama mkwe wake na akajiua, aliacha barua isemayo; ‘Kwa sababu ya msimamo wa mke wangu na kwa sababu hakuwa tayari kwenda Abdan na mimi, niliamua kuiaga dunia hii. Mke wangu na mama yake wanahusika na kifo changu.’ Hivyo mwanaume ambaye alichoshwa na uingiliaji wa mama mkwe wake, alijiua.”
Mwanamume ambaye alikuwa amechoshwa na uingiliaji wa mama mkwe wake, alimtupa nje ya teksi.
Bila shaka, mabinti ambao huwatii mama wa aina hii na kukubali matakwa yao, wanaweza kusababisha pigo lisiloweza kurudishwa kwao.
Kwa hiyo, mwanamke yeyote ambaye anajali familia yake, asivutiwe na matakwa ya mama yake na lazima asiyafikirie kwamba matakwa hayo ni sahihi asili mia kwa mia.
Mwanamke mwenye busara na mwerevu kila mara atapima ushauri na usemi wa mama yake kabla ya kutekeleza katika maisha ya familia yake. Anaweza kuyatekeleza kama hayakupingana au kuhatarisha mkataba wa familia yake. Kwa vyovyote vile binti atalazimika kukubali matakwa ya mama yake. Vinginevyo, kama binti akifikia hitimisho kwamba mama yake si mjuzi, na ushauri wake unaweza kusababisha ugomvi na mabishano, basi anaweza kuukataa ushauri wake.
Kwa vyovyote vile, upo uchaguzi wa aina mbili kwa binti: Kuendelea kutekeleza matakwa ya mama yake na katika hali hiyo,
kitakacho fuatilia ni mabishano ya kifamilia; au Ampuuze mama yake na kukubali kutekeleza matakwa ya mume wake.
Ni wazi kwamba, mtu hatachagua mfano wa (a) kwa sababu kama akichagua, basi ama itamlazimu aishi maisha ya kuteseka na mume wake au amtaliki. Kama ikitokea wakiachana labda mwanamke atakwenda kuishi na wazazi wake. Kwa vyovyote vile hawatamkubali kuwa kama mmoja wao wa familia na watajaribu kumfukuza. Atashushwa hadhi mbele ya watu wengine wa familia. Pia si rahisi kuishi peke yake. Pia haitakuwa rahisi kuolewa kwa mara nyingine. Anawezaje kuwa na uhakika kwamba ndoa nyingine itakuwa nzuri kuliko ya kwanza? Vipi watoto? Vipi watoto wa mume wa ndoa nyingine?
Anaweza kukata tamaa sana hivyo kwamba anaweza akajiua. Anaweza akawa mwanamke ambaye hatoweza kuishi naye hivyo kwamba mwanamume mwingine anaweza kumkimbia au hata kujiua. Mara mwanamke akitafakari matokeo ya kuendekeza matakwa ya ubinafsi na ya yasio na maana ya mama yake au watu wengine, basi lazima afanye uamuzi thabiti wa kudharau mazungumzo yote ili asihatarishe uhusiano wake na mume wake.
Angeweza akamwambia mama yake kwa hekima na adabu: “Sasa mimi nimeolewa, ni vema zaidi mimi nikijaribu kuilinda ndoa yangu na kumridhisha mume wangu. Ningependa kuwa mwema kwake, kwa sababu ni mwenzangu. Anaweza kunifurahisha na anaweza kunisaidia. Mazuri na mabaya ya maisha yanatupata tukiwa wote. Yeye ni chaguo langu na kama tukipata matatizo yoyote tutajaribu kuyatatua sisi wenyewe. Tunaweza kupanga sisi wenyewe, bila ya kupuuza ushauri wako mzuri mama. Kuingilia sana kwenye mambo yetu, inaweza kuwa sababu ya kuongeza ubaya juu ya hali mbaya ikawa mabaya zaidi.
“Kama unataka sisi kuwa na uhusiano mzuri na wewe, basi usiyaingilie maisha yetu, usimseme kwa ubaya mume wangu. (Mama naomba unielewe hivyo) vinginevyo nitalazimika kusitisha uhusiano wangu na wewe.”
Kama mama, yako kutokana na ushauri wako, anaacha kuingilia familia yenu, basi hutasumbuliwa tena. Hata hivyo, kama mama yako hayupo tayari kutilia maanani matakwa yako, punguza kumtembelea, na usiache kumshawishi mara chache hizo utakazomtembelea mpaka auone ukweli wa mambo.
Ambapo kutokana na wewe kuvunja uhusianao na wazazi wako, unaweza kupoteza kiasi fulani cha heshima yako miongoni mwa watu wa familia yako. Hivyo uwe na busara na hekima katika kumshauri mama yako, usiwe fedhuli kwake.
Mtume (s.a.w.w) alisema: “Mwanamke mzuri zaidi miongoni mwa wanawake ni yule anayezaa watoto wengi, ana upendo na safi; ambaye hakubali kutekeleza matakwa ya ndugu zake lakini mtiifu kwa ajili ya mume wake tu na hujilinda mbele ya wageni, humsikiliza mume wake na kumtii, hutimiza matamanio yake ya faragha na hapotezi staha yake kwa namna yoyote ile.”
Mtume (s.a.w.w) aliongeza: “Mwanamke mbaya zaidi miongoni mwa wanawake ni yule anaye watii ndugu zake lakini hakubali kutekeleza matakwa ya mume wake, mgumba na asiye samehe, haogopi kufanya matendo maovu, hujiremba wakati mume wake hayupo, hatimizi matakwa ya mume wake katika faragha, mume wake akimwomba msamaha hataki kumsamehe makosa yake.”
Uwe Safi Na Mrembo Nyumbani Pia
Ni desturi ya wanawake wengi kwamba huvaa nguo zao nzuri na kujipamba sana, wakati wanapokwenda kwenye hafla au mikutanoni. Hata hivyo, wanaporudi nyumbani wanavua hayo mavazi mazuri na kuvaa nguo za zamani na chakavu. Wanawake hawa hawako makini na usafi nyumbani na hawajipambi. Wanapokuwa nyumbani nywele zao zinakuwa timtim, nguo zenye madoa na soksi zilizotoboka.
Kwa kweli hali inatakiwa ibadilishwe kabisa kwa kiasi kikubwa kabisa, kwamba mwanamke anatakiwa ajipambe akiwa nyumbani na awe mchangamfu kwa mume wake ili aweze kuvutia moyo wake na ili asiache ufa wowote ambao unaweza kujazwa na wanawake wengine. Kwa nini mwanamke aoneshe uzuri wake kwa watu wengine? Hivi inastahiki mwanamke kuonesha uzuri wake kwa wanaume wengine na kusababisha matatizo kwa vijana?
Mtume (s.a.w.w) wa Uislamu alisema: “Mwanamke yeyote anayejipaka manukato na kuondoka nyumbani hawezi kupata neema za Mwenyezi Mungu Mweza wa yote hadi anaporudi nyumbani.”
Mtume (s.a.w.w) pia alisema: “Mwanamke bora zaidi miongoni mwa wanawake ni yule ambaye ni mtiifu kwa mume wake, hujiremba kwa ajili ya mume wake lakini haoneshi urembo wake kwa wageni na mwanamke mbaya kuliko wote miongoni mwa wanawake wenu ni yule anayejipamba wakati mumewe hayupo.”
Bibi mpendwa! kuuteka moyo wa mwanaume hususan kwa muda mrefu si rahisi, Usifikirie hivi kwamba: “Ananipenda, hivyo Sihitaji kuonekana mrembo kwake au kujaribu kushinda moyo wake au kumshawishi.” Lazima udumishe mapenzi yako kwake kila siku. Uhakikishe mume wako atafurahi kuwa na mke safi na mrembo hata kama hawezi kutamka. Kama ukishindwa kuridhisha matamanio ya moyo wake na huvai nguo za kuvutia unapokuwa nyumbani, anaweza akawaona wanawake wazuri wenye kuvutia nje ya nyumba.
Anaweza akakatishwa tamaa na wewe na anaweza kuelekeza mapenzi yake nje ya njia iliyo nyooka. Akiwaona wanawake wazuri anawalinganisha na wewe. Kama wewe ni mchafu, mzembe, na nywele zako ni matimtim, anaweza akadhani kwamba wanawake wengine ni malaika ambao wameteremka kutoka mbinguni. Kwa hiyo jaribu kuonekana unapendeza na kuvutia wakati ukiwa nyumbani na uhakikishe kwamba atavutiwa na wewe kila wakati.
Soma barua ifuatayo iliyoandikwa na mume: “Mtu hawezi kubainisha mke wangu na mtumishi wangu wa ndani ya nyumba. Ninaapa kwa jina la Allah kwamba wakati mwingine hufikiri: natamaani angevaa nyumbani mojawapo ya mavazi haya yalioshonwa kwa ajili ya karamu. Natamani angetupa zile nguo zilizochakaa. Nimemwambia mke wangu mara kadhaa; Mpenzi angalau vaa zile nguo nzuri hapa nyumbani unapokuwa likizo. Akajibu kwa ukali ‘ Sihitaji kwa tofauti ninapokuwa nyumbani, lakini kama siku moja ninaonekana mchafu, mbele ya wafanyakazi wenzangu, nitaona aibu.’ ”
Msomaji anaweza kuamini kwamba wakati mwanamke anaangalia usafi wa nyumba na kupika hawezi kuvaa vizuri na kupendeza.
Hii inawezekana kuwa kweli lakini mama wa nyumba anaweza kuwa na nguo tofauti za kuvaa wakati wa kufanya usafi wa nyumba; na anaweza akabadilisha nguo zake za kufanyia kazi anapokuwa mbele ya mume wake au anapokuwa amerudi nyumbani. Wakati wote unaweza kuchana nywele zako na kujiweka katika hali ya usafi baada ya kufanya usafi wa nyumba.
Imamu Baqir (a.s) alisema: “Ni wajibu wa mwanamke kujipaka manukato na kuvaa nguo nzuri sana, kujipamba kadiri iwezekanavyo, na kukutana na mume wake katika hali hii mchana na usiku.”
Imamu Sadiq (a.s) alisema: “Wanawake hawatakiwi kuacha kujiremba iwe hata kuvaa kidani tu. Usiwe na mikono isiyo tiwa rangi kidogo, hata kama ni hina kidogo tu. Hata wanawake wazee wasiache kujipamba.”
Uwe Kama Mama Kwake
Wakati wa kazi nyingi na kuumwa maradhi, mtu anahitaji kutunzwa na watu wengine. Muuguzi anaweza kusaidia kupona kwa mgonjwa vizuri mno kwa sababu ya kumwangalia mgonjwa kwa wema na mapenzi. Wanamume ni watoto wadogo ambao wamekuwa. Watahitaji matunzo kama ya mama. Mwanamume akioa mwanamke, anatarajia mke wake kuwa kama mama yake kwake wakati akiugua na matatizo.
Bibi mpendwa! Kama mume wako anaugua, muangalie zaidi kuliko ilivyo kawaida.
Onesha huruma yako kwake na uoneshe kwamba umefadhaishwa sana na ugonjwa wake huu. Mliwaze, tayarisha mahitaji yake yote na wanyamazishe watoto ili mgonjwa apumzike. Kama anahitaji daktari au dawa, basi fanya atakavyo. Mpikie chakula anacho kipenda na ambacho ni kizuri kwake. Muulize kuhusu afya yake mara kwa mara. Jaribu kukaa karibu naye kadiri iwezekanavyo. Kama anaumwa sana hivyo kwamba hawezi hata kupata usingizi na wewe usilale kadiri iwezekanavyo. Mara utakapo amka, mwendee.
Muulize hali yake inaendeleaje. Kama usiku huo hakulala kabisa, basi onesha masikitiko yako. Hakikisha chumba chake kipo kimya wakati wa mchana. Matunzo yako kwake yatasababisha mgonjwa kupata nafuu haraka. Atafurahia juhudi zako na kukupenda zaidi. Zaidi ya hayo angefanya hivyo kwako endapo ungeugua.
Mtume (s.a.w) wa Mwenyezi Mungu alisema: “Jihadi ya mwanamke ni kumtunza vizuri mume wake.”

Comments
Post a Comment