Makonda awakabidhi Suma JKT ujenzi hospitali Ubungo
Kitengo cha uzalishaji mali cha Jeshi la kujenga Taifa (suma JKT), kimepewa kazi ya kujenga hospitali ya wilaya ya Ubungo.
Amebainisha hayo jana alipotembelea eneo itakapojengwa hospitali hiyo Kimara Baruti, ambapo aliambatana na viongozi wengine na kuangalia jinsi maandalizi mbalimbali yalivyoanza kufanyika.
Makonda ametoa shukurani zake kwa mara nyingine tena kwa Rais Dkt. John Magufuli kwa kukubali ombi lake la sh 1.5 bilioni za ujenzi wa hospitali hiyo.
” Wilaya hii ni mpya inahitaji viongozi shupavu wa kuwaletea maendeleo, ni kazi ya viongozi wanaochaguliwa na wananchi.
“Kwa bahati mbaya Ubungo ilipata viongozi wanaojali matumbo yao tu. Hata leo hapa hawapo ila kesho watakuja na maneno matamu ili muwape kura” Alisema Mkuu huyo wa mkoa.
Mkurugenzi mtendaji wa Suma JKT, Kanali Rajabu Mabele amesema kuwa watahakikisha ujenzi huo unakamilika kwa muda uliopangwa.

Comments
Post a Comment