Korea Kaskazini “Kim Jong Un yuko fiti” Sio Mara ya Kwanza Kwenda Mafichoni

Rais Donald Trump wa Marekani amesema kwamba anajua hali ya Kim Joing un , kufuatia madai kuhusu afya ya kiongozi huyo wa Korea Kaskzini.

Rais huyo alisema kwamba hawezi kutoa maelezo lakini anatumai kwamba bwana Kim yuko shwari.

Kumekuwa na uvumi uliokuwa ukizunguka tangu bwana Kim alipokosa kuhudhuria sherehe za kuadhimisha siku kuu muhimu.

Hatahivyo Maafisa wa Korea Kusini wanasema kwamba hakuna lisilo la kawaida nchini Korea Kaskazini.

Katika kikao cha faragha siku ya Jumapili waziri anayehusika na maswala ya kuleta amani kati ya mataifa hayo mawili Kim Yeon – chul alisema kwamba serikali ina uwezo wa kiintelijensia kusema kwamba hakuna kisicho cha kawaida kilichokuwa kikifanyika nchini humo.

Uvumi kuhusu hali ya kiafya ya kiongozi huyo wa Korea Kaskazini ulianza baada ya kutoonekana katika maadhimisho ya sikukuu ilofanyika tarehe 15 mwezi Aprili.

TAZAMA VIDEO HII KISHA SUBSCRIBE YOUTUBE WAKUBWA TU


Vyombo vya habari vya Korea Kusini wiki iliopita viliripoti kwamba Kim Joing un huenda alifanyiwa upasuaji wa moyo ama alikuwa amejitenga ili kuzuia maambukizi ya virusi vya corona.

Hatahivyo pia vilisema kwamba ametuma ujumbe wa pongezi kwa wafanyakazi waliokuwa wakijenga hoteli ya kitalii katika mji wa Wonsan , eneo ambalo vyombo vya habari vya Korea Kusini vinasema huenda ndiko Kim anakoishi.

‘Msimamo wa serikali yetu ni thabiti”, Moon Chung-in, mshauri mkuu wa maswala ya kigeni wa rais wa Korea Kusini Moon Jae-in akijibu maoni ya vyombo vya habari nchini Marekani.

”Kim Jong un yuko hai na hali yake ni shwari. Amekuwa akiishi katika eneo la Wonsan tangu tarehe 13 mwerzi Aprili. Hakuna kisicho cha kawaida ambacho kimegunduliwa”, alisema akinukuliwa na chombo cha habari cha Aljazeera.

Je uvumi huo ulianza lini
Baada ya kukosa kuhudhuria sherehe ambayo hajawahi kukosa kuhusu kuadhimisha kuzaliwa kwa babu yake mnamo tarahe 15 mwezi Aprili .

Kukosekana kwake ndiko kulizua majadala wa hali yake ya afya kwa kuwa hajawahi kukosa sherehe kama hiyo .

Mara ya mwisho alionekana katika chombo cha habari cha serikali mnamo tarehe 12 mwezi Aprili akikagua kundi la ndege za kivita .

Uvumi ulianza wakati Kim Jong un alipokosa sherehe ya kuzaliwa kwa babu yakeHaki miliki ya pichaEPA
Image captionUvumi ulianza wakati Kim Jong un alipokosa sherehe ya kuzaliwa kwa babu yake
Katika ukaguzi huo alionekana kuwa mtu ambaye afya yake ilikuwa shwari.

Treni ya kibinafsi
Picha za setlaiti za wiki iliopita , zilionyesha treni maalum inayomilikiwa na Kim Jong un katika eneo la Wonsan na hivyobasi kuziongezea uzito ripoti hizo.

Wiki iliopita China ilidaiwa kutuma kundi moja la maafisa wake kwenda Korea Kaskazini wakiwemo wataalam wa kimatibabu.

Sio mara ya kwanza Kim kwenda mafichoni
Mwaka 2014, Kim Jong un alitoweka kwa siku 40 kuanzia mapema mwezi Septemba hatua iliozua uvumi mwingi , ikiwemo ule kwamba huenda amependuliwa na wanasiasa wengine.

Gazeti la Korea Kaskazini Rodong Sinmun lilichapisha picha kadhaa za kiongozi huyo akiwa amebeba mkwaju Oktoba 2014.Haki miliki ya pichaAFP
Baadaye akajitokeza akipigwa picha na mkwaju.

Vyombo vya habari vya serikali vilikiri kwamba alikua akiugua, lakini havikuzungumzia alikuwa akiugua nini.

Ripoti ya kuugua
Madai kwamba afya ya Kim Jong Un ilikuwa mbaya yalijitokeza katika ripoti ya tovuti iliokuwa ikimilikiwa na watoro wa Korea kaskazini.

Mara ya mwisho Kim Jong un alipigwa picha katika sherehe ya kukagua gwaride tarehe 12 ApriliHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMara ya mwisho Kim Jong un alipigwa picha katika sherehe ya kukagua gwaride tarehe 12 Aprili
Chanzo ambacho hakijulikani kiliambia gazeti la kila siku la DK kwamba wanaelewa amekuwa akiugua ugonjwa wa moyo tangu mwezi Agosti , lakini hali hiyo ikazidi kuwa mbaya baada ya kuzuru mlima Paetku mara kwa mara.

Hatua hiyo ilivifanya vyombo vya habari vya kimataifa kuanza mjadala

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

Kisa Cha Nabii Ibraahiym عليه السلام - Sehemu Ya 1