Posts

Showing posts from January, 2020

NAMNA YA KUSWALI

Image
Nia: Nia ni sharti la swala kuwa sahihi, kwa maana ya mtu kukusudia kwa moyo wake kumuabudu Allah kwa kuswali, huku akijua kwamba swala anayoswali ni Magharibi kwa mfano au Isha. Haitakiwi na sheria kuitamka hii nia, bali makusudio ya moyoni na akilini ndio yanayotakiwa. Kuitamka Nia ni jambo ambalo hilo halikuthibiti kunukuliwa kwa Mtume,swallalahu alayhi wasalam, wala maswahaba wake watukufu. Atasimama wima kwa ajili ya swala na kusema:  (Allahu Akbar). Atanyanyua mikono yake mpaka usawa wa mabega yake au juu yake huku matumbo ya viganja vya mikono akiyaelekeza upande wa Kibla. Takbira haiwi sahihi isipokuwa tu kwa tamko hili la (Allahu Akbar). Maana yake ni kumtukuza na kumuadhimisha Allah. Allah ni mkubwa zaidi kuliko kila kisichokuwa yeye. Ni mkubwa zaidi kuliko dunia pamoja na starehe zote na matamanio yote yaliyomo humo. Tunaziweka kando starehe zote hizo na tunaelekea kwa Allah mkubwa, mtukufu katika swala kwa nyoyo zetu na akili zetu huku tukiwa w...

Hekima Na Mawaidha Mazuri Aya 125 -128

Image
W aite   kwenye   njia   ya   Mola   wako   kwa   hekima   na   mawaidha   mazuri   na ujadiliane   nao   kwa   namna   iliyo   bora. Aya hii inatupa mwongozo wa mambo yafuatayo:- 1. Mwito unapasa uwe wa haki usiokuwa na lengo jingine lolote. Mtu yeyote anayetoa mwito usiokuwa wa haki, basi mwito wake utakuwa ni ufisadi na upotofu. Kosa kubwa zaidi ni la yule anayeufanya mwito wa kumwendea Mungu na kwenye haki kuwa ni nyenzo za kufikia kwenye mambo yake na jaha yake; kama wafanyavyo viongozi na maraisi wa dini na dunia. 2. Mwito uwe kwa hekima na mawaidha mazuri. Ni wazi kuwa vitenda kazi vya hekima ni elimu na akili. Akili ndiyo itakayoweza kutofautisha anayetoa mwito wa haki na wa batili na wa heri na wa sahari. Hali za wahutubiaji hujulikana kulingana na ukali na upole. 3. Mawaidha mazuri zaidi ni kuhutubia yule anayemuongoza aliyekosea kwa mfumo unaotambulisha kuwa amekosea, sio kur...

Breaking NEWS: Viongozi wa Ulaya waingia kwenye mzozo mpango wa nyukilia wa Iran

Image
Viongozi wa Ulaya wameanzisha mchakato wa kuingiza kwenye mzozo mpango wa nyukilia wa Iran, baada ya nchi hiyo kulegeza msimamo wake kuhusu mpango huo. Iran ilijiondoa katika masharti yaliyofikiwa katika mkataba huo yanayodhibiti viwango vya uzalishaji madini ya urani, ambayo inaweza kutumiwa kuunda silaha za nyuklia. TAZAMA VIDEO HII KISHA SUBSCRIBE YOUTUBE Inasema ilifanya hivyo kujibu vikwazo vipya ya Marekani dhidi yake ilipojiondoa katika mkataba wa nyukli mwaka 2018. Ufaransa, Ujerumani na Uingereza zimesema hazijaridhishwa na hoja ya Iran.

Mume Adaiwa Kumuua Mkewe kwa Kumchinja Kama Kuku

Image
MARA: Wimbi la mauaji ya wanawake yanayofanywa na waume zao waliowapenda kwa dhati na kuahidi kuishi nao kwa shida na raha, linaendelea kutikisa kila kona nchini, Gazeti la IJUMAA WIKIENDA lina mkasa wa kusikitisha.   Katika hali ya kushtua, mwanaume Juma Marwa, mkazi wa Butiama, Mara, anadaiwa kumuua mkewe wa ndoa, Devota Boniface (16) kwa kumchinja kama kuku. Kwa mujibu wa mashuhuda, tukio hilo la kutisha lilijiri baada ya mwanamke huyo kumuomba mdogo wake amletee beseni ili amnawishe mikono mumewe huyo kwa ajili ya kula chakula cha jioni.   Akilisimulia Gazeti la IJUMAA WIKIENDA juu ya tukio hilo, kaka wa marehemu, Chacha Mwita alisema mdogo wake huyo aliyekutwa na umauti aliolewa na jamaa huyo yapata miezi nane tu iliyopita. Alisema, siku ya tukio, ilikuwa yapata saa 2:00 usiku, familia hiyo ilipojumuika kwenye chakula cha jioni baada ya jamaa huyo kurejea nyumbani.   Alisema shemeji yake huyo aliporudi nyumbani, mkewe alimteng...