Naibu Waziri wa Ardhi Aagiza Wadaiwa NHC Kuchululiwa Hatua

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amekutana na Menejimenti ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwa saa nne na kulitaka shirika hilo kuhakikisha kufikia Januari 2020 inawachukulia hatua wapangaji wote wa Shirika hilo wanaodaiwa kodi inayofikia bilioni 8.23.

  • TAZAMA VIDEO HII KISHA SUBSCRIBE YOUTUBE

Dkt Mabula alikutana na Menejiment ya Shirika hilo mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam ikiwa ni mkakati wake wa kulifanya Shirika la Nyumba la Taifa kuimarika kimapato pamoja na kufanya kazi zake kwa ufanisi.

Alisema, katika kuifanya NHC inaimarika kimapato ni lazima madeni kutoka kwa wapangaji wake yanakusanywa kwa kuanzisha opreresheni maalum inatakayowezesha kutambuliwa wadaiwa wote wa kodi ili waweze kulipa kwa wakati.

‘’Ukiacha zile taasisi za serikali, wote wanaodaiwa ikifika januari 2020 wafikishwe kwenye vyombo vya sheria na zile taasisi za serikali mkamuone Katibu Mkuu HAZINA ili taasisi hizo zikatwe fedha moja kwa moja’’ alisema Dkt Mabula

Kwa mujibu wa Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, wakati wa zoezi la kufanya opresheni ya kukusanya madeni sheria lazima ifuatwe ikiwemo kutoa hati za wito wa madai kwa wadaiwa wote kabla ya hatua nyingine kuchukuliwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Umiliki na Uendelezaji wa Shirika la Nyumba la Taifa Greyson Godfrey alimueleza Dkt Mabula kuwa, pamoja na NHC kuimarika katika makusanyo lakini liko kwenye mikakati maalum wa kukusanya madeni kutoka kwa wadaiwa wake na moja ya jitihada zake ni kuingia makubaliano maalum ya namna wadaiwa watakavyolipa madeni.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa Dkt Maulid Banyani alisema Shirika lake limekuwa na mikakati mbalimbali ya kuhakikisha linaimarika kimapato ikiwemo kutoa motisha kwa watumishi wanaofanya vizuri katika mikoa itakayofikia lengo la makusanyo na  kutokuwa na malimbikizo ya madeni kutoka kwa wadaiwa wa kodi.

‘’Tumekuwa tukitoa motisha kwa watumishi wanaofanya vizuri na sasa tunaangalia ile mikao ambayo haina malimbikizo ya madeni kwa wapangaji wake kwa asilimia mia moja tuone namna tutakavyotoa motisha ili kuhamasisha mikoa kutokuwa na madeni’’ alisema Dkt Banyani

Aidha, Dkt Banyani alisema, kwa sasa NHC imeanza kufanya uhakiki kwa wapangaji wake ili kubaini wapangaji waliopangisha watu wengine ambapo eneo la Ubungo limetumika kama eneo la majaribio  na tayari wapangaji sita washaondolewa na kusisitiza kuwa zoezi hilo litakuwa ni la nchi nzima.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri Mabula aliagiza kupatiwa orodha ya nyumba zote za NHC zilizouzwa, zisizouzwa, zilizopangishwa na zisizozopangishwa, viwanja vya Shirika hilo visivyoendelezwa pamoja na Nyumba zilizokuwa za Msajili wa Majumba zilizohamishiwa NHC  hilo ili kujua hali ya shirika na mkakati wake katika kuleta ufanisi.

Pia Dkt Mabula alitembelea maendeleo ya ujenzi wa Machinjio ya Vingunguti na kuridhishwa na maendeleo ya ujenzi huo ambao uko katika hatua za mwisho za kukamilika.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

Kisa Cha Nabii Ibraahiym عليه السلام - Sehemu Ya 1