TARATIBU ZA KULA NA KUNYWA

TARATIBU ZA KULA NA KUNYWA

Uislamu unatufundisha kuwa na kiwango cha juu cha adabu, kuheshimu neema wakati wa kula na kujali usafi.
Allah ameweka taratibu kadhaa katika kula na kunywa zinazohakikisha kuwepo kwa makusudio, hekima na busara za Allah, kama kukumbusha neema za Allah kwa mwanadamu, kujikinga na maradhi, kutofanya ubadhirifu na kiburi. 
Miongoni mwa taratibu hizo ni hizi:
  1. Imekatazwa kula na kunywa katika chombo kilicho tengenewa kutokana na Dhahabu au Fedha, au kilicho nakshiwa kwa dhahabu au fedha, kwa sababu huo ni ubadhirifu na kuchupa mipaka na pia ni kuwanyongesha watu masikini. Mtume,swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Msinywe katika vyombo vya Dhahabu na Fedha, na msile katika mabakuli yake, kwa sababu vyombo hivyo ni vyao (makafiri) hapa duniani na ni vyetu (Waislamu) huko Akhera».(Bukhariy, Hadithi Na. 5110. Muslim, Hadithi Na. 2067)
  2. Kuosha mikono kabla na baada ya kula. Linasisitizwa zaidi jambo hili kama mikono ina uchafu au mabaki ya chakula.
  3. Kutaja jina la Allah kwa kusema (Bismillah) kabla ya kuanza kula au kunywa. Maana yake ni kwamba: Ninaomba baraka na ninaomba msaada kwa jina la Allah. Kama atasahau na kukumbuka katikati ya kula, atasema: (Bismillah awwalihi wa aakhirihi) (Kwa jina la Allah mwanzo na mwisho wake)
Mtume,swallalahu alayhi wasalam alimuona mtoto mdogo ambaye alikuwa hajui taratibu za kula. Alimuambia, akiwa na lengo la kumfundisha, kwamba: «Ewe kijana, litaje jina la Allah (sema Bismillah) na kula kwa mkono wako wa kulia na kula sehemu ya chakula iliyopo mbele yako». (Bukhariy, Hadithi Na. 5061. Muslim, Hadithi Na. 2022)
  1. Kula na kunywa kwa mkono wa kulia. Amesema Mtume,swallalahu alayhi wasalam, kuwa: «Msile kwa mkono wa kushoto, kwa sababu shetani anakula kwa mkono wa kushoto».(Muslim, Hadithi Na. 2019)
  2. Inapendekezwa kwamba mtu asile au kunywa akiwa amesimama.
  3. Kula chakula kilichopo karibu yake, naasile katika sehemu ya wengine, kwa sababu kula katika sehemu ya wengine ni taratibu mbaya. Mtume,swallalahu alayhi wasalam amesema kumwambia kijana mdogo kuwa: «…na kula sehemu ya chakula iliyopo mbele yako».
  4. Inapendekezwa kuokota tonge lililo dondoka, kulipangusa kama kuna kitu na kuila kama itawezekana kufanya hivyo. Kufanya hivyo ni kuijali neema na chakula.
  5. Kutokitia dosari chakula, kutokidharau na kutokibeza. Mtu anatakiwa akisifie chakula au akiache na kunyamaza. Mtume,swallalahu alayhi wasalam, hakuwahi asilani kukikashifu chakula. Akikipenda alikuwa anakila, na asipokipenda alikuwa akikiacha. (Bukhariy, Hadithi Na. 5093.  Muslim, Hadithi Na.2064)
  6. Kutokula sana na kutoshiba kupita kiasi, kwa sababu hiyo ni sababu ya maradhi na uvivu. Kula kwa wastani ndio jambo bora zaidi. Mtume,swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwanadamu hajajaza chombo kibaya sana kuliko tumbo. Vinamtosha mwanadamu vijitonge vichache vitakavyo upa nguvu mgongo wake. Ikiwa ni lazima (kula zaidi ya vitonge hivyo vichache), basi theluthi (ya tumbo) iwe kwa chakula chake, na theluthi kwa kinywaji chake, na theluthi kwa kupumua kwake».(Tirmidhiy, Hadithi Na. 2380. Ibnumaajah, Hadithi Na. 3349)
  7. Muislamu akimaliza kula atasema: (Alhamdullilah).  Atamshukuru Allah kwa neema hii ya chakula ambayo amemneemesha kwayo na kawanyima watu wengi. Inawezekana kuongeza kusema: (Alhamdu Lillaahil-ladhii Atw-amanii Haadhatw-twaama Waraqaniihi Min-ghairi Hawlin Minnii Walaa Quwwa = Ninamshukuru Allah ambaye amenipa chakula hiki na amenipa riziki si kwa ujanja wangu wala nguvu zangu). 

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU