SWALA YA IJUMAA

SWALA YA IJUMAA

Katika siku ya Ijumaa na katika wakati wa swala ya Adhuhuri, Allah amefaradhisha swala ambayo ni katika alama kubwa sana za Uislamu, na ni katika faradhi zake muhimu sana. Katika swala hiyo Waislamu hukusanyika mara moja kwa wiki, na husikiliza mawaidha na maelekezo ambayo imamu wa swala ya Ijumaa anayatoa kwao, kisha wanaswali swala ya Ijumaa.
Thawabu katika swala ya Jamaa zinakuwa kwa kadiri ya kwenda mapema kwenye swala hiyo.

Utukufu wa siku ya Ijumaa

Siku ya Ijumaa ni siku tukufu na bora zaidi katika siku za wiki. Allah ameichagua kuwa siku bora zaidi ya  nyingine, na akaitukuza kuliko nyakati nyingine kwa sifa nyingi za kipekee. Miongoni mwa sifa hizo za kipekee ni hizi: 
  • Kwamba Allah ameiteua siku hiyo iwe maalumu kwa umati wa Muhammad na wala sio kwa nyumati nyingine, kama Mtume,swallalahu alayhi wasalam, alivyosema kuwa: «Allah amewakosesha Ijumaa wale waliokuwa kabla yetu. Wayahudi wakawa na siku ya Jumamosi na Wakristo wakawa na siku ya Jumapili. Allah akatuongoza sisi kwa kutupatia  siku ya Ijumaa». (Muslim, Hadithi Na. 856)
  • Kwamba katika siku hiyo aliumbwa Adamu, na pia katika siku hiyo kitatokea Kiyama, kama Mtume,swallalahu alayhi wasalam, alivyosema kuwa: «Siku bora zaidi ambayo jua limechomoza ni siku ya Ijumaa. Katika siku hiyo aliumbwa Adamu, na katika siku hiyo aliingizwa peponi, na katika siku hiyo  alitolewa peponi, na Kiyama hakitatokea isipokuwa tu katika siku ya Ijumaa». (Muslim, Hadithi Na. 854).

Nani analazimika kuswali swala ya Ijumaa?

Swala ya Ijumaa ni wajibu kwa mwenye sifa zifuatazo:
  1. Swala ya
 Ijumaa ni wajibu kwa mwenye sifa zifuatazo
  1. Mukallaf (Mwenye kubeba majukumu kisheria):
 Sio wajibu kwa mwendawazimu, wala kwa mtoto ambaye hajabaleghe.
  1. Mkazi:
 Sio wajibu kwa msafiri, na kwa anayekaa mashambani; nje ya miji na vijiji.

Namna na sheria za swala ya Ijumaa

  1. Inapendekezwa kwa Muislamu kuoga kabla ya swala ya Ijumaa, kwenda mapema msikitini kabla ya kuanza kwa hotuba na kuva nguo nzuri sana.
  2. Waislamu wakusanyike katika msikiti mkubwa na waongozwe na imamu. Apande juu ya Minbari, awakabili  waliokuja kuswali, awahutubie hotuba mbili akitenganisha kati ya hotuba hizo kwa kukaa kidogo.  Awakumbushe kumcha Allah na kuwapa maelekezo pamoja mawaidha na aya mbalimbali
  3. Ni wajibu kwa waliokuja kuswali kusikiliza hotuba. Ni haramu kwao kuzungumza au kushughulika na jambo jingine na kuacha kufaidika na hotuba, hata kama kushughulika huko ni kwa kuchezea zulia kijiwe au mchanga. 
    Kisha imamu atateremka kwenye Minbari. Swala itaqimiwa na atawasalisha watu rakaa mbili, akisoma kwa sauti ya juu katika rakaa hizo.
  4. Sheria inataka Swala ya Ijumaa itekelezwa kwa mkusanyiko wa idadi fulani ya watu. Kwa hiyo, mwenye kupitwa na swala ya Ijumaa au akaichelewa kwa dharura basi atasali swala ya Adhuhuri badala ya Ijumaa, na wala haitasihi kwake swala ya Ijumaa.
  5. Mwenye kuchelewa swala ya Ijumaa, na ikawa hakuwahi pamoja na imamu isipokuwa sehemu chache tu ya rakaa, atakamilisha kuswali swala ya Adhuhuri.
  6. Kila ambaye sio wajibu kwake kuswali swala ya Ijumaa kama vile mwanamke na msafiri akisali msikitini pamoja na Waislamu, swala yake ya Ijumaa itakuwa sahihi, na hatalazimika kuswali swala ya Adhuhuri.

Wanaosameheka kutoswali Ijumaa

Sheria imehimiza ulazima wa kuswali swala ya Ijumaa kwa  ambao ni wajibu kwao, na ikahadharisha kuiacha na  kushughulika na mambo ya kidunia. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Enyi mlioamini,  itakapo adhiniwa kwa ajili ya swala katika siku ya Ijumaa, basi fanyeni haraka kwenda kwenye utajo wa Allah na acheni biashara. Kufanya hivyo ni bora zaidi kwenu ikiwa mnajua». (Sura Aljum-a, aya 9) 
Na sheria imemuonya anayeacha kuisali bila ya sababu za kisheria kwamba mtu huyo atapigwa chapa  katika moyo wake. Mtume,swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kuacha Ijumaa  tatu kwa kuzembea bila ya udhuru wowote, Allah atapiga chapa juu ya moyo wake». (Aabudaud, Hadithi Na.1052, Ahmad, Hadithi Na. 15498).
Maana ya kwamba Allah ataupiga chapa moyo wake ni kwamba Allah atauwekea lakiri moyo wake, ataufinika na kuweka humo ujinga na ugumu wa kutenda mema, kama zilivyo nyoyo za wanafiki na wanaofanya maasi.
Udhuru unaoruhusu kuacha kuswali Ijumaa ni kila jambo linalo kusababishia uzito mkubwa usiokuwa wa kawaida, au jambo ambalo linahofiwa kukuletea madhara makubwa katika maisha yako na afya yako.
«Enyi mlioamini, inapoadhiniwa kwa ajili ya swala katika siku ya Ijumaa, fanyeni haraka kwenda kumtaja Allah na acheni biashara». Sura Aljum’a, aya 9.

Je, ratiba ya kazi ni udhuru katika kuacha kuswali swala ya Ijumaa?

Msingi ni kwamba kazi na majukumu kudumu sio udhuru kwa Muislamu katika kuacha swala ya Ijumaa. Allah anatuamrisha kuacha kazi zetu na kwenda kuswali. Anasema «Enyi mlioamini,  itakapo adhiniwa kwa ajili ya swala katika siku ya Ijumaa, basi fanyeni haraka kwenda kwenye utajo Allah na acheni biashara. Kufanya hivyo ni bora zaidi kwenu ikiwa mnajua». (Sura Aljum-a, aya 9).
Inatakiwa kwa Muislamu kuchagua kazi na majukumu  ambayo katika kazi na majukumu hayo atapata nafasi ya kutekeleza maamrisho ya Allah hata kama masilahi yake ni madogo sana kuliko kazi na majukumu mengine. Allah Mtukufu anasema kuwa: «Na mwenye kumcha Allah atamfanyia njia, na atamruzuku kwa namna asiyodhania, na mwenye kumtegemea Allah, basi anamtosha». (Sura Attalaak, aya 2-3).

Ni wakati gani kazi inakuwa udhuru wa kuacha swala ya Ijumaa?

Kazi ya kudumu na ya kuendelea haizingatiwi kuwa udhuru wa kuacha kuswali swala ya Ijumaa kwa mtu ambaye swala ya Ijumaaa ni wajibu kwake isipokuwa tu katika hali mbili: 
  1.  Yawepo katika kazi manufaa makubwa ambayo hayapatikani isipokuwa tu kwa kubakia kwake kazini na kuacha Ijumaa, na kwamba kwa kuiacha kazi yake yatatokea madhara makubwa, na pia asiwepo mtu wa kushika nafasi yake katika kazi hiyo. 
Mifano: 
• Daktari aliyeko katika uokoaji, ambaye anatoa huduma katika kesi na matukio ya dharura.
• Mlinzi na polisi ambaye analinda mali za watu na nyumba zao zisiibwe na kudhibiti matukio ya uhalifu.
• Mtu anayesimamia utendaji wa kazi za viwanda vikubwa na mfano wake, kazi ambazo zinahitaji uangalizi wa karibu.
  1. Kazi itakapokuwa ndio chanzo pekee cha kupatia riziki yake, na hana njia nyingine ya kukidhi mahitaji yake ya msingi ikiwa ni pamoja na chakula, maji na mahitaji mengine ya msingi kwake yeye na kwa familia yake isipokuwa kazi hiyo tu, ataruhusiwa kubakia kazini na kuacha kuswali swala ya Ijumaa kwa dharura hiyo mpaka apate kazi nyingine au apate chanzo kingine kitachompatia mahitaji yake ya chakula, maji na mahitaji ya msingi yatakayomtosha yeye na anaowahudumia. Pamoja na hayo, ni wajibu kwake kuendelea kutafuta kazi na chanzo kingine cha riziki.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU