Ni nini Sunnah? Unaweza kufafanua umuhimu wa Sunnah katika Uisilamu?

Sunnah ni kile ambacho Mtume amekifanya, amekisema na matendo yake yote na ishara. Basi, tunaweza kusema kuwa alichokifanya wakati wa uhai wake ni Sunnah.

Neno sunnah limetumiwa katika vitabu vya fiqh likimaanisha “kuna malipo kama tutalifanya lakini sio dhambi kama hatulifanyi.” Mathalani, kula kwa mkono wa kulia, kusafisha meno, kutokula hali ya kuwa umesisima, n.k.
Hata hivyo, tunapolizingatia neno sunnah katika ufahamu wake mpana, linajumuisha kila alilofanya Mtume wetu. Kwa hali hiyo, utashi, na makatazo ya Allah pia yanaingia katika Sunnah. Mathalani, je Mtume wetu amesimamisha sala? Ndio. Basi ni sunnah kusimamisha sala.
Kwa mujibu wa hayo, ni lazima kuzigawa sunnah katika makundi.
FardhNi kila jambo ambalo Allah kwa hakika anatutaka tutekeleze au tuepuke. Ni Mtume wetu ambaye anaefikisha maamrisho na makatazo ya Allah kwa njia iliyo bora zaidi na ambaye anakuwa ndio kigezo. Tunapaswa kumfuata yeye ili kutekeleza kikamilifu maamrisho na makatazo ya Allah. Kama vile kusimamisha sala, kufunga swaumu, kuepuka uasherati na kutokula kitu chochote cha haram (kilichokatazwa).
Wajibu: Mambo ya wajibu katika dini yetu: kwa mfano, ni wajibu kusimamisha sala ya witr kuwa ni rakaa tatu.
Nafilah: Yale mambo mengine yasiyokuwa faradhi na wajibu ambayo yanatekelezwa kikamilifu wakati wa kusimamisha sala. Mathalani, kusoma baadhi ya aya kutoka katika Quran wakati wa kusali ni faradhi lakini kusoma dua ya subhanaka ni nafilah.
Adab: Ikiwa tutafanya harakati zetu za kila siku kama alivyofanya Mtume kama vile kula, kulala, kuingia msikitini au chooni, n.k. tutafanya kwa mujibu wa taratibu zake. Mtu asiyefanya kwa mujibu wa taratibu hizo hazingatiwi kuwa ametenda dhambi.
Hii inamaanisha tunaweza kuigawa sunnah kuwa ni faradhi, wajibu, nafilah na adab. Ni mpangilio wa ubora wa sehemu za sunnah.
Tunaweza kuifikiria kama mwili wa binadamu. Mtu ana viungo vya lazima ili aishi: mathalani, ubongo, moyo, kichwa, n.k. Kanuni ambazo ni lazima tuziamini ni kama vile moyo na ubongo kwa roho yetu.
Viwiliwili vyetu vina viungo vya hisia kama vile macho, masikio, mikono, miguu, n.k. Faradhi ni kama viungo hivyo. Faradhi ni macho, masikio, mikono na miguu kwa roho yetu. Mtu asiyetekeleza faradhi ni kama mtu asiye na mikono, miguu, macho na masikio.
Pia tuna mazuri na mapambo mengine kama vidole, nyusi na nywele katika miili yetu. Tunaweza kuishi bila ya hivyo. Hata hivyo, tukiwa navyo, tutakuwa kamilifu. Vivyo hivyo, sehemu za nafilah na adab za sunnah ni mapambo na urembo wa roho zetu. Kama tutayatekeleza, tutapata malipo mengi; kama hatuyatekelezi, hatutopata madhambi.
Kwa kuongezea, mambo ya faradhi na wajibu ni sunnah ambazo ni lazima kutekelezwa. Tutapata thawabu nyingi kama tutatekeleza nafilah na adab.
Kama ilivyo kwa haramu, lazima tuzihifadhi nafsi zetu kutokana na kuua na kutia sumu haramu kama tunavyoihifadhi miili yetu kutokana na sababu zenye kuua kama ukimwi, sumu na moto.
Umuhimu wa Sunnah
Sahihi Muslim inaeleza kwa kifupi  umuhimu wa Sunnah kama ifuatavyo:
Chochote au vyovyote Mtume wa Mungu (amani imtue) alivyofanya au kusema kuhusu jambo lolote, anafanya hivyo kama ni mtume. Kila alichokifanya huwa amelifanya bila ya mkengeuko au kasoro. Maneno yake yote na matendo yamewekewa mipaka ya mpango wa Mungu. Kwa hivyo, kila mmoja analazimika kufuata na kuiga kila hatua ya maisha yake. Maisha yake ni Quran hai, na majumlisho ya Sheria za Kiungu.
Zipo aya nyingi na hadithi nyingi katika Quran na vitabu vya hadithi, ambazo kwa usahihi kabisa zinaeleza kuwa kushikamana na Sunnah ndio msingi mkuu wa dini.
Baadhi yake ni kama ifuatavyo:
Enyi mlio amini! Mt’iini Mwenyezi Mungu, na mt’iini Mtume na wenye madaraka katika nyinyi. Na mkizozana katika jambo basi lirudisheni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume, ikiwa mnamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Hayo ndiyo bora zaidi na ndiyo yenye mwisho mwema. (an-Nisa, 4:59)
Wanazuoni wa tafsir ya Quran wamefasiri amri, “lirudisheni kwa Mwenyezi Mugu na Mtume” kuwa ni “ishaurini Quran na Sunnah”.
Badiuzzaman Said Nursi anafasiri aya hiyo, Waambie (wao, ewe Mjumbe):
“Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni na atakufutieni madhambi yenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kufuta madhambi na Mwenye kurehemu. (Aal-i Imran, 3:31) kuwa ni, kama mnamwamini Mungu (Mtukufu Aliyetakasika), kwa hakika mtampenda Yeye. Kwa kuwa mnampenda Mungu, mtatenda kwa namna anayoipenda Yeye. Ili kufanya hivyo, lazima mfanane na wale anaowapenda Mungu. Na anaweza kufananishwa kwa kumfuata yeye. Kila mnapomfuata, Mungu hukupendeni, pia. Isitoshe, mnalazimika kumpenda Mungu kwa ajili hiyo Atakupendeni.
Ibara hizi zinaunda ufupisho tu na maana ya aya kwa maneno machache. Inamaanisha kuwa lengo adhimu zaidi kwa binadamu ni kuyapokea mapenzi ya Mungu Mtukufu. Aya hiyo inaonesha kuwa njia ya kufanikiwa lengo adhimu ni kumfuata Mpenzi wa Mungu na Matendo yake. (Nuru, nuru ya 11)
Al Maududi anahutubia maelezo ya hapo chini kuhusu kujisalimisha kwenye Sunnah:
Kuziacha Sunnah za Mtume Muhammad hata kwa kiasi kidogo kunakupelekea kukosa mapenzi ya dhati kutoka kwa Mungu na mjumbe Wake. Hali ya kwanza ya upendo ni kujisalimisha kikamilifu. Mtu anayempenda Mjumbe wa Mungu, Mtume Muhammad (s.a.w.), anapaswa ajisalimishe kwake na anapaswa atiii maamrisho yake.

Katika muunganiko huu, napendelea kueleza baadhi ya sehemu zinazohusiana na kushikamana na Sunnah kutoka katika Mkusanyiko wa Risale-i Nur.

Vyanzo vya Matendo Adhimu ya Mtume Mtukufu ni vitatu: maneno yake, matendo yake, na ruhusa yake. Na vipo vifungu vitatu kwa kila moja ya vyanzo hivi vitatu: wajibu, kujitolea, na kusifika.

Ni sharti kuyafuata yote ya wajibu na ya lazima, na kuna adhabu kwa kuyaacha. Kila mmoja ana jukumu la kuyafuata. Kama ilivyo utaratibu wa kujitolea, na wa kusifika, waumini kwa mara nyengine tena wana jukumu la kuyafuata, lakini hakuna adhabu ikiwa yataachwa. Hata hivyo, kuna faida kubwa kuyatenda kwa mujibu wake na kuyafuata. Na kuyabadilisha ni uzushi, kutoongoka, na kosa kubwa. Kufuata na kuyaiga matendo ya desturi ya Mtume ni kusifiwa vilivyo na kwa mujibu wa hekima, na kuna manufaa kwa maisha ya mtu na jamii na kwa utu. Kwa hivyo katika matendo yote ya mwenendo wake kuna mambo mengi yenye manufaa kwa maisha, na halikadhalika, kwa kuyafuata hayo, ruhusa hiyo na matendo hayo kunakuwa ni kama ibada.
Ndio, kwa kuwa rafiki na adui wanakubaliana, haiba ya Muhammad (S.A.W.) inadhihirisha viwango vya juu vya maadili ya wema; na kwa kuwa wote wamekubaliana, yeye ndiye mtu mashuhuri zaidi na mbora zaidi katika watu; na kwa kuwa kama ilivyoorodheshwa na maelfu ya miujiza yake, na kuthibitishwa na Dunia ya Kiisilamu ambayo ameiasisi na mafanikio yake, na kutiliwa mkazo na ukweli wa Quran ya kuwa alikuwa ni mbashiri na mfasiri, alikuwa ni mtu bora zaidi na Sahihi na mwongozo bora zaidi; na kwa kuwa kama lilivyo tunda la kumfuata yeye, mamilioni ya watu wa usahihi wameboreka kupitia daraja za kuifikia furaha ya dunia zote mbili; kwa hakika Matendo yake ni mifano murua ya kufuatwa, na mwongozo salama zaidi, na sheria nzuri mno kuwekwa kuwa ni kanuni. Wenye furaha ni wale ambao ushiriki wao wa kuyafuata Matendo ya Mtume (S.A.W.) ni mkubwa. Ilhali wale wavivu na wasiyoyafuata hupata hasara kubwa, na wale wanaoyazingatia kuwa hayana umuhimu wanatenda uhalifu mkubwa, ilhali kama wanayakosoa, ambako kunaashiria kuyakanusha, ni kupotoka kikweli kweli. (kifungu cha maneno kutoka kitabuni)

Ewe Rafiki! Nilipokuwa natenda njia yangu kwa wasiwasi na kujawa na dukuduku, nimeshuhudia Sunnah ya Mtume Muhammad ikitoa msaada kama nyota na taa. Kila sunnah au sharia inang’aa kama jua linavyoangaza kwenye njia za uasi wa dhuluma dhini ya mtindo wa Mungu. Kama mtu, hata kama, ameacha walau punje na kujiweka mbali na njia hiyo iliyonyooka (njia ya Mungu) ya sunnah; anakuwa ni mwanasesere wa Shetani, hatua ambayo hofu na amali mbovu hutokea, na mzigo hujazwa kama mlima. (Mesnevi-i Nuriye)
Matendo ya Mtume (S.A.W.) ni adabu. Hakuna doa kati ya hayo ambayo chini yake kuna mwangaza, na adabu, sio ya kupekuliwa. Mtume Mtukufu (rehema na amani zimshukie) amesema:

Wale wanaomtii Mungu na mjumbe Wake watafuatana na mitume, waliojitolea, mashahidi, na wale ambao Mungu amewatunuku fadhila na tunu Zake. Ni marafiki wema walioje hao!

Mtu yeyote anayemtii mjumbe Wake, huwa anamtii Mungu.

Addabani Rabbi fa ahsana tadibi, maana yake ni: “Mola Wangu Mlezi amenifundisha tabia njema, na mafunzo yake ni mazuri mno.” Ndio, yeyote atakayeisoma tawsifu ya Mtume na kujua Matendo yake kwa hakika atafahamu kuwa Mungu Mtukufu amekusanya adabu mbalimbali kwa Kipenzi Chake na tabia njema. Yeyote atakayeacha matendo hayo basi ameacha adabu. Anathibitisha sheria, “Mtu mwenye maadili-mabaya amekosa baraka za Kiungu,” na kukosa adabu kwa namna ambayo humsababishia hasara.
Hadithi zinazothibitisha muungano usiovunjika kati ya Quran na hadithi:
Abu Dawud anasimulia kutoka kwa Irbad b. Sariya. Siku moja Mjumbe wa Allah alisalisha na kisha akatugeukia: akatoa hutuba fasaha mno kiasi kwamba nyoyo zinatetemeka na macho yanabubujikwa na machozi. Mmoja ya wasikilizaji alisema, “Ewe Mjumbe wa allah! Inaonekana kama ni hotuba ya kutuaga; sasa ni maamrisho gani unatupa?” Mjumbe wa Allah akasema, “nakuusieni kumcha Allah, na kusikiliza na kutii hata kama atakuwa ni mtumwa; kwa kuwa, wale watakaoishi baada yangu watashuhudia mfarakano mkubwa. Ni lazima mfuate sunnah zangu na za makhalifa waongofu. Zishikeni na lazimikianeni nazo. Jiepusheni na mambo ya kuzuazua, kwa sababu ni uzushi, na kila uzushi ni upotovu. Utakupelekeeni mtoni.”

Muslim anasimulia kutoka kwa Jabir (r.a.):
Wakati Mjumbe wa Allah anatoa hotuba, macho yake yalipiga wekundu, sauti yake ilikuwa kali na hasira zake ziliongezeka kwa hivyo alikuwa ni kama mtu anaetoa onyo dhidi ya adui na kusema, “adui amekushambulieni asubuhi na jioni pia.” Akasema pia, “Saa ya mwisho na nimeletwa kama hivi viwili” na akaunganisha kidole chake cha shahada na cha kati, na akaendelea kusema: “maneno mazuri zaidi ni yale yanayotoka kwenye kitabu cha Allah, na mwongozo bora zaidi ni ule uliotolewa na Muhammad. Na mambo maovu zaidi ni yale yaliyozushwa; na kila uzushi ni upotovu.”

Bukhari na Muslim wanasimulia kutoka kwa Anas (r.a.):
Mjumbe wa Allah (s.a.w.) alisema, “Hakuna yeyote miongoni mwenu atakayezingatiwa kuwa ni muumini isipokuwa anipende mimi zaidi ya nafsi yake, baba yake, watoto wake na kila mtu.

Mtume amesema, “Rehema za Allah ziwashukie wasaidizi wangu.” Alipoulizwa, “ni nani hao wasaidizi wako?”, akasema, “Wale wanaotekeleza Sunnah zangu na kuzifundisha kwa wengine.”

Mjumbe wa Allah anahutubia ufahari na utukufu wa Sunnah na umuhimu wa kumfuata yeye kwa muhtasari kama ifuatavyo: “Kama Musa Ibn Imran angeishi katika zama zangu, asingefanya chochote zaidi ya kunifuata mimi.”

Yaani, hakuna njia nyengine isipokuwa ni kumfuata Bwana Muhammad, ambae ni mtu sahihi kabisa, hata kwa Musa, ambae ni mtume aliyepewa kitabu; ni wema ulioje na bahati kwa mtu wa kawaida na ummah wenye dhambi kama sisi kufuata Sunnah za Mtume mkarimu.

“Kama mtaacha sunnah za Mtume wenu, mtapotea.”

“Kama mtu atafuata matamanio yake binafsi badala ya yale niliyoyaleta, hatozingatiwa kuwa ni muumini wa kweli.”

“Allah na mimi tunawalaani wale wanaoacha Sunnah zangu.”

“Mtu anaezikengeuka Sunnah zangu hazingatiwi kuwa anaifuata njia yangu.”

“Amali ya mtu ambayo haiendani na njia yangu basi hukataliwa.”

Hizo ni baadhi aya na hadithi zinazohusiana na suala hili. Kuna aya na hadithi nyingi katika Qurani na vitabu vya hadithi zinazoeleza kwa uwazi kuwa kushikamana na Sunnah ni kanuni ya lazima kwa dini. Kisha, madai ya kuwa “wacha tutende kwa mujibu wa Quran tu” yako mbali ya umakini. Waisilamu wanyoofu hawayatilii maanani madai kama hayo.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU