Kulalamika Kusiko Na Lazima katika ndoa mmh!!!!!!!!

Matatizo ya maisha ni mengi. Hakuna mtu ambaye anayo furaha kamili na hali yake. Lakini baadhi ya watu ni wavumilivu zaidi kwa matatizo yao kuliko wengine. Hujaribu kuyaweka
katika kumbu kumbu ya akili zao na hawayataji isipokuwa kama ipo sababu ya kuyafichua.
Kwa upande mwingine, wapo watu ambao ni wadhaifu mno hivyo kwamba hawawezi kuishi na matatizo yao bila ya kuyafichua. Wanayo mazoea makubwa kulalamika hivyo kwamba kila wanapokutana na watu wengine, huanza kulalamika. Popote wendapo na wakati wowote wanapokuwa kwenye mkusanyiko, hulalamika kuhusu matukio ya kila siku ambayo yameathiri maisha yao. Inakuwa kama vile wametumwa kwenye misheni na shetani mwenyewe, kuharibu furaha ya wengine. Ndio maana marafiki wengi sana na ndugu hawapendi kutiwa wasi wasi na watu wenye tabia hii na hujaribu kuwakwepa kadiri iwezekanavyo.
Lakini lazima watu wawasikitikie wake zao, na watoto wao ambao wanatakiwa kuvumilia tabia yao. Kwa sababu hakuna mtu mwingine ambaye yupo tayari kusikiliza malalamiko yao, watu hawa hutoa matatizo yao mbele ya familia zao.
Wakati mwingine hulalamika kuhusu matumizi yao, kodi marafiki zao na wakati mwingine hulalamila kuhusu wafanya kazi wenzao biashara zao, maradhi, madakitari na kadhalika.
Watu hawa ni wenye kuona kila kitu kuwa kibaya hawaoni chochote kizuri katika dunia hii. Wanateseka wao na wengine, pia na hususan familia zao huteseka pia.
Mpendwa Bwana! Kuna maana gani kulalamika wakati wote? Unafanikiwa nini katika kulalamika?
Kwa nini familia yako iteseke kwa sababu wewe umekasirishwa na dereva wa teksi? Kwa nini umlaumu mke wako kwa sababu biashara yako haiendi haraka?”
Usisahau kwamba msimamo wako utaifukuza familia yako kutoka kwako. Watakukasirikia na kukata tamaa. Wanaweza hata wakakimbia kutoka kwako na inawezekana wakaangukia kwenye mtego wa uovu na ukhalifu
Jambo la mwisho ni kwamba tabia hii huweka kovu la kiakili kwa watu wako.
Je, huoni kwamba sio jambo jema zaidi kutokuharibu furaha ya familia yako? Unaporudi nyumbani, jaribu kusahau matatizo. Furahi na familia yako. Kula nao cheka nao na furahia kuwa pamoja nao.
Pia Uislamu unachukulia uvumilivu na kutokulalamika kuwa ni tabia njema na hata umetenga thawabu kwa sifa hii. Imamu Ali (a.s) alisema: “Matatizo yanapo mpata Mwislamu, si vizuri alalamike kuhusu Mwenyezi Mungu kwa watu wengine, isipokuwa anachotakiwa kufanya ni kumpelekea Mwenyezi Mungu matatizo yake ambaye ndiye mwenye ufunguo wa matatizo yote.”
Imamu Ali (a.s) pia alisema: “Imeandikwa kwenye Taurati; yeyote anaye lalamika kuhusu tatizo ambalo limempata kwa kweli atakuwa analalamika kuhusu Mwenyezi Mungu.”
Mtume (s.a.w.w) wa Uislamu alisema: “Yeyote anayepata matatizo ya afya yake na halalamiki kuhusu jambo hilo kwa watu, basi ni wajibu Mwenyezi Mungu kumsamehe dhambi zake zote.”

Kuanzisha Ugomvi

Baadhi ya wanaume wakati wote hutafuta visingizio vya kuona kosa katika kila kitu. Hulalamika kuhusu kila jambo dogo. Kwa nini meza hii chafu? Kwa nini chakula cha mchana hakipo tayari? Kwa nini jagi la maua lipo hapa? Hivi sijasema kabla kwamba visahani vya majivu visiwekwe chini? Na kadhalika.
Wanaume hushikilia msimamo huu hadi kufika kiasi cha kusababisha ugomvi na migongano ndani ya familia zao, na wakati mwingine familia huvunjika kwa sababu ya tabia yao.
Kama mambo yalivyo hatusemi kwamba wanaume hawana haki ya kuwaambia wake zao nini cha kufanya. Mwanzoni mwa kitabu hiki, wanawake walishauriwa kukubali haki hii. Tumesema kwamba wanawake hawatakiwi kuonesha kiburi kwa ushauri wa waume zao kuhusu mambo ya familia. Hata hivyo, wanaume wanatakiwa kutumia mantiki na busara zao. Wao ni walezi wa familia zao na kwa hali hiyo, wanatakiwa kuwa na mwenendo unaostahili.
Kama mwanaume anataka kushiriki kwenye mambo ya familia basi anatakiwa kuwa na mwenendo unaostahili.
Kama mwanaume anatakiwa kushiriki kwenye mambo ya familia basi anatakiwa kufanya hivyo kwa namna iliyo fanywa. Kwa kweli, kwa kuwa mwanaume hana muda wa kutosha kushiriki katika mambo yote yahusuyo nyumba yake na kwa sababu hana utaalamu muhimu kuhusu shughuli hizo, basi ni kwa manufaa yake kumwachia mke wake kazi za nyumbani. Mwanaume anatakiwa kumwacha mke wake afanye shughuli za nyumbani kwa uhuru.
Hata hivyo, wanaume kwa kisingizio cha kutoa ushauri, wanaweza kuwakumbusha wake zao kuhusu mambo fulani bila kuwalazimisha. Mara mwanamke mwenye busara anapoona matakwa ya mume wake kufuatana nayo. Kwa hiyo, mwanaume na mwanamke ambao hujaliana wao kwa wao na familia yao.
Kwa kuzungumza pamoja kwa jinsi ilivyo wanaweza kukubaliana mambo yote. Kwa njia hii, wanawake wengi wapo tayari kukubaliana na matakwa ya waume zao ya mara kwa mara.
Lakini kama kushiriki kwake ni kutafuta dosari na kulalamika mfululizo, basi huzoea na kwa hiyo, basi mke huzoea na kwa hiyo msimamo huu unakuwa jambo la kawaida na hakuna lolote la maana litakalo tokana na hali hiyo.
Mwanamke mwenye mume mlalamikaji, hatakuwa makini naye. Mke anaweza hata asijali mambo yake yanayofaa na muhimu. Atajishauri yeye mwenyewe: “Kwa nini nipoteze nguvu zangu, kama mume wangu hatosheki hata kidogo na kazi yangu?”
Si tu kwamba hatajali shutuma za mume wake, lakini anaweza hata akalipiza kisasi.
Hapa ndipo ambapo nyumba yao hugeuka kuwa uwanja wa vita. Kushutumiana mfululizo wao kwa wao kutatayarisha uwanja wa kutengana na hivyo familia huvunjika. Katika tukio hili mwanamke hatalaumiwa kwa sababu hata mke aliye na busara na mvumilivu atashindwa kuendelea kuvumilia kwa sababu ya msimamo wa mume wake wa kudhalilisha.
“Mwanaume alipiga simu kwenye kituo cha polisi na kudai kwamba mke wake aliondoka nyumbani kwake miezi miwili iliyopita na kwamba alikuwa anaishi na wazazi wake. Baada ya uchunguzi zaidi, mke wa huyu mwanaume alisema; ‘Mume wangu hapendi mtindo wangu wa kutunza nyumba.
Wakati wote hunilaumu kuhusu mapishi yangu na uendeshaji wa mambo ya nyumbani. Kwa hiyo nimemwacha ili nipate amani mahali pengine.’ ”
Wanaume lazima wakumbuke kwamba kazi za nyumbani ni eneo la wake zao kutekeleza wajibu wao. Ni makosa kuwanyang’anya haki yao au kuwageuza kuwa vibaraka. Ni busara zaidi kuwaacha waendeshe mambo ya nyumba jinsi watakavyo.
Matokeo yake, mke wako hufanya kazi kwa shauku kubwa, utafurahi na nyumba yako itakuwa makazi ya familia yenye furaha.

Mridhishe Na Mliwaze Mke Wako

Pia mwanamke, kama ilivyo kwa mwanamume, hupata mabadiliko ya hisia kubwa. Huhisi furaha, hasira, huzuni na kadhalika. Huchoka kutokana na kazi za nyumbani na inawezekana akaudhiwa na watoto.
Watu wengine wanaweza kumtibua kwa shutuma zao. Inawezekana akaingia kwenye mashindano na wengine. Kwa ufupi, mwanamke hukabiliana na matatizo mengi ambapo mengine miongoni mwa hayo humuathiri sana hivyo kwamba anaweza kukata tamaa kwa kiwango ambacho kitasababisha atoe majibu yasiyofaa hata kwa mambo madogo.
Hususan mfano huu ni kwa upande wa wanawake, kwa sababu wao ni wepesi sana na hutoa majibu kwa umakini zaidi kwa matukio yasiyo pendeza ikilinganishwa na wanume.
Wanawake ambao hupata matatizo huhitaji kutulizwa. Wanaume lazima wawafariji kwa sababu ni wenzi wao na wao ndio wanaoaminiwa na wake zao.
Mpendwa bwana! Unapomwona mke wako katika huzuni na hasira basi jaribu kuelewa hali yake. Kama ukiingia nyumbani kwako na hakusalimu, wewe mtolee ‘salaam’. Tendo hili halita kudhalilisha wewe. Ongea naye ukiwa katika tabasamu. Epuka ukali. Msaidie kazi za nyumbani. Uwe mwangalifu usimuudhi kwa namna yoyote. Usimtanie. Kama hajisikii kuzungumza, basi mwache. Usiseme: “Unasumbuliwa na nini?”
Kama anayo hali ya kutaka kuzungumza, msikilize na mliwaze. Jifanye unahusika zaidi na tatizo lake kuliko yeye. Mruhusu akwambie malalamiko yake kwako. Halafu, kama vile baba mwema au mume mwenye huruma jaribu kumsaidia apate ufumbuzi wa tatizo lake. Mpe moyo wa kuwa mvumilivu. Kwa busara na mantiki mfanye ayaone matatizo yake kama madogo. Imarisha tabia yake na msaidie kushinda sababu ya hasira yake, uwe mvumilivu na mtendee kufuatana na mantiki yako. Kwa hakika atauona, msaada wako kuwa unafaa na maisha yatarudi katika hali yake ya kawaida baada ya muda mfupi kwenu nyinyi wote.
Kinyume chake, ukimwendea isivyo sahihi, inawezekana ukasababisha mateso zaidi kwake. Pia wewe utateseka na inaweza kusababisha ugomvi mkubwa ambao utawapa usumbufu wote wawili.

Usitafute Makosa Yake

Hapana mtu yeyote hapa duniani ambaye anazo sifa zote na hana makosa. Watu wengine wanweza kuwa wanene sana au wembamba sana. Wenye midomo mikubwa pua kubwa au meno makubnwa. Wengine wanakuwa wachafu, hawana adabu, wenye haya, fidhuli, wenye kuvunjika moyo, hasira, wivu au wachoyo. Wanawake wengine si wapishi wazuri au mwanamke mwenye kipaji. Watu wengine wanaweza kuwa walaji sana au kutumia kwa fujo.
Kwa ufupi, hakuna mtu ambaye hana mapungufu, na hakuna mtu yeyote hapa duniani anayeweza kuchukuliwa kama kiumbe kilichokamilika.
Kwa kawaida, wanaume, kabla ya kuoa hudhani kwamba atakaye muoa awe hana dosari yoyote. Hawajali ukweli huu kwamba hakuna kiumbe kifananacho na malaika hapa ulimwenguni. Wanaume hawa, mara waoapo huwaona wake zao waliodhani wakamilifu, si wakamilifu na hivyo huanza kuonesha mapungufu yao. Hudiriki kuona kuwa ndoa zao hazikufuzu na wao wenyewe kuwa na ‘bahati mbaya.’
Wanaume hawa hulalamika kila mara na hawaachi kulalamika hata dosari ndogo za wake zao.
Wanaume wengine hukuza dosari sana hivyo kwamba kila mara huziona kubwa kama milima mirefu. Mara kwa mara huzitaja dosari hizo kwa wake zao na kuwadhalilisha. Pengine huzitaja hata mbele ya marafiki na ndugu.
Matokeo ni kwmaba, msingi wa maisha yao ya ndoa huanza kutetemeka. Mwanamke hufadhaika na hupoteza shauku kwa mume wake na familia yake. Atadhani hakuna mantiki yoyote kufanya kazi kwenye nyumba ya mtu ambaye humshutumu. Inawezekana akalipiza kisasi.
Mwanaume anasema kwa mke wake: “Tazama pua yako ilivyo kubwa, na mbaya ilioje!” Na mwanamke atajibu: “Si mbaya kama uso wako mbaya na kiwiliwili chake kilicho kwenda kombo!”
Halafu mwanaume atasema: “Meno yako yananuka harufu mbaya! Na mwanamke anajibu: “Funga domo lako kubwa.” Na kadhalika.
Kuendelea kwa mazungumzo haya hufungua mlango wa shutuma na kuigeuza nyumba kuwa uwanja wa vita ambamo wanandoa hutukanana na kushushiana hadhi.
Wakiendelea kuishi namna hii, hawatafurahia maisha yao tena hata kidogo, kwa sababu nyumba isiyokuwa na mapenzi ya familia na uaminifu, si mahali pa faraja.
Zaidi ya haya, mwanaume anayejihisi kwamba yeye hana bahati na ndoa yake imeshindikana, na mwanamke ambaye hudhalilishwa wakati wote, wote wawili wanaweza kupata maradhi ya kiakili na mengineyo.
Kama ukubwa wa ugomvi wao unazidi kuongezeka basi kila mara huwepo uwezekano wa hatari ya kutalikiana au kutengana. Kutalikiana ni hatua isiyosaidia sana kwa pande zote zinazohusika, haswa kama wapo watoto katika familia.
Jamii haingeheshimu mtalaka mwanaume au mwanamke. Zaidi ya hayo kutalikiana ni hatua inayosababisha hasara ya kiuchumi kwa mwanaume; ambayo si rahisi kurekebishwa hasa zaidi hii ni kweli hapo mtalaka anapotaka kuoa tena, kwani pia atahitaji kutumia fedha tena kwenye ndoa
yake ya pili. Zaidi ya hayo, hakuna uhakika wa mtalaka kupata mwanaume ambaye atamridhisha kufuatana na matumaini yake.
Kufunga ndoa mara ya pili haitakuwa rahisi kwa sababu ya historia yake. Hata kama mwanamume atapata mwanamke mwingine, bila shaka atakuwa na mapungufu fulani pia.
Anaweza hata akawa mbaya zaidi kuliko mke wake wa kwanza. Atakuwa hana budi kumvumilia. Hii ni kwa sababu wanaume wengine wanayo majivuno makubwa kukubali dosari zao.
Ni mara chache sana utamuona mwanaume ambaye ameridhika kabisa na ndoa yake ya pili. Imewahi kutokea kwamba baadhi ya wanaume hurudi kwa wake zao wa mwanzo.
Bwana mpendwa! Kwa nini umwangalie mke wako kwa lengo la kutaka kugundua dosari zake; na kwa nini utilie maanani sana kuhusu mapungufu madogo? Kwa nini uyakuze sana makosa yake hivyo kwamba husababisha mateso kwako wewe na familia yako?
Umepata kumuona mwanamke asiye na dosari kabisa? Wewe mwenywe ni mbora kiwango gani? Ni dosari zipi ndogo ndogo zinazostahili kuhatarisha kuvunjika kwa ndoa yenu?
Uwe na uhakika kwamba kama ukimuona mke wako kwa makusudio yenye mantiki na haki, itagundua mambo mengi mazuri kuhusu yeye. Wewe tazama na uone kwamba sifa zake zitazidi dosari zake.
Uislamu unauona msimamo huu kuwa na madhara na haupendezi na kwa hiyo unakataza watu wote kutafuta na kugundua makosa ya wengine.
Mtume (s.a.w) alisema: “Enyi mnao sema, kwa ndimi zenu tu kwamba nyinyi ni Waislamu lakini imani haijaingia nyoyo zenu! Usiwaseme vibaya Waislamu na usianze kutafuta makosa yao kwa sababu yeyote anaye tafuta na kugundua dosari za wenzake, atashutumiwa na Mwenyezi Mungu na hata kama mtu kama huyu yupo nyumbani kwake, atafedheheka.”

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

Kisa Cha Nabii Ibraahiym عليه السلام - Sehemu Ya 1