Aya 6-18: Wewe Ni Mwendawazimu

Na walisema: “Ewe uliyeteremshiwa ukumbusho! Wewe ni mwen- dawazimu.
Waliosema ni maquraysh wakimwambia Muhammad aliyeteremshiwa Qur’an, kwa kumdharau. Kwa vile katika mantiki yao na vipimo vyao ni kwamba yeye ni mkichaa kwa kuwa anawaambia mambo yasiyowaingia; hata kama ni rehema kwa walimwengu na muujiza ulioshinda kwa elimu yake na mafunzo yake.
Mantiki haya hayahusiki na waabudu masanamu pekee yao wala wazandiki au walahidi; isipokuwa yanamkusanya kila anyeifanya dhati yake na manufaa yake ndio kipimo cha haki na mizani ya uadilifu, hata kama atasema: Lailaha illallah Muhammadur-rasulullah (Hapana mola isipokuwa Mwenyezi Mungu na Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu).
Kabisa! Hakuna tofauti baina ya Mwislamu huyu wa masilahi, ambaye amekubali utume wa Muhammad na mshirikina ambaye anapinga utume wa Muhammad; isipokuwa Mwislamu huyu amemwamini Muhammad kinadharia na akamakana kimatendo; na mshirikina amemkana kikauli na kimatendo. Kwa hiyo natija kwa upande wa kimatendo ni moja tu.
Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli?
Hii ni kauli ya washirikina kwa Mtume (s.a.w.). Walitoa sharti la kuamini kwao kuwa Malaika wateremshwe kutoka mbinguni na washuhudie utume wa Muhammad, ndio akawajibu kwa kusema:
Hatuteremshi Malaika ila kwa haki na hapo hawatapewa muda.
Ufupisho wa jibu ni kuwa Mwenyezi Mungu huwateremsha Malaika kwa ajili ya kufikisha ujumbe na hawateremshi kwa waongo wenye inadi, isipokuwa kwa adhabu na maangamizi; kama alivyofanya kwa umma zilizopita. Lau kama Mwenyezi Mungu angeliwajibu washirikina kwa kuwateremshia Malaika, wangeliangamia wote. Umetangulia mfano wa Aya hii kwa swali na jawabu katika Juz. 7 (6:8).
Hakika sisi tumeuteremsha ukumbusho huu na hakika sisi ndio tuulindao.
Makusudio ya ukumbusho ni Qur’an. Imesemekana kuwa dhamir katika neno kulinda inamrudia Mtume kwamba yeye ndiye alindwaye kukingwa na maadui zake, lakini hilo ni kinyume na dhahiri ya Aya. Kwa hiyo inarudia kwenye ukumbusho ambao ni Qur’an, kama tulivyofasiri.
Unaweza kuuliza kuwa Mwenyezi Mungu anailinda na nini? Ikiwa ni kuilinda na kupotolewa, kama walivyosema wafasiri wengi, basi juzi juzi1 tu Israil ilichapisha maelfu ya nakala za Qur’an na wakaipotosha Aya hii: “Na mwenye kutaka dini isiyokuwa Uislam haitakubaliwa kwake” Juz. 3 (3:85), ambayo kwenye Qur’an ya Israil inasomeka hivi: “Na mwenye kutaka dini isiyokuwa Uislam itakubaliwa kwake.”
Na kama ukisema kuwa makusudio ni kuwa hakuna yeyote atakayeitia ila, itakuwa ni kinyume na hali halisi ilivyo. Sasa ni kulindwa vipi?
Razi na Tabrasi wameleta majibu mengi yasiyokinaisha. Tuonavyo sisi ni kuwa makusudio ya kulindwa Qur’an ni kuwa kila liliomo ndani yake ni haki inayothibiti kila wakati, isiyowezwa kupingwa wala kutiwa ila kwa hoja; bali kila akili na elimu zinaavyozidi kupanuka, hujitokeza dalili mpya za ukweli wa Qur’an na utukufu wake.
Maana haya ya kulindwa Qur’an tunayapata katika kauli yake Mwenyezi Mungu:
لَا يَأْتِيهِ الْبَاطِلُ مِنْ بَيْنِ يَدَيْهِ وَلَا مِنْ خَلْفِهِ ۖ تَنْزِيلٌ مِنْ حَكِيمٍ حَمِيدٍ {42}
“Hautakifikia upotofu mbele yake wala nyuma yake, kimeteremshwa na Mwenye hekima, Msifiwa” (41:42).
Na hakika tulikwisha watuma Mitume kabla yako katika mataifa ya mwanzo. Na hakuwajia Mtume ila walikuwa wakimfanyia istihzai.
Maneno haya anaambiwa Muhammad. Mataifa ya mwanzo ni umma uliokwishapita. Maana ni kuwa hali ya washirikina - kukukadhibisha wewe na kukuita kuwa ni mwendawazimu - ni kama hali ya washirikina wa zamani. Hakuwajia Mtume ila walimkadhibisha. Pamoja na hivyo walikuwa na subira na kuvumilia upumbavu wao. Lengo ni kumtuliza Mtume mtukufu (s.a.w.). Umepita mfano wake katika Juz. 7 (6:34).
Hivyo ndivyo tunavyouingiza katika nyoyo za wakosefu hawauamini na hali umewapitia mfano wa wa kwanza.
Dhamir ya tunavyouingiza na hawauamini inarudia kwenye ukumbusho (Qur’an). Maana ni kuwa Qur’an haiingii katika nyoyo za wakosefu kiukweli na kiimani; isipokuwa inaingia kidharau na kikejeli.
Kauli yake Mwenyezi Mungu ‘hawauamini’ ni tafsiri ya ‘tunavyouingiza.’ Maana ya ‘umepita mfano wa wa kwanza ni kuwa wakadhibishaji wa sasa ni kama wakadhibishaji wa zamani. Nyoyo zao zinaingia batili badala ya imani na upotevu badala ya uongofu.
Kusema kuwa Mungu anawaingiza ni kunasibisha kitu kwa sababu yake ya mbali moja kwa moja. Yamekwishapita maelezo ya hayo mara kadhaa.
Na lau tungeliwafungulia mlango wa mbingu wakawa wanapanda, baswangelisema“Machyetyamelevywabalsisnwatu waliorogwa.”
Katika Aya ilyotangulia, wapinzani walimtaka Muhammad (s.a.w.) kuwateremshia Malaika. Mwenyezi Mungu akwajibu kwamba Malaika hushuka na adhabu ya mangamizi kwa wapinzani na wakadhibishaji.
Kisha katika Aya hii akafuatishia jibu hilo kwa kusema kuwa lau atawafungulia milango ya mbinguni, kisha wapande kwa mili yao na wawaone Malaika na maajabu mengi, wangelisema: hakika Muhammad ameturoga na ametuonyesha njozi kuwa hali halisi na halisi kuwa njozi. Umetangulia mfano wake katika Juz. 7 (6:7).
Hakika tumeweka katika mbingu buruji na tumezipamba kwa wenye kuangalia.
Baadhi ya wafasiri wamesema kuwa makusudio ya buruji ni nyota. Wengine wakasema ni vituo vya sayari ya Jua na Mwezi.
Vyovyote iwavyo, lengo la Aya sio kutufundisha elimu ya falaki ili tujue hiyo buruji hasa ni nini; isipokuwa lengo la kwanza kabisa ni kuzingatia na kutilia manani (tadabbur) uwezo wa Mwenyezi Mungu na hekima yake katika kuumba mbingu na ardhi na kwamba undani, nidhamu na uzuri aliouumba ni dalili wazi ya kuweko Mwenyezi Mungu na umoja wake, kuliko kuteremsha Malaika na kuliko miujiza yote wanayoitaka
Na tukazilinda na kila shetani afukuzwaye; isipokuwa asikilizaye kwa kuiba, naye hufuatwa na kijinga kinachoonekana.
Watu wa wakati wa jahilia walikuwa wakiamini kuwa kila kuhani ana shetani wake apandae mbinguni na kusikiliza mazungumzo ya Malaika kuhusu watu wa ardhini, kisha anashuka ardhini kwa kuhani wake kumpa habari. Aya mbili hizi zinapinga na kukana ngano hizi na kwamba mashetani hawawezi kabisa kupanda mbinguni. Na kusema kwake kijinga kinachoonekana ni fumbo la kuwa shetani hawezi kabisa hata kukurubia kuwasikilza Malaika; kama walivodai watu wa zama za jahiliya.
وَالْأَرْضَ مَدَدْنَاهَا وَأَلْقَيْنَا فِيهَا رَوَاسِيَ وَأَنْبَتْنَا فِيهَا مِنْ كُلِّ شَيْءٍ مَوْزُونٍ {19}
Na ardhi tumeitandaza na tumeweka humo milima na tumeotesha kila kitu kwa wizani.
وَجَعَلْنَا لَكُمْ فِيهَا مَعَايِشَ وَمَنْ لَسْتُمْ لَهُ بِرَازِقِينَ {20}
Na tumejaalia humo maisha. Na ya ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.
وَإِنْ مِنْ شَيْءٍ إِلَّا عِنْدَنَا خَزَائِنُهُ وَمَا نُنَزِّلُهُ إِلَّا بِقَدَرٍ مَعْلُومٍ {21}
Na hakuna chochote ila hazina yake iko kwetu na wala hatukiteremshisipokuwa kwa kipimo maalum.
وَأَرْسَلْنَا الرِّيَاحَ لَوَاقِحَ فَأَنْزَلْنَا مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَأَسْقَيْنَاكُمُوهُ وَمَا أَنْتُمْ لَهُ بِخَازِنِينَ {22}
Ntukazipelekpepza kupandishia na tukateremsha kutokmbingunmaji tukawanyweshhaywala nyinysimnaoyaweka akiba.
وَإِنَّا لَنَحْنُ نُحْيِي وَنُمِيتُ وَنَحْنُ الْوَارِثُونَ {23}
Na hakika sisi ndio tunaohuyishntunaofishaNsisi ndio warithi.
وَلَقَدْ عَلِمْنَا الْمُسْتَقْدِمِينَ مِنْكُمْ وَلَقَدْ عَلِمْنَا الْمُسْتَأْخِرِينَ {24}
Na hakika tunawajua watanguliao katika nyinyi na hakika tunawajua wachelewao.
وَإِنَّ رَبَّكَ هُوَ يَحْشُرُهُمْ ۚ إِنَّهُ حَكِيمٌ عَلِيمٌ {25}
Na hakika Mola wako ndiye atakayewakusanyaHakika YeynMwenyhekima, Mjuzi.
  • 1. Kumbuka juzijuzi hiyo, ilikuwa ni katika mwaka wa 1969 - Mtarjumu.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU