Aya 101 – 105: Aya Mahali Pa Aya Nyingine

Lugha

Tofauti kati ya neno Aa’jamiyy na A’jamiyy ni kuwa la kwanza lina maana ya mtu asiyekuwa fasaha katika Kiarabu, hata kama ni mwarabu. Na lapili lina maana ya lugha nyingine isiyokuwa Kiarabu.

Maana

Na tunapobadilisha Aya mahali pa Aya nyingine, na Mwenyezi Mungu anajua anayoteremsha. Wao husema: “Hakika wewe ni mzushi.” Bali wengi wao hawajui.
Wanaosema hapa ni washirikina waliomkadhibisha Muhammad (s.a.w.). Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amewaumba viumbe na Yeye ni mwenye hekima, Mjuzi wa kujua masilahi yao na uharibifu wao. Mara nyingine hekima inaona kuwa ni masilahi kuweka kwa waja wake sharia ya hukumu kwa muda fulani, wakafanya.
Kisha ukiisha ule muda, sharia ile inaondolewa naYule ambaye imetukuka hekima yake huweka hukumu nyingine mahali pa ile hukumu ya kwanza kulingana na masilahi vilevile.
Haya ndiyo makusudio ya kauli yake Mwenyezi Mungu: Tunapobadilisha Aya mahali pa Aya nyingine’
Washirikina walipokuwa wakiona hivi humwambia Muhammad (s.a.w.) kuwa wewe unajifanyia mwenyewe tu haya kisha unayanasibisha kwa Mwenyezi Mungu kwa uwongo na uzushi. Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anajua kuwa Yeye ndiye aliyeteremsha mabadiliko haya kwa Mtume wake mkweli, mwaminifu na anajua kuwa wao ndio wazushi kwa kusema kwao kuwa Mtume ni mzushi.
Tafsiri wazi zaidi niliyosoma kuhusu Aya hii ni ile iliyopokewa kutoka kwa Ibn Abbas, kwamba inapoteremshwa Aya ya ugumu kisha ikateremshwa Aya ya laini, maquraishi husema kuwa Muhammad anawachezea maswahaba zake; leo anawaamrisha hivi na kesho anawakataza na kwamba yeye hayasemi haya ila yeye mwenyewe tu, ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha Aya hii. tumezungumzia kuhusu kufuta hukumu katika Juz. 1 (2:106).
SemameiteremshRohtakatifkutokkwMolwakoili awathibitishe wale walioamini na kuwa ni uwongofu na bishara kwa Waislamu.
Roho takatifu ni Jibril. Ameitwa hivyo kwa sababu ameteremsha Qur’an ambayo ni takatifu kutoka kwa Mwenyezi Mungu hadi kwa Muhammad (s.a.w.). Umetangulia mfano wa Aya hii katika Aya ya 89 ya sura hii.
Hapa imetajwa kwa kuwarudi washirikina walionasibisha kubadilisha kwa Mtume. Kule imetajwa kwa mnasaba wa kuwa Mwenyezi Mungu amesema atamleta shahidi kwa kila umma na Muhammad atakuwa shahidi wa umma wake kwamba yeye amiefikisha Qur’an ambayo ni ubainifu wa kila kitu.
Na hakika tunajua kwamba wao wanasema yuko mtu anayemfundisha.
Washirikina walimtuhumu Muhammad (s.a.w.) kwamba yeye anafundishwa Qur’an na mtu mwingine. Hakuna mwenye shaka kwamba hii ni aina ya vita vya propaganda za uwongo wanazozitangaza wafisadi duniani kwa masilahi yao. Leo watu wameendelea na mfumo wa aina yake katika propaganda dhidi ya wenye ikhlasi na viongozi wema. Wamekuwa na ufundi ambao unawahadaa watu wema wengi walio wasafi.
Lugha ya huyo wanayemuelekezea sio fasaha na hii ni lugha ya kiarabu bayana.
Yaani lugha ya huyo mtu wanayemsema ni kiarabu cha mtaani.
Hii ni kuwarudi washirikina na kauli yao kuhusu Muhammad (s.a.w.) kwamba anafundiswa na mtu mwingine. Hapa inaonyesha kwamba huyo mtu waliyemsema kuwa anamfundisha, lugha yake ni ya mtaani na lugha ya Qur’an ni kiarabu fasihi. Sasa itawezekana vipi asiyejua fasihi amfundishe mwengine fasihi.
Walirudiarudia uzushi huu maadui wa Uislamu baadae na mpaka leo wahubiri wengi wa Kikiristo wanathubutu kusema, kwa kutojua au kujitia kutojua, kwamba kwenye Qur’an kuna fani na hekima ambazo wakati huo hazikuwa na athari yoyote.
Kama tukichukulia kuwa zilikuweko, basi isingewezekana yeyote kuzikusanya na kuzijua na kama angelizijua basi umashuhuri wake ungelizidi ule wa Aristatle ambaye Waarabu wanamwita mwalimu wa kwanza. Licha ya wao kujua kwamba hakuwa na yeyote aliyekuwa wakati wa Mtume aliyedaiwa kujua hizo elimu zilizomo ndani ya Qur’an.
Hakika wale ambao hawaziamini Aya za Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu hawaongoi, nao watapata adhabu chungu.
Makusudio ya Aya za Mwenyezi Mungu ni dalili zinazosema kuhusu kuweko kwake, miujiza inayoshuhudia utume wa Mitume na hukumu zilizoteremshwa kwao. Ama makusudo ya uongofu hapa ni thawabu; yaani Mwenyezi Mungu hatampa thawabu, bali atamwadhibu kwa aina za adhabu

Mwongo Kafiri

Hakika wanaozua uwongo ni wale tu wasioziamini Aya za Mwenyezi Mungu wala ufufuo, hisabu na malipo; kama washirikina waliomwambia Muhammad (s.a.w.) yale waliyomwambia.
Na hao ndio waongo.
Wanajasiri kusema uwongo na kufanya ufisadi na dhambi kwa vile wao hawaogopi adhabu ya uwongo na wala hawatarajii thawabu.
Unaweza kuuliza: Kauli yake Mwenyezi Mungu: Hakika wanaozua uwongo ni wale tu wasioziamini Aya za Mwenyezi Mungu’ si inatosha, sasa kuna haja gani tena ya kusema: Na hao ndio waongo’? Je, kuna makusudio gani ya kukaririka huku? Wafasiri wamejibu kuwa lengo ni kutanabahisha kuwa sifa ya uwongo kwao imethibiti; sawa na kumwambia mtu: ‘Wewe ni mwongo tena mwongo sana’ yaani hali yako na mazoweya yako ni uwongo tu.
Swali la pili ni: Mwenyezi Mungu anasema “Hakika wanaozua uwongo ni wale tu wasioziamini Aya za Mwenyezi Mungu” Hii si ni kuwafanya makafiri kuwa ndio waongo tu; na inajulikana kuwa kuna makafiri walio wakweli sana na wakutegemewa zaidi, katika mazungumzo yao, kuliko wale wanaomwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho?
Jibu: Hakika Mwislamu muongo anamwamini Mwenyezi Mungu kinad- hariya na ni kafiri kimatendo. Kwa hiyo yeye kwa wasifu wake ni muumini kinadhariya na kifikra, atachukuliwa duniani kuwa ni Mwislamu. Na kafiri kwa wasifu wake atachukuliwa kuwa ni kafiri kulingana na Aya hii na yaliyopokewa kutoka kwa Mtume, alipoulizwa: Je, Mumin anasema uwongo? Akajibu: La; kisha akasoma Aya hii.
مَنْ كَفَرَ بِاللَّهِ مِنْ بَعْدِ إِيمَانِهِ إِلَّا مَنْ أُكْرِهَ وَقَلْبُهُ مُطْمَئِنٌّ بِالْإِيمَانِ وَلَٰكِنْ مَنْ شَرَحَ بِالْكُفْرِ صَدْرًا فَعَلَيْهِمْ غَضَبٌ مِنَ اللَّهِ وَلَهُمْ عَذَابٌ عَظِيمٌ {106}
AnayemkufurMwenyezi Mungbaadyimani yakeIsipokuwaliyelazimishwa na hali ya kuwa moyo wake umetua juu ya imani. Lakini aliyekifungulia kifua chake ukafiri, basi haghadhabya Mwenyezi Mungu iko juu yanwatapatadhabu kubwa.
ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمُ اسْتَحَبُّوا الْحَيَاةَ الدُّنْيَا عَلَى الْآخِرَةِ وَأَنَّ اللَّهَ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْكَافِرِينَ {107}
Hiyo ni kwa sababu wao wamestahabmaishya dunia kuliko ya akhera. Na kwamba Mwenyezi Mungu hawaongoi watu makafiri.
أُولَٰئِكَ الَّذِينَ طَبَعَ اللَّهُ عَلَىٰ قُلُوبِهِمْ وَسَمْعِهِمْ وَأَبْصَارِهِمْ ۖ وَأُولَٰئِكَ هُمُ الْغَافِلُونَ {108}
Hao ndio ambao Mwenyezi Mungu amepiga chapa juu ynyoyzanjuya masikio yao; na hao ndio wenye kughafilika.
لَا جَرَمَ أَنَّهُمْ فِي الْآخِرَةِ هُمُ الْخَاسِرُونَ {109}
Hapanshakkwamba wao ndio wenye kuhasirika Akhera.
ثُمَّ إِنَّ رَبَّكَ لِلَّذِينَ هَاجَرُوا مِنْ بَعْدِ مَا فُتِنُوا ثُمَّ جَاهَدُوا وَصَبَرُوا إِنَّ رَبَّكَ مِنْ بَعْدِهَا لَغَفُورٌ رَحِيمٌ {110}
Kisha hakika Mola wako kwa wale waliohajiri baada ykusumbuliwkisha wakafanya jihadi na wakasubiribilshakMola wakbaadyhayni Mwingwmaghufira, mwenye kurehemu.
يَوْمَ تَأْتِي كُلُّ نَفْسٍ تُجَادِلُ عَنْ نَفْسِهَا وَتُوَفَّىٰ كُلُّ نَفْسٍ مَا عَمِلَتْ وَهُمْ لَا يُظْلَمُونَ {111}
Sikambayo kila nafsi itakuja jitetea. Na kila nafsi italipwa sawa na yale iliyoyafanyanahawatadhulumiwa.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

Kisa Cha Nabii Ibraahiym عليه السلام - Sehemu Ya 1