Nini maana ya utumwa (kunyenyekea) kwenye Uislamu? Ni nini maana ya kumuabudu Allah?

Dear Brother / Sister,
Utumwa ni kitendo cha kutengeneza uhusiano baina ya mwanadamu na Muumba, Allah. Hivyo basi, ukweli kwamba Allah ndie Muumbaji na mwanadamu ameumbwa unasisitizwa kwenye aya za mwanzo kabisa kama zilivyoshushwa:
“Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba. Amemuumba binaadamu kwa tone la damu” (al-Alaq, 96/1-2).
Qur’an inavuta hisia za umakini kuhusu uhusiano huu mwanzo mwa aya inayomtaka mwanadamu kuabudu:
“Enyi watu! Muabuduni Mola wenu Mlezi aliye kuumbeni nyinyi na wale wa kabla yenu, ili mpate kuokoka.” (al-Baqara, 2/21).  
Inafahamika kuwa kutoka kwenye aya ya hapo juu kwamba kuabudu ni jukumu la kiuumbaji la asili ya mwanadamu, ni kupeleka shukrani kwa Muumba, na ni tendo tukufu linalopelekea kutambua lengo la kiroho na kimwili.
Sasa tutawasilisha ukweli wa kunyenyekea, ambao tumejaribu kuonesha katika baadhi ya mambo:
Kunyenyekea hufanywa kwa njia mbili: Ya kwanza ni unyenyekevu unaofanywa bila kuzingatia kuonekana kwa Muumbaji na kutokuzungumza na Yeye.; na wa pili ni unyenyekevu wa kumuelekea Yeye.
1. Unyenyekevu unaofanywa bila kuzingatia kuonekana kwa Muumbaji unaweza kufupishwa kama ifuatavyo:
a. Utumwa (Servitude): Kuthibitisha ukubwa wa Allah kusifia ufundi wake kwa kuangalia utendaji usiokifani wa Muumba unaoonekana ulimwengu mzima kama vile kutengeneza, kudhibiti, kupanga na kusanifu. 
b. Utumwa (Servitude): Kuangalia uzuri wa usanifu unaoakisi majina mazuri ya Mungu, kuyazungumzia, na kila mmoja kumuonesha mwenzake ili kupata mazingatio kupitia majina hayo.
c. Utumwa (Servitude): Kutathmini lengo la uzuri wa majina ya Allah, ambayo yana faida za kiroho, pamoja  na kiakili na kuyasifu toka moyoni.
d. Utumwa (Servitude): Kupokea, kufikiri na kutafakari kurasa za ulimwengu kama kitabu kilichoandikwa na kalamu ya nguvu na hekima ya Allah.
e. Utumwa (Servitude): Kuangalia Sanaa ya hali ya juu, darizi nzuri na maumbo yaliyopambwa yanayoonekana pembe zote za dunia, kuangalia uzuri wa kiroho na ukamilifu wa Muumbaji na kumjua kwa ukaribu mno, ili kumpenda na kumuheshimu.
2. Unyenyekevu mbele ya Allah na kuzungumza nae unaweza kufupishwa kama ifuatavyo: The servitude in the presence of the Creator addressing Him can be summarized as follows:
a. Utumwa (Servitude): Kujua kwamba mwanadamu siku zote yupo mbele ya Allah na kutenda ipasavyo. Kumfikia mtendaji kupitia matendo na kumfikia msanii kupitia Sanaa.
b. Utumwa (Servitude): Kufahamu kwamba Muumbaji anataka ajulikane kwa kuonesha Usanii wa hali ya juu na wa kimaajabu; na kujibu jambo hili kupitia Imani.
c. Utumwa (Servitude): Kufahamu kwamba Allah, ni mwingi wa huruma, anataka  kupendwa kwani huonesha matunda ya huruma yake   kama akisi/picha ya huruma yake isiyo na ukomo kwa kukamilisha hitaji hili la Allah; mwanadamu kuuweka upendo wake kwa Allah na kujaribu kujipendekeza ili apandwe na Yeye kupitia kumuabudu Allah.
d. Utumwa (Servitude): Kufahamu kwamba Allah, ambae ni Mkarimu, huwapa watu neema zisizo na ukomo za kimwili na za kiroho pamoja na kuvielekeza viungo vya hisia vya kimwili na vya kiroho vya watu, anataka avipe raha viwiliwili na akili; na hivyo basi, kupeleka sifa na shukran zake kwa Allah kupitia vitendo, maneno na fikra kwa kadri awezavyo.
e. Utumwa (Servitude): Kusema Subhanallah, Alhamdulillah, Allahuakbar”  (Ametukuka Allah, Shukran zote zinamstahikia Allah, Allah ni mkubwa) kwa ajili ya kumtukuza Allah juu ya utukufu wake (majesty) na uzuri wake (beauty), ambapo mfano wake unaonekana kila mahala kuanzia chembe ndogo ndogo (atoms) hadi maumbo makubwa (galaxies); kusimama, kurukuu na kusujudu mbele ya uwepo wake.
Kwa kuongezea, utumwa umegawika katika makundi mawili makubwa ambayo ni kuabudu na kuhudumia: funga, kuswali, kutekeleza nguzo ya Hijja, zaka ambapo zote hizi ni mifumo ya ibada; kuzalisha utaalamu wa aina zote wa kiteknolojia ambao unarahisisha maisha nayo pia huzingatiwa kama ibada. Kwa mfano, kutengeneza gari, kuunda meli, kutengeneza barabara na madaraja, kuanzisha viwanda ambavyo vitatoa bidhaa kadhaa za kiteknolojia vile vile nayo huzingatiwa kama ibada. Ni umuhimu usio na shaka kuazimia kupata radhi za Allah na kuwa mkweli hasa ikiwa mtu anataka ibada zake zikubaliwe.
Maswali juuyau islamu

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU