01-Ruqyah Ya Shariy'ah Na Hukmu Zake


 Ruqyah: Kinga Na Tiba Katika Shariy'ah

Ruqyah Ya Kishariy’ah Na Hukmu Zake


 
Maradhi  na  madhara yoyote yale hayamsibu mtu isipokuwa kwa majaaliwa ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa), lakini kwa rahmah Yake ‘Azza wa Jalla, Amejaalia shifaa (poza) kwa kila maradhi na kila dhara, kwa kutumia ruqyah pamoja na tiba ya Sunnah, na pia kutokana miti na majani kadhaa ambayo Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Amejaalia kuwa ina tiba ndani yake kwa dalili:

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه عَنِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((مَا أَنْزَلَ اللَّهُ دَاءً إِلاَّ أَنْزَلَ لَهُ شِفَاءً)) رواه البخاري   
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Allaah Hakuteremsha maradhi isipokuwa Ameyateremshia shifaa)) [Al-Bukhaariy]

Pia:
وعَنْ جَابِرٍعَنْ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم؛ أَنَّهُ قَالَ: ((لِكُلِّ دَاءٍ دَوَاءٌ، فَإِذَا أُصِيبَ دَوَاءُ الدَّاءِ بَرَأَ بِإِذْنِ اللَّهِ عَزَّ وَجَلَّ)‏) رواه مسلم  
Imepokelewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Kuna dawa kwa kila maradhi, na pindi dawa inapotumiliwa katika maradhi huponyesha kwa idhini ya Allaah ‘Azza wa Jalla)) [Muslim katika Kitaab As-Salaam]

Pia:

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ ابن مَسْعُدٍ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((إِنَّ اللَّهَ عَزَّ وَجَلَّ لَمْ يُنْزِلْ دَاءً إلاَّ  أَنْزَلَ لَهُ شِفَاءً عَلِمَهُ مَنْ عَلِمَهُ، وَجَهِلَهُ مَنْ جَهِلَهُ))
Kutoka kwa Ibn Mas’uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika Allaah ‘Azza wa Jalla) Hakuteremsha maradhi ila Ameteremsha pamoja nayo shifaa, amejifunza aliyejifunza na amekuwa jahili aliyekuwa jahili kwayo)) [Musnad Ahmad (6/121) kwa isnaad Swahiyh. Taz. Majmuw’ Fataawa Ibn Baaz (1/171), (6/290)]


Imekatazwa kutumia dawa za haraam kwa dalili:

عَنْ أَبِي الدَّرْدَاءِ (رضي الله عنه)  قَالَ:  قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((إِنَّ اللَّهَ أَنْزَلَ الدَّاءَ وَالدَّوَاءَ، وَجَعَلَ لِكُلِّ دَاءٍ دَوَاءً، فَتَدَاوَوْا ولاَ تَدَاوَوْا بِحَرَامٍ))
Kutoka kwa Abuu Ad-Dardaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika Allaah Ameteremsha maradhi na dawa zake, Akajaalia kwa kila maradhi kuna dawa yake, basi jitibuni wala msijitibu kwa yaliyo haraam)) [Abuu Daawuwd, Ibn Hajar Al-‘Asqalaaniy ameipa daraja ya Hasan, Taz. Takhiryj Mishkaat Al-Maswaabiyh (4/272), Imaam Al-Albaaniy ameisahihisha katika Swahiyh Al-Jaami’ (1762) au (2390)]

Inafaa kusoma Suwrah au Aayah ambazo imepatikana dalili zake, lakini Qur-aan nzima ni shifaa kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَنُنَزِّلُ مِنَ الْقُرْآنِ مَا هُوَ شِفَاءٌ وَرَحْمَةٌ لِّلْمُؤْمِنِينَ ۙ وَلَا يَزِيدُ الظَّالِمِينَ إِلَّا خَسَارًا ﴿٨٢﴾
Na Tunateremsha katika Qur-aan ambayo ni shifaa na rahmah kwa Waumini; na wala haiwazidishii madhalimu isipokuwa khasara. [Al-Israa 17: 82]

Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

يَا أَيُّهَا النَّاسُ قَدْ جَاءَتْكُم مَّوْعِظَةٌ مِّن رَّبِّكُمْ وَشِفَاءٌ لِّمَا فِي الصُّدُورِ وَهُدًى وَرَحْمَةٌ لِّلْمُؤْمِنِينَ ﴿٥٧﴾
Enyi watu! Kwa yakini yamekujieni mawaidha kutoka kwa Rabb wenu, na shifaa ya yale yaliyomo vifuani, na mwongozo na rahmah kwa Waumini. [Yuwnus 10: 57[

‘Ulamaa wamejuzisha ruqya pindi ikipatikana masharti matatu ambayo ameyanukuu Al-Haafidhw Ibn Rajab (Rahimahu-Allaah):
  1. Iwe kwa maneno ya Allaah (Ta’aalaa) au kwa Majina Yake na Sifa Zake.
  2. Isomwe kwa lugha ya Kiarabu.
  3. Aitakidi kwamba si ruqya pekee ndiyo itakayomponyesha bali aitakidi kwa uwezo wa Allaah (Ta’aalaa).
Pia zifutazo ni nukta muhimu Muislamu azingatie kabla ya kufanya ruqyah:

1-Uitakidi moyoni mwako kwamba njia yoyote uitumiayo ikiwa ni ruqyah, au kutumia dawa, hakupatikani shifaa isipokuwa kwa uwezo wa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Kwa hiyo uanze kumuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Pekee ili Akutakabalie ruqyah yako.


2-Unaweza kutumia Aayah na du’aa za Qur-aan na Sunnah madamu tu hutozitumia kwa kuziwekea idadi maalumu, au wakati maalumu ambavyo haikupatikana dalili, au kutumia njia nyinginezo kama kuweka kwenye hirizi, au kutundika mahali n.k. ambapo itakuingiza katika shirki. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameonya hayo aliposema:

عَنْ عَوْفِ بْنِ مَالِكٍ الأَشْجَعِيِّ قَالَ: كُنَّا نَرْقِي فِي الْجَاهِلِيَّةِ فَقُلْنَا يَا رَسُولَ اللَّهِ، كَيْفَ تَرَى فِي ذَلِكَ؟ فَقَالَ: ((اعْرِضُوا عَلَيَّ رُقَاكُمْ لاَ بَأْسَ بِالرُّقَى مَا لَمْ يَكُنْ فِيهِ شِرْكٌ))
Kutoka kwa ‘Awf bin Maalik Al-Ashja’iyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: “Tulikuwa tunafanya ruqyah katika zama za jahiliyyah, tukasema: Ee Rasuli wa Allaah,  unaonaje katika hayo (ruqyah yetu]? Akasema: ((Nionyesheni ruqyah yenu, hakuna ubaya katika ruqyah madamu tu haitokuwa na shirki)) [Muslim katika Kitaab As-Salaam, Abuu Daawuwd katika Kitaab Atw-Twibb]

3-Akipenda mtu, anaweza kubakia katika kutawakkal kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Pekee bila ya kujizingua au kuomba kufanyiwa ruqyah kama ni mojawapo ya fadhila za kumuingiza mtu Jannah bila ya kuhesabiwa kama alivyosema  Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

عَنْ ابْنِ عَبَّاسٍ (رضي الله عنهما)  أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((يَدْخُلُ الْجَنَّةَ مِنْ أُمَّتِي سَبْعُونَ أَلْفًا بِغَيْرِ حِسَابٍ: هُمْ الَّذِينَ لاَ يَسْتَرْقُونَ ولاَ يَتَطَيَّرُونَ وَعَلَى رَبِّهِمْ يَتَوَكَّلُونَ))
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Wataingia Jannah kati ya Ummah wangu watu elfu sabini bila ya hesabu; hao ni wale ambao hawaombi kufanyiwa ruqyah, wala hawatabirii nuksi au mkosi, wala kujitibu kwa moto, bali wanatawakkal kwa Rabb wao tu.)) [Al-Bukhaariy, Muslim]


​Tunaona kwenye Hadiyth hiyo kuwa, ni bora zaidi mtu kujizuia kuomba kufanyiwa ruqyah -  japo ni jambo lenye kuruhusiwa-, lakini ni bora zaidi kuacha kuomba kufanyiwa ruqyah na kuwa ni mwenye kutawakkal kwa Allaah, kwa sababu hiyo ni katika sababu ya kupata Pepo.


4-Ujiepushe  na kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kinyume chake ni kudumisha Tawhiyd ya Allaah (kumpwekesha) kwa Ar-Rubuwbiyyah (Uola), Al-Uluwhiyyah ('Ibaadah), na Asmaa wasw-Swifaat (Majina na Sifa Zake).

5- Ujiepushe na maasi na ubakie katika utiifu wa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa).


5-Udumishe Adhkaar za asubuhi na jioni, na Adhkaar za kulala kwa mfululizo bila ya kuacha  hata baada ya kupata tiba ili ujikinge kutokurudiwa tena kudhuriwa na viumbe viovu na shari zao.


6-Uvute subira na ukumbuke fadhila za kuvuta subira ili zikusaidie kuvumilia madhara yaliyokusibu.


7-Uanze kusoma ruqyah kwa thanaa - kumtukuza na kumsifu Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na kufuata adabu za kuomba du’aa  ili itakabaliwe ruqyah yako.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU