Unashindwa Kuweka Akiba Ya Kipato Chako Kidogo? Tumia Njia Hizi..!!!


“Kweli natafuta na napata… lakini fedha hazitoshi kabisa…”. Hizo ni kawaida kuzisikia kauli hizi katika maisha ya kila siku ya watanzania wengi hususan huku uswahilini kwetu ambapo wengi tunafanya kazi za kipato cha chini.

Ingawa kuweka akiba ni mtihani mkubwa kwa watanzania wengi, lakini ni mtihani mgumu zaidi kwa wananchi wa kipato cha chini ambao maisha yao yanategemea sana kile wanachokipata, lakini hata wanapokipata huwa hakitoshi siku zote.

Kwa bahati mbaya utamaduni wa kuweka akiba kwa wananchi wengi nchini ni utamaduni mgumu kuuishi, hii inatokana na mtazamo wa wengi kuwa akiba ni fedha inayowekwa kutokana na ‘ziada katika kipato’ cha mtu fulani. Mtazamo huo ni kikwazo kikuu cha kwanza, kwa kuwa kama unataka kuweka akiba lazima ujenge tabia ambayo baadae itakuwa utamaduni wako (mtindo wa maisha) wa kuweka akiba.

Tunapaswa kufahamu kuwa kipato kinachoitwa cha ‘ziada’ hakina maana ya kuwa ‘kimezidi’, hivyo kutokuwa na pato la ziada kwenye pato kuu kisiwe kigezo cha kwanza cha kutoweka akiba. Lakini hili halitawezekana kama hautajenga utamaduni wa kuweka akiba na kuuishi utamaduni huo.  Yaani kuweka akiba kuwe sehemu ya maisha yako.

Ni muhimu sana kuweka akiba, hiyo nilijifunza kutoka kwa bibi yangu ambaye hivi sasa amepumzika (Apumzike kwa Amani), ambaye alikuwa akiweka kibubu kwa kufukia kwenye sakafu ya udongo ya nyumba yake ya nyasi. Alikuwa na kipato kidogo sana na kisichotabirika, lakini ilikubidi uwe na maelezo ya kutosha kumshawishi kukigusa kibubu chake.

Ingawa nilimuona kama bahili kwa kuwa nilikuwa najua kuna sarafu anapata kutokana na kilimo chake cha mihogo kupitia shamba lake dogo, kila alipokivunja kibubu chake tulitabasamu muda wote na kusahau machungu kwani alifanya vitu vya maendeleo na kutimiza lengo fulani.

Kwa maisha ya sasa, njia hiyo inaweza kuwa ‘kituko’ lakini unaweza kutumia njia mbadala kwa lengo lilelile.

Hii ni namna ya kujenga utamaduni wa kuishi na kuweka akiba kupitia kipato kidogo unachokipata. Kama kipato chako ni kidogo sana, ukizifuata hizi unaweza kuwa na uwezo wa kuweka akiba angalau kwa asilimia 10 ya pato lako kwa kila mwezi.

1. Kuwa na nidhamu ya fedha

Iheshimu kila sarafu unayoipata. Tengeneza bajeti yako na utafakari kwa kuweka vipaumbele vya mahitaji yako kulingana na kipato. Hakikisha hautumii fedha bila kuwa na sababu za msingi na kujiridhisha kuwa unahitaji kutumia kiasi hicho cha fedha.

Hii ndio maana ya kuwa na nidhamu katika matumizi ya fedha kwa kuwa ingawa unao uwezo wa kutumia chochote ulichonacho bila kuhojiwa, bado unaweza kutengeneza ‘bunge’ kichwani kwako na kujadili mantiki ya matumizi husika.

2. Weka Malengo yanayopimika, yategemeze na akiba yako

Ili uwe na nguvu ya kuweka akiba, unapaswa kuweka malengo muhimu unayotakiwa kuyafikia katika kipindi fulani. Hakikisha malengo hayo yanapimika na yanatekelezeka endapo utaweza kuweka akiba kwa kipindi hicho. Ukiweka lengo kubwa sana, unaweza kukata tamaa baada ya kugundua hautaweza kutekeleza bila kujitesa sana au kwa muda uliopanga.

Malengo yanayopimika yatakupa nguvu ya kuweka akiba yako ndogo kwa kuwa utakuwa unaona jinsi unavyoyasogelea malengo yako kwa kupima ongezeko la akiba husika. Kumbuka kila ongezeko katika akiba yako lina maana kubwa sana kuliko kile unachokitumia kikakwisha.

3. Jitenge na Kipato chako

Ingawa wewe ndiye msimamizi na mdhibiti wa fedha zako, unapaswa kujitenga na fedha zako na kuhakikisha kuwa unakuwa msimamizi unayezitendea haki fedha hizo. Usiishi kwa kufuata kile anachofanya mtu fulani. Kama unapenda kile anachokifanya, jaribu kutafakari, weka kwenye mpango wako, kipime na anza kukifanyia kazi.

Kumbuka kuwa fedha unazoweka akiba, usipojitenga nazo na kuzichukulia kama ni fedha unazodaiwa kwa ajili ya kukamilisha jukumu au lengo fulani muhimu, utazitumia aghalabu.

4. Jipunguzie Kipato kwa Asilimia

Kwa kipato chako kuwa kidogo hakimaanishi hupati kabisa, au ndio kipimo cha mwisho cha kipato chako. Kumbuka utatumia kulingana na kile unachoingiza. Hivyo, kuwa na utaratibu wa kujipunguzia kipato chako angalau kwa asilimia 10. Asilimia hizo uzihamishie kwenye kibubu chako cha muda mrefu cha malengo makubwa. Hata kama umechukua mkopo kwa ajili ya kitu fulani, tumia njia hii kuweka akiba. Wakati unamaliza kurejesha mkopo wako, kibubu chako kitakuwa mtaji mpya.

5. Kaa Mbali na Kibubu chako!

Kwa usili ya binadamu yoyote, tamaa ni sehemu ya maisha yetu, ila tunazidiana kiwango cha tamaa. Unapotamani kuwa na kitu fulani, mara nyingi unajiangalia mifukoni. Hivyo tamaa ya jambo fulani ikikuzidia, unaweza kujikuta ukivunja kibubu chako kabla ya muda muafaka kwa sababu tu kiko karibu na wewe.

Tafuta namna nzuri ambayo itakuwa rahisi zaidi kwako kuweka pesa hiyo lakini vigumu sana kwako kuichukua.

Kwa mfano wa kawaida tu, unaweza kufungua akaunti Benki, kisha ATM Card ukaiacha kwa mtu unaemuamini mkoa fulani, mtu huyo asifahamu ‘password yako’ lakini pia mwambie lengo lako. 
Wakati yeye hajui password ya ATM Card yako japo anayo (Hasa zile zenye picha), wewe pia unafahamu password lakini huna uwezo wa kuchukua pesa bila ATM Card yako. Ugumu huo unaweza kukusaidia wewe kwa hali ya kawaida kabisa.

Hata hivyo, hivi sasa kuna mifuko mingi ya kijamii pamoja na njia za kibenki ambazo ni salama zaidi ambazo zitakufanya kuweka pesa kwenye akaunti yako lakini huwezi kuichukua kwa muda fulani, na utakapofikisha muda muafaka unapata riba ya asilimia kadhaa.

Kumbuka usipoweka akiba huku unawaza maendeleo makubwa, ni kama unakimbiza upepo. ‘Akiba Haiozi’.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU