JINSI ya Kutumia Fedha Kidogo Kufanikisha Makubwa Katika Hali ‘Ngumu’..!!!


Katika maisha ya kawaida ya Watanzania tulio wengi, kwa namna moja ama nyingine umewahi kusikia au wewe binafsi kulalama kuwa pesa yako haikai au haiendi kama unavyotegemea. Hiki ni kilio cha kawaida ambacho hakitokani na kutapanya fedha bali kutojua mbinu sahihi ya kawaida tu ya kuzitumia vyema pesa ‘kidogo’ kupata matokeo makubwa.

Moja kati ya tabia ya fedha hasa hizi tunazopata watu wa kima cha chini ni kwamba huwa ni kama zinayaita matatizo au matumizi, pindi tunapokuwa nazo. Yaani mambo yanaweza kwenda tofauti na ulivyokuwa umepanga, matumizi yanaongezeka kidogo-kidogo ila unashtuka umebaki na kisalio ‘kiduchu’ au hata umefilisika kabisa. Ndio hapo kilio cha ‘mishahara haikutani’ kinazidi.

Leo tutakupa mbinu ya namna ya kubadili kidogo mtindo wako wa maisha bila kujibana bali kubana mianya ya kutumia fedha zako bila kufuata mipango uliyojiwekea.

Epuka vishawishi vya ATM, Simu Pesa:

Jitahidi mara kadhaa kukwepa kutembea na ATM au kuweka fedha nyingi kwenye simu yako ya mkononi. Chukua kiasi fulani cha fedha taslimu uliyopanga kutumia siku hiyo au wiki hiyo, ongeza na kiasi kidogo tu cha ‘dharura’. Hii ni kwa ajili ya mahitaji ya kawaida. Itakusaidia kuepuka kutumia fedha za akiba mara kwa mara pale uonapo kitu bila mpangilio kwa sababu tu unajua utaingia ATM na kuchomoa au utaivuta kutoka Simu pesa.

Itakusaidia kukwepa pia kuwapa ofa rafiki na jamaa kwa ‘mizuka’, hasa baada ya kupata kilevi. Hatusemi usiweke fedha kwenye simu, bali usiweke kiasi kikubwa kama akiba tu na kutembea nazo. Hakika utazitumia bila kupanga kama huna msimamo wa ‘bahiri’. Kumbuka kutumia ATM/ simu pesa mara kadhaa unaongeza makato ya fedha kwa huduma.

Epuka tabia za ‘nunua sasa lipa baadae’

Kampeni za ‘nunua sasa, lipa baadae’ zina msaada mkubwa kwa watu wenye mahitaji fulani kwa wakati huo lakini wanategemea kupata fedha baadae kidogo. Lakini ni hatari zaidi kwa usawa huu kwani ni rahisi kunogewa kuchukua vitu ambavyo sio vya lazima sana ukiiwaza fedha ya baadae bila kuweka akilini kuwa hiyo baadae pia itakuwa na mahitaji yake.

Jitahidi kutumia fedha kutoka kwenye mfuko uliopo sasa kama suala hilo sio la lazima sana kwa wakati huo, kama ni kiatu kizuri, kumbuka kinaweza kupatikana kizuri zaidi wakati ujao na ukakilipia kulingana na pesa itakayokuwepo kwa mazingira hayo.

Usifuje pesa yako kwenye majina ya bidhaa

Hakikisha unanua bidhaa unayoihitaji kwa gharama ambazo unaweza kuzimudu bila kufuata mkumbo wa jina la duka fulani. Usitafute jina tu kuwa umeweza kununua sehemu fulani kama fulani. Fikiria kwanza kama bidhaa hiyo haiwezi kupatikana sehemu nyingine unayoweza kufika na kupunguza gharama. Zingatia pia uhalisia wa ubora wa bidhaa husika ili isije kugeuka hasara kubwa na kukugharimu zaidi.

Andaa, pitia na ifanyie tathmini bajeti yako

“Mali bila daftari, huisha bila habari”. Hakikisha sio tu kwamba unaandaa bajeti ya matumizi yako ya mwezi, lakini pia ifanyie mapitio wakati wa matumizi na ifanyie pia tathmini kama umeitumia ipasavyo. Hii itakusaidia kuondoa matumizi yasiyo ya lazima na kujiwekea kiwango cha wastani wa matumizi yako ili kupata nafasi ya kuweka akiba kwa ajili ya maendeleo na mambo mengine makubwa.

Usiogope kuahirisha

Unapaswa kufahamu kuwa kuna wakati inakulazimu kuahirisha mpango wa kufanya matumizi fulani sio kwa sababu hauna fedha inayotosha, bali matumizi ya pesa hiyo yatakupa ukata wa haraka na kilio kabla ya kupata nyingine.

Kama ni hivyo, usiogope kuahirisha mpango wako mzuri. Ni vyema ukaahirisha na kujiandaa vizuri zaidi ili uweze kumudu kufanya matumizi hayo husika bila kilio cha baadae. Kuahirisha kwa sababu za msingi ni bora kuliko kulazimisha kwa shida ya kipindi.

Kumbuka, hakuna fedha nyingi bila fedha ndogo, unapotumia fedha kwa matumizi unayoyaita madogo tu fahamu kuwa unabandua sehemu ya gogo lako. Hivyo, halitakuwa kama ulivyotaka kwa muda husika.

Ukitoa shilingi moja kwenye milioni moja haitaitwa tena milioni moja. Kuwa na nidhamu ya fedha, ni siri ya mafanikio hasa kwenye kipindi kigumu cha maisha.

Hii ni sehemu tu ya unayopaswa kuyafanya kuepuka matumizi yasiyo ya lazima.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU