VIDEO: Tazama A-Z Jengo la Ghorofa lilivyowaka Moto Kariakoo
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
Leo Novemba 2 moja ya jengo lililopo mtaa wa Livingston na Pemba, Karikaoo jijini Dar es salaam limewaka moto ghorofa ya nne ambapo mpaka sasa chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana.
Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo ...
WADAU mbalimbali wa mchezo wa ngumi wamemtaka bondia, Hassan Mwakinyo, kumwomba radhi bondia mkongwe hapa nchini, Rashid Matumla "Snake Boy" kutokana na kitendo chake cha kumponda kutokana na uchambuzi aliokuwa akiufanya wakati wa pambano lake dhidi ya Mfilipino Arnel Tinampay likiendelea. Rashid Matumla 'Snake boy' ni nguli wa masumbwi Tz alilalamika sana juu uwezo wa Mwakinyo kiufundi, uvumilivu na mambo mengine ikafika pahala akapandwa na hasira kutokana na approach ya game (Muda mwingi yupo kwenye kamba, kitu kilichomfanya kumpa nafasi Tinampay kumshambulia na kumpunguza nguvu za miguu kwa kumpiga mbavuni). Kwa tukio kama lile Chid kuzungumzia issue ya kocha wake si dhambi kwa kuwa anaexperience nazo, Hivi kwamba Chid hazijui ngumi zinazotoa points kama sisi wandengeleko? Mwakinyo alikosa vitu vingi kwanza hanyumbuliki, poor coordination yawezekana katika maandalizi yake alikimbia sana kwenye vilima au kwenye ngazi kutafuta stamina pamoja na pumzi ikamchosh...
Na Amiri kilagalila Njombe TAZAMA VIDEO HII KISHA SUBSCRIBE YOUTUBE Mwanaume aliyefahamika kwa jina la Sosteni Myamba (44) mkazi wa kijiji cha Itipingi halmashauri ya wilaya ya Njombe mkoani Njombe inasemekana ameuawa kwa kupigwa nyundo kwa madai ni kutokana na imani za kishirikina. Mwenyekiti wa kijiji cha Itipingi Ayubu Mgeni amethibitisha hilo na kufafanua kuwa marehemu huyo alikuwa na tabia ya kuwatuhumu baadhi ya ndugu akiwemo baba yake mzazi kuwa ni mshirikina hali ambayo imepelekea kuibuka kwa mgogoro ndani ya familia hiyo. Kiongozi wa familia hiyo Aidani Myamba amesema marehemu alikuwa ana matatizo ya akili hali ambayo ilimfanya awe mtu wa kutuhumu wengine kuwa wanajihusisha na imani za kishirikina. Hata hivyo Jacob Myamba ambaye ni mdogo wa marehemu huyo anashikiliwa na jeshi la polisi wilaya ya kipolisi makambako kwa tuhuma za kuhusika na mauaji hayo.
Comments
Post a Comment