VIDEO: Tazama A-Z Jengo la Ghorofa lilivyowaka Moto Kariakoo
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
Leo Novemba 2 moja ya jengo lililopo mtaa wa Livingston na Pemba, Karikaoo jijini Dar es salaam limewaka moto ghorofa ya nne ambapo mpaka sasa chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana.
Nia: Nia ni sharti la swala kuwa sahihi, kwa maana ya mtu kukusudia kwa moyo wake kumuabudu Allah kwa kuswali, huku akijua kwamba swala anayoswali ni Magharibi kwa mfano au Isha. Haitakiwi na sheria kuitamka hii nia, bali makusudio ya moyoni na akilini ndio yanayotakiwa. Kuitamka Nia ni jambo ambalo hilo halikuthibiti kunukuliwa kwa Mtume,swallalahu alayhi wasalam, wala maswahaba wake watukufu. Atasimama wima kwa ajili ya swala na kusema: (Allahu Akbar). Atanyanyua mikono yake mpaka usawa wa mabega yake au juu yake huku matumbo ya viganja vya mikono akiyaelekeza upande wa Kibla. Takbira haiwi sahihi isipokuwa tu kwa tamko hili la (Allahu Akbar). Maana yake ni kumtukuza na kumuadhimisha Allah. Allah ni mkubwa zaidi kuliko kila kisichokuwa yeye. Ni mkubwa zaidi kuliko dunia pamoja na starehe zote na matamanio yote yaliyomo humo. Tunaziweka kando starehe zote hizo na tunaelekea kwa Allah mkubwa, mtukufu katika swala kwa nyoyo zetu na akili zetu huku tukiwa wanyenyekevu...
Msikiti Mtukufu unapatikana katika mji wa Makka, magharibi ya rasi ya Arabuni. Katika Uislamu, msikiti huu una sifa nyingi takatifu za kipekee, na miongoni mwa sifa hizo ni hizi: Ndani ya msikitini wa Makka kunapatikana Kaaba Takatifu: Kaaba ni jengo la pande nne na takriban lenye umbo la ujazo. Ipo katikati ya Msikiti Mtukufu katika mji wa Makka. Kaaba ndio Kibla ambacho Waislamu wanaelekea hapo wakati wa kuswali, na wakati wa kufanya ibada nyingine ambazo Allah ameziamrisha. Nabii Ibrahimu kipenzi cha Allah na mwanawe Ismail, Allah awafikishie rehema na amani, ndio walioijenga kwa amri ya Allah Mtukufu, kisha jengo lake limefanyiwa maboresho mara nyingi. Allah amesema kuwa: «Na (kumbukeni) wakati Ibrahimu alipoinua kuta za nyumba (Kaaba yeye na) na Ismaili wakasema: Ewe Mola wetu, tukubalie. Hakika, wewe tu ndiye mwenye kusiki, mwenye kujua». (Sura Abaqara, aya 127) Mtume Muhammad,swallalahu alayhi wasalam, alishiriki yeye na makabila ya Makka katika...
UTANGULIZI Ibraahiym عليه السلام alizaliwa Iraq, inavyosemekana Babylonia . Baba yake akiitwa Aazar na kauli nyingine inasema kuwa huyu ni ami yake aliyemlea tokea mdogo baada ya kufa baba yake. Allaah سبحانه وتعالى Anajua zaidi. Na huyu Aazar alikuwa akichonga masanamu. Ibraahiym عليه السلام ni Khaliylul-Allaah yaani 'rafiki mwendani wa Allaah' Amemchagua kumpa ujumbe na Akamfadhilisha zaidi ya viumbe Vyake vingine. Alikuwa akiishi na watu waliokuwa wakiabudu sayari (nyota, mwezi, jua na kadhalika), na wengine wakiabudu masanamu na wengine wakiabudu wafalme wao. Hakuridhika na ibada hizo zao, bali alihisi kuwa yupo Aliyeanzisha maumbile yote na kwamba kuna Mungu Mtukufu Anayestahiki kuabudiwa. Akawa anawaza na kutafuta uhakika hadi Allaah سبحانه وتعالى Akamhidi na kumchagua kumpa utume. Akaanza Ibraahiym عليه السلام kuwaita watu wake katika Tawhiyd yaani ibada ya kumuabu Allaah Pekee, lakini ha...
Comments
Post a Comment