Usitafute Dosari Za Mwenzio

Hakuna mtu aliyekamilika. Watu wengine ni warefu sana au wafupi sana au wanene sana au wembamba sana, wanapua kubwa au pua ndogo, wanasema sana au wakimya sana, wana hasira zana au wanaelewana na watu haraka sana weusi sana rangi ya wastani au wanakula sana au wanakula kidogo na orodha inaweza kuendelea. Wanaume na wanawake wengi sana wanazo dosari hizi. Ni matumaini ya kila mwanaume na kila mwanamke kutafuta mwenzi aliyekamilika, lakini matumaini ya aina hiyo si sahihi. Hakuna uwezekano wa kumpata mwanamke anaye muona mumewe kama mtu aliye kamilika.
Wanawake hao ambao hutafuta makosa ya waume zao bila shaka watayapata.
Wanaweza wakaona dosari ndogo na kuzikuza kwa kushughulikia jambo hilo hadi kiwango cha kuwa kipingamizi kisichovumilika. Dosari hii huchukua nafasi ya sifa zingine zote za mume. Kila mara huwalinganisha waume zao na wanaume wengine. Wameanzisha kitu kinachoitwa mwanaume anayefaa katika dhana yao kiwango ambacho hakiafikiani na waume zao. Kwa hiyo, kila mara wanalalamika kuhusu dosari ndani ya ndoa zao. Wanawake hao hujifikiria kuwa na bahati mbaya na kushindwa na maisha na pole pole huwageuza kuwa wanawake |wenye chuki.
Tabia ya aina hiyo ya mwanamke humfanya nini mumewe? Anaweza kuwa ni mtu mvumilivu sana ambaye anaweza kustahamili ujeuri lakini upo uwezekano mkubwa atafedheheshwa na atakuwa na kinyongo kwa mkewe.
Hali hii inawezekana ikawatumbukiza wanandoa husika kwenye mabishano na kuelezana dosari za kila mwanandoa. Wote wawili watadharauliana na maisha yao yatageuka kuwa na mlolongo wa ugomvi na mabishano. Hivyo, ama wataishi katika mateso wakiwa pamoja au wataamua kutalikiana. Katika hoja zote mbili, wote watahasarika, hususan ambapo hakuna uhakikisho kwamba ndoa nyingine inaweza kuthibitisha vinginevyo.
Inasikitisha kwamba wapo wanawake wasiojua na wanakaidi katika huo ujinga wao. Inawezekana kwamba wanaweza kuharibu maisha ya familia zao kwa jambo dogo. Ifuatayo ni mifano ya wanawake wa aina hiyo: “Mwanamke alimwacha mume wake na akaenda nyumbani kwa baba yake kwa sababu mume wake alikuwa ananuka mdomo. Mwanamke huyo hakuwa tayari kurudi kwa mumewe hadi atatue tatizo lake. Kufuatana na malalamiko ya mume, mahakama iliwasuluhisha wana ndoa hao na mke akarudi kwa mumewe. Walipokwenda nyumbani, mke aligundua kwamba pumzi ya mumewe ilikua bado inanuka, kwa hiyo alihamia chumba kingine.”
“Daktari wa meno mwanamke alimtaliki mume wake kwa sababu hakuwa katika kiwango kinacholingana na cha kwake; mwanaume alifuzu na kupata taaluma hiyo miaka mitatu baada ya mke wake.”
“Mwanamke aliomba kumtaliki mume wake kwa sababu alikuwa na desturi ya kuketi chini na kula kwa kutumia vodole vyake, alikuwa hanyoi kila siku na hakujua jinsi ya kuishi na watu.”
Kama mambo yalivyo, si kwamba wanawake wote wapo hivi. Wapo wanawake wenye akili, wa kweli, na wanao utambuzi wa kutosha kwamba hawa hatarishi ndoa na furaha kwa kukuza dosari za waume zao. Mpendwa Bibi! Mumeo ni binadamu kama wewe. Hakukamilika, lakini anaweza kuwa na sifa nyingi. Kama unapendezwa na ndoa yenu na familia yenu basi usitafute udhaifu wake.
Usifikirie dosari zake ndogo kuwa muhimu. Usimlinganishe na mwanaume huyo ambaye umembuni akilini mwako. Inawezekana mumeo awe na udhaifu fulani ambao haupo kwa wengine. Lakini kumbuka kwamba wanaume wengine wanaweza kuwa na kasoro ambazo hazipo kwa mumeo. Ridhika na sifa zake. Hatimaye, utaona kwamba sifa zake zinazidi dosari zake. Zaidi ya hayo kwa nini utarajie kumpata mume mkamilifu ambapo wewe mwenyewe si mkamilifu. Kama wewe unajivuna kiasi cha kutosha kujiona wewe ni mkamilifu, basi waulize watu wengine:
Mtume (s.a.w.w) alisema: “Hakuna kitu kibaya zaidi kwa binadamu kuliko kutafuta dosari za watu wengine, ambapo hawajali mapungufu yao.”
Kwa nini ukuze dosari ndogo? Kwa nini uharibu maisha yako kwa kitu kisichokuwa maanani?
Uwe na busara, acha upuuzi! Puuza dosari za mumeo na usizitaje mbele yake au nyuma yake. Jaribu kutengeneza hali ya hewa ya uchangamshi katika familia yako na ufurahie neema za Mwenyezi Mungu.
Hata hivyo, inawezekana pawepo dosari katika tabia ya mumeo ambazo unaweza kuzirekebisha. Kama ni hivyo, unaweza kufaulu kufanya hivyo hapo tu ambapo utakuwa na busara na uvumilivu. Hutakiwi umlaumu au kuanza kumgombeza, lakini mwendee kwa njia ya kirafiki.

Usimwangalie Mtu Yeyote Isipokuwa Mumeo

Mpendwa Bibi! Kabla hujaolewa inaewezekana ulikwisha chumbiwa na watu wengine. Posa za uchumba huu inawezekana zilitoka kwa watu matajiri, wasomi, wenye sura nzuri na kadhalika ambao ungependa wakuoe.
Matarajio ya aina hiyo yalikuwa ni jambo la kawaida kabla ya kuolewa. Lakini sasa umechagua mwenzi wako na kuwekeana mkataba wa dhati naye kuwa wapenzi katika maisha yenu yote, hivyo, sahau yaliyopita kabisa. Lazima uyaweke pembeni matamanio yako ya zamani na usahau ofa hizo za zamani. Usimfikirie mwamanume mwingine yeyote isipokuwa mumeo na utafute amani naye. Kama ukifanya vinginevyo, utajiweka katika hali ya mashaka.
Sasa basi, umekubali kuishi na mumeo, kwa nini wakati wote uendelee kuwatilia maanani wanaume wengine? Kwa nini umlinganishe mumeo na wanaume wengine? Unapata manufaa gani unapowatazama na kuwatilia maanani wanaume wengine isipokuwa kujiweka katika hali ya mateso yasiyo na mwisho na kusababisha upate maumivu makali ya akili?
Imam Ali (a.s) alisema: “Yeyote anayeyaacha macho yake huru, kila mara atapata maumivu ya neva na atanasa kwenye mtego wa wivu wakati wote.”
Kwa kuwatazama waume wengine na kuwatilia maanani na kuwalinganisha na mumeo, utamuona mwanaume ambaye hana dosari za mumeo. Unaweza kudhani kwamba labda mwamaume huyo amekamilika kwa sababu huzijui dosari za mwanaume huyo. Utafikiria kuwa ndoa yako ina mushkeli, na fikira hii inaweza ikawafikisheni mahali penye mwisho wenye hatari.
Mke wa mtu, umri wake miaka 18 ambaye alitoroka nyumbani kwake alikamatwa na polisi usiku wa jana. Akiwa kituo cha polisi mwanamke huyu alisema kwamba baada ya miaka mitatu ya ndoa, pole pole alihisi kwamba hampendi mume wake. Alisema: “Nilikuwa na tabia ya kulinganisha uso wa mume wangu na nyuso za wanaume wengine na nikajuta kwa nini niliolewa naye.”
Mpendwa Bibi! kama unataka ndoa ya kudumu daima milele, kama hutaki mateso ya kiakili, na kama unataka muendeshe maisha ya kawaida, basi acha kuwa mbinafsi na sahau hayo matarajio yako yasiyofaa. Usiwapongeze wanaume wengine. Usimfikirie mwanaume yeyote isipokuwa mumeo. Usiendekeze fikira hizi:
‘Afadhali ningeolewa na fulani’
‘Ningependa mume wangu aonekane kama . . . . . .’
‘Natamaani mume wangu angefanya kazi ya. . .. . . . . .’
‘Natamaani….. Natamaani……. Natamaani….’
Kwa nini ujifunge jela kwa kuendekeza mawazo hayo? Kwa nini utibue misingi ya ndoa yako? Kama lolote kati ya matakwa hayo yangefanikiwa kwa kweli, ungejuaje kwamba ungefanikiwa kuridhika zaidi? Unao uhakika kwamba wake za waume wajulikanao kama ‘hawana dosari; wanaridhishwa nao?
Mpendwa Bibi! Kama mumeo anashuku kwamba unaonesha kuvutiwa na wanamume wengine, atakata tamaa na kuacha kuvutiwa na wewe. Usitaniane na wanamume wengine au kufuatana nao. Wanamume ni wepesi kuhisi hivyo kwamba hawawezi hata kuvumilia wake zao kuonesha kuvutiwa na picha ya mwanamume mwingine.
Mtukufu Mtume (s.a.w.w) alisema: “Mwanamke yeyote aliyeolewa ambaye huwatazama wanamume wengine atakabiliwa na adhabu kali ya Mwenyezi Mungu.”

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU

Kisa Cha Nabii Ibraahiym عليه السلام - Sehemu Ya 1