Rais Magufuli apiga simu LIVE kongamano la Sanaa la Mwalimu Nyerere likiendelea


Rais Magufuli amempigia simu rais wa Chama cha Muziki wa Injili Tanzania, Ado Novemba na kumwambia anafuatilia shughuli hiyo ya kongamano la Sanaa la Mwalimu Nyerere.

Kongamano la Sanaa la Mwalimu Nyerere linafanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es salaaam.

"Nakusikiliza usiwe na wasiwasi na maagizo yangu niliyoyatoa Waziri Mkuu atayawasilisha hapo kwenu, ninawapenda sana, wasanii oyeeee," alisema Rais Magufuli.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa anamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli katika Kongamano hilo.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU

Kisa Cha Nabii Ibraahiym عليه السلام - Sehemu Ya 1