Mfahamu Baharia wa Meli, Idara za Meli na Nafasi za Mabaharia Katika Meli


Baharia (Seafare) ni mfanyakazi yeyote katika meli.Katika meli kuna mabaharia ambao ni maofisa(Officers) na ambao si maofisa(Crew).

Meli ina idara kuu 3 kulingana na mgawanyo wa majukumu na vitengo.
1.DECK DEPARTMENT (Kuongoza meli)
2.ENGINE DEPARTMENT (Wahandisi wa meli)
3.CATERING DEPARTMENT ( Huduma za vyakula)

NAFASI ZA AJIRA 98 MPYA ZILIZOTANGAZWA BONYEZA HAPA



1. DECK DEPARTMENT
Hii ni idara inayohusika na uongozaji wa meli.Hawa ni mabaharia kuanzia maofisa mpaka wafanyakazi wa kawaida na majukumu yao.

Master/Captain (Nahodha)
Huyu ni kiongozi mkuu katika meli na yeye ndio msemaji wa mwisho. Ni mwakilishi wa mmiliki wa meli sehemu anapokuwa na meli. Ni mwakilishi wa nchi ambayo meli inapeperusha bendera iliyosajiliwa.

Majukumu yake ni kusimamia shughuli za kila siku za meli,hali ya amani katika chombo na kusaini documents kama bill of lading ya mzigo.Kusimamia sheria na taratibu kwa watu wote melini na kuwepo sehemu ya kuongozea na kutoa maagizo wakati wa meli kuingia na kutoka eneo la bandari.

Chief Officer
Huyu ni ofisa anayefuata baada ya nahodha wa meli, ana vyeti sawa na nahodha pia akifanya kwa kipindi kirefu anakidhi kupewa unahodha wa meli. Chief officer anaripoti kwa nahodha.

Majukumu yake ni kusimamia na kuandaa cargo plan, yeye ni incharge wa mabaharia wote walio chini yake. Kusimamia majukumu ya mawasiliano ya radio katika meli,matengenezo ya meli.

Second Officer
Huyu ni afisa anayefata baada ya Chief officer na anaripoti kwa Chief officer.
Majukumu yake ni kusimamia uchoraji wa route ya safari,ramani za safari na vifaa vya kuongozea meli. Huyu pia ni incharge wa vifaa vya mawasiliano ya radio na anafanya kazi kama afisa afya.

Third Officer
Huyu ni afisa anayefuata baada ya Second Officer.
Majukumu yake ni kusimamia vifaa vya uokoaji na vifaa vya kuzimia moto,kuandaa ripoti ya drill zifanyikazo melini, kumsaidia Chief Officer wakati wa kupakia na kupakua mizigo. Kusimamia sehemu za ufungaji kamba katika meli.

Deck Cadet
Huyu afisa mwanafunzi katika idara ya uongozaji meli. Anajifunza kazi na anakuwa chini ya uangalizi wa chief officer. Na anafanya kazi mbalimbali za usafi,kupaka rangi na kamba.

Mabaharia wasio maofisa

Bosun
Huyu ni kiongozi mkuu wa mabaharia wa kawaida melini.
Majukumu yake ni kusimamia usafi,upakaji rangi,kazi za kufunga kamba,kusimamia stoo na kumsaidia chief officer wakati wa kuweka nanga. Pia anaripoti kesi za utovu wa nidhamu za mabaharia kwa Chief Officer.

Able-Bodied Seaman (AB)
Huyu ni baharia wa kawaida ambaye majukumu yake ni usafi,kupaka rangi, kazi za kamba na kushika usukani wa meli pia kumsaidia afisa wa zamu wakati meli inapotembea.AB mzoefu anaweza akapanda mpaka kuwa Bosun.

Ordinary Seaman
Huyu majukumu yake ni usafi, kugonga kutu, kupaka rangi na kazi za kamba.
Huyu haruhusiwi kushika usukani meli inapotembea wala kukaa zamu sehemu ya kuongozea meli.

2. ENGINE DEPARTMENT
Hii ni idara inayohusisha wahandisi wa meli ambao ni maofisa na baharia wa kawaida wenye ujuzi wa ufundi wa meli.

Chief Engineer
Huyu ni kiongozi mkuu katika idara ya injini.
Majukumu yake ni kutoa oda na kusimamia kazi zote engine room. Kuandaa ripoti za kiufundi kuhusu meli kwenda kwa mmiliki.Kufanya mahesabu ya mafuta, kusimamia sheria eneo la chumba cha injini na kuripoti hali yoyote ya hatari kwa nahodha.

Second Engineer
Huyu ni injinia baada ya chief injinia.
Majukumu yake ni kumsaidia Chief injinia, incharge wa mashine zote kama injini, jenereta, pampu na steering gear.Kuandaa orodha ya marekebisho na kupanga ratiba ya marekebisho.

Third Engineer
Majukumu yake ni kusimamia na marekebisho ya jenereta, boiler, kuangalia mifumo ya boiler na maji.

Fourth Engineer
Majukumu yake ni kusimamia ujazaji mafuta na kumsaidia chief ofisa katika mahesabu ya mafuta. Kusimamia shughuli za mtambo wa maji taka, uchomaji taka, maji safi na mtambo wa kuchuja maji na oil.

Engine Cadet
Huyu ni afisa mwanafunzi katika idara ya injini na anakuwa chini ya usimamizi wa Second Officer. Majukumu yake ni usafi chumba cha injini na kusimamia uendeshaji wa injini meli inapotembea.

Mabaharia wa kawaida katika idara hii

Fitter
Huyu ana ujuzi wa kuchomelea, kukata vyuma,kutoboa na kuchomela kwa gesi. Huyu anafanya kazi chini ya Second officer.

Oiler
Huyu anafanya kazi za marekebisho katika injini, aawasaidia mainjinia wakati wa kufungua injini,kufanya usafi na kupaka rangi.

Wiper
Kazi yake kubwa ni kufanya usafi eneo la injini.Anafanya kazi ya kuwasaidia mainjinia wakati wa marekebisho ya injini.Akipata uzoefu wa kutosha hupewa nafasi ya oiler.

3.CATERING DEPARTMENT
Hii idara inashughulika na chakula na usafi wa maeneo ya kulia chakula (Mess).

Chief Steward
Majukumu yake ni kupanga ratiba za usafi wa mess, ratiba ya chakula na usimamizi. Pia anajukumu la kuangalia overtime za watu na kipindi cha nyuma yeye alikuwa akitumika kugawa posho na mishahara.

Chief Cooker
Huyu ni mpishi mkuu katika meli, majukumu yake ni kupika vyakula na kuandaa ratiba ya chakula. Kupika vyakula kulingana na mapishi ya mataifa mbalimbali ya wafanyakazi katika meli na kumsadia nahodha kutoa orodha ya mahitaji katika idara anayosimamia. Anapaswa ajue lugha na mapishi ya vyakula mbalimbali.

Stewards
Huyu ni msaidizi wa mpishi mkuu na anasaidia shughuli za kupika, kufanya usafi na kuandaa chakula. Pia anafanya kazi ya kufanya usafi vyumba vya maofisa, kusimamia ugawaji chakula.

Galley Boy
Huyu huwa baadhi ya meli kazi yake kubwa ni kuosha vyombo jikoni na kufanya usafi. Pia hushiriki kukata mboga, nyanya na vitunguu. Huwa ni mtu asiyepewa heshima sana na kudharaurika katika meli.

NAFASI ZA AJIRA 98 MPYA ZILIZOTANGAZWA BONYEZA HAPA

SARE ZA MABAHARIA
Mabaharia ambao ni maofisa huvaa shati yenye rangi nyeupe,bluu au kaki ikiwa na beji pembeni ya bega la kulia na kushoto. Wale wa upande wa uongozaji kuanzia Nahodha yeye huwa na alama ya nanga au usukani na mistari 4. Anayefuata mistari 3,2,1 na Cadet yeye mstari wake huwa ni mmoja uliolala.

Pia upande wa engine Chief engineer huvaa beji yenye alama ya propela ya meli na mistari 4, Second engineer 3, Third engineer 2, Fourth engineer 1 na Cadet engineer ni mstari 1 uliolala.

Kwa mabaharia wasio maofisa wao hawavai beji nguo zao begani huwa hazina kitu. Tisheti za mabaharia zote ni sawa kwa ngazi ya ofisa na wa kawaida.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU