Mchungaji akamatwa na pembe za ndovu


Jeshi la Polisi Mkoani Dodoma linawashikilia watu 22 kwa matukio tofauti ambapo watatu kati yao akiwemo mchungaji wa Kanisa la Aglikana Shekandi Ashery Mkombola (44) wanatuhumiwa kukutwa na nyara za Serikali vipande18 vya meno ya Tembo.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoani Dodoma, Gilles Muroto amesema watuhumiwa hao wa nyara za Serikali walikamatwa katika matukio mawili tofauti ambapo mchungaji huyo wa Kanisa la Kijiji cha Chinyika kilichopo Wilayani Mpwapwa amekutwa akisafirisha meno mawili ya Tembo yenye uzito wa kilogram 15.

“Mchungaji huyu alikamatwa katika Kijiji cha Pwaga kilichopo tarafa ya Kibakwe ingawa anaishi Kijiji cha Mungui na alikua akisafirisha meno hayo kwa kutumia pikipiki aina ya Fekon yenye namba za usajili MC 772 AYK,” amefafanua Muroto.

Amesema katika tukio la pili watuhumiwa wawili ambao majina yao yanahifadhiwa kwa sababu za kiupelelezi wamekamatwa katika stendi ya mabasi ya nanenane Jijini Dodoma wakiwa na vipande 16 vya meno ya Tembo wakitumia mbinu ya kuvificha katika dumu la lita 20 lililokatwa juu.

Katika tukio jingine Kamanda Muroto amesema Polisi inawashikilia watu wawili Sam Ally Isihaka (44) dereva wa gari aina ya benz lenye namba za usajili AIB 5596 na Mwinyi Ramadhani Magumila (47) dereva wa gari aina ya benz lenye namba za usajili AIB 6924 kwa kosa la kukwepa ushuru.

Amesema watuhumiwa hao wakiwa safarini kutoka Malawi kuelekea Rwanda walikwepa ushuru wa Serikali katika mizani ya Uyole Mbeya, Makambako Njombe na Wenda Tanangozi Iringa kwa kushawishi na kutoa rushwa kwa maafisa wa mizani.

“Maafisa hawa wa mizani nao walipokea rushwa na kutoa risiti bandia ili kuruhusu magari hayo mali ya kampuni ya Reginal Logistics ya Dar es salaam kupita bila kupima ambapo walikuwa wamezidisha uzito wa mizigo zaidi ya 650 gvm yaani gross vehicle mass,” amebainisha Kamanda Muroto.

Kufuatia tukio hilo Muroto amesema watuhumiwa sita wakiwemo maafisa wa mizani waliokuwa zamu katika vituo hivyo wanashikiliwa na Jeshi la Polisi na wanatarajia kufikishwa Mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.

Aidha katika tukio jingine Polisi inawashikilia watu kumi kwa makosa ya kuvunjwa na kuiba nyakati mbalimbali na kukutwa na mali za wizi flat screen TV 13, simu janja saba, home theater moja, laptop mbili, CPU moja na monitor moja.

Kamanda Muroto amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Amani Ally (26), Juma Said (22), Jumanne Ernest (21), Jafari Juma (25), Joseph Donald (30), Mena Ramadhani (52) na Rekresia Mchiwa (36) wote wakiwa ni wakazi wa Jijini Dodoma.

” Yupo pia mtuhumiwa Fatma Mchiwa (35), Catherine Mtaturu (52) na Charles Mjema (52) hawa wote kwa pamoja wanatarajia kufikishwa Mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili mara baada ya upelelezi kukamilika,” ameongeza Muroto.

Aidha katika tukio la mwisho Polisi inamshikilia Adema Massawe (44) kwa kukutwa na pombe haramu ya moshi lita 60 Novemba 3, 2019 katika eneo la maili mbili lililopo Jijini Dodoma na anatarajia kufikishwa Mhakamani.

Kufuatia matukio hayo Kamanda Muroto amesema jamii ikubali kubadilika kwa kufanya kazi halali ya kujiingizia kipato ili kuepuka uhalifu unaoweza kusababisha familizia zao kuteaeka kwa kukosa uangalizi kwani mwisho wa uhalifu ni majuto.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU