Jafo atoa ujumbe kwa wananchi kuelekea uchaguzi
Wananchi waliojiandikisha kupiga kura katika uchaguzi ujao wa serikali za mitaa, wametakiwa kutumia turufu ya kura yao kuchagua viongozi wenye weledi watakaoshiriki kuwaletea maendeleo.
Kwa upande wake mkuu wa chuo cha serikali za mitaa Dk. Mpamila Madale, amesema mbali na kuzalisha wataalamu pia wamekuwa wakishirikiana na mamlaka mbalimbali za serikali za mitaa katika kupanga na kutekeleza mipango ya maendeleo inayohusu wananchi.
Awali rais wa wanafunzi AMANI KISWABI ameiomba serikali kuwapa kipaumbele cha ajira kwa wahitimu hususani wa chuo hicho kutokana na kuwa na uelewa mkubwa wa serikali za mitaa.

Comments
Post a Comment