Gloomy Sunday, Wimbo Uliosababisha Watu zaidi ya 100 Kujiua


Gloomy Sunday (Jumapili ya Huzuni) ni wimbo uliotungwa na Rezso Seress (Rudi Spitzer), msanii kutoka nchini Hungary mwaka 1933. Reszo alitunga maneno ya wimbo huo na kupiga mwenyewe ala ya huzuni ya wimbo huo, baada ya kuachwa na mpenzi wake.

Inaelezwa kwamba kitendo cha kuachwa na mwanamke aliyekuwa akimpenda sana, kilimfanya apatwe na huzuni kali na msongo wa mawazo, na katika kipindi hicho ndipo alipopata wazo la kutunga mashairi na baadaye kuutengeneza wimbo huo.

Kwa sababu aliuimba akiwa na huzuni kali, wimbo nao ulijawa na hisia kali, za mtu anayelalamika kuvunjwa moyo na mpenzi wake, akifananisha kitendo cha kuachwa kuwa sawa na kufiwa na mpenzi aliyekuwa anampenda.idk_1-png.1046884

Awali ulionekana kuwa wimbo wa kawaida wa huzuni, lakini matukio ya watu kuyakatisha maisha yao baada ya kuusikiliza mara nyingi wimbo huo kwa kuurudiarudia yalianza kuripotiwa, wengine wakiacha kabisa ujumbe kwamba wamejiua baada ya kusikiliza wimbo huo.

Miaka miwili baadaye, serikali ya Hungary iliupiga marufuku wimbo huo, hata hivyo tayari ulikuwa umesambaa sana, kiasi kwamba watu bado waliendelea kuusikiliza, hasa pale inapotokea mtu ameachwa au ameumizwa na ampendaye.

Sifa za wimbo huo zilianza kusambaa duniani kote na mwaka 1936, wanamuziki wa Marekani na Uingereza waliutafsiri wimbo huo kwa lugha ya Kiingereza, kutoka lugha ya awali ya Ki-hungary, bado tatizo lilelile likawa linaendelea hata kwa matoleo yaliyotafsiriwa, watu wakawa wanaendelea kujiua baada ya kuusikiliza.

Mwanzoni mwa miaka ya 1940, toleo la Kiingereza la wimbo huo lilipigwa marufuku nchini Uingereza baada ya idadi ya waliokuwa wakijiua kuzidi kuongezeka lakini Marekani na sehemu nyingine duniani wimbo huo uliendelea kupigwa

Miaka michache baada ya wimbo huo kumpatia mafanikio makubwa na kuwa gumzo dunia nzima, Seress aliamua kumtafuta mwanamke aliyemuacha na kusababisha atunge wimbo huo, lengo lake likiwa ni kujaribu kumbembeleza ili warudiane kwani kama ni pesa, tayari alikuwa nazo baada ya wimbo huo kuwa maarufu dunia nzima.

Hata hivyo, katika hali ya kustaajabisha, inaelezwa kwamba Seress alipofika mahali alipokuwa akiishi mwanamke huyo, alikuta watu wamejaa, baadaye ikabainika kwamba mwanamke huyo amekunywa sumu na kujiua na kwenye chumba alichojiulia, ilibainika kwamba alikuwa akisikiliza wimbo huo na pia aliacha ujumbe wenye maneno mawili, kama sababu za kujiua kwake; Gloomy Sunday.

Inaelezwa kwamba Seress alibaki na hatia kubwa ndani ya moyo wake, akiamini kwamba yeye ndiyo chanzo cha kifo cha mwanamke huyo na mwaka 1968, naye aliamua kuyakatisha maisha yake kwa kujirusha ghorofani kupitia dirisha la chumba alichokuwa akiishi, nchini Budapest.

Seress aliacha ujumbe kwamba ameamua kuyakatisha maisha yake baada ya kuona wimbo alioutunga, umekuwa sababu za watu wengi kujiua hivyo anahisi hatia kubwa ndan ya moto wake, akawaomba radhi ndugu na marafiki wa wote waliojiua kwa sababu ya kusikiliza wimbo huo.

Lyrics (Literal Translation)
On a sad Sunday with a hundred white flowers
I was waiting for you, my dear, with a church prayer
That dream-chasing Sunday morning
The chariot of my sadness returned without you.
Ever since then, Sundays are always sad
Tears are my drink, and sorrow is my bread.
Sad Sunday. Last Sunday, my dear, please come along,
There will even be priest, coffin, catafalque, hearse-cloth.
Even then flowers will be awaiting you, flowers and coffin.
Under blossoming (flowering in Hungarian) trees
My journey shall be the last.
My eyes will be open, so that I can see you one more time
Do not be afraid of my eyes as I am blessing you even in my death.
Last Sunday."

Sikiliza Wimbo Wenyewe hapa:

By Hashpower7113

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU