DC Mjema Ashiriki Kumtafuta Aliyezama mto Msimbazi

Mtu mmoja mkazi wa Jiji la Dar es salaam, anahifiwa kupoteza maisha baada ya kuzama katika bonde la mto Msimbazi maeneo ya Jangwani.

Imeelezwa kuwa mtu huyo alikuwa katika shughuli zake za Kuokota chupa za plastic katika mtohuo.

Mkuu wa Wilaya ya ya Ilala, Sophia Mjema ameshirikiana kumtafuta mtu huyo na amewataka wakazi wa Jiji kuwa waangalifu ili wasipatwe na madhara kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.

Mjema amesema kuwa licha ya kuwa jitihada za kumtafuta mkazi huyo hazijazaa matunda, vikosi vya uokoaji vinaendelea kumtafuta.

Aidha amesema kuwa ” Tusiwe Tusiwe tunasema haya maji Ni kidogo Mimi Ni mzoefu, unaweza ukaingiza mguu, tope likakukamata maji yakiendelea kuja Hina ujanja, kitakachotokea Ni Kama kilichomtokea huyu mwenzetu”

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU

Kisa Cha Nabii Ibraahiym عليه السلام - Sehemu Ya 1