Wakati inapotajwa ibada, vinvyokuja akilini ni amri kama vile swala na kufunga. Jee ibada inahusisha swala na funga tu?
Hapana. Ibada haihusishi maamrisho ya dini kama vile kuswali kila siku na kufunga tu. Kila kitu, kila jambo, neno, kitendo, fikra au nia kwa kutafuta radhi za Allah, vyote huzingatiwa kama ibada. Kufanya yote mawili, kutekeleza amri za Allah na kuacha makatazo Yake kwa usawa huzingatiwa kuwa ni ibada. Hivyo basi, inawezekana kuigawa ibada kwenye mafungu mawili:
1. Matendo sahihi,
2. Ucha Mungu (Taqwa).
Matendo sahihi maana yake ni kutekeleza maamrisho ya Allah kama vile kuswali daima, kufunga, n.k.
Ucha Mungu maana yake ni kuepuka mambo yote aliyoyakataza Allah kama vile ulevi, Kamari na zinaa.

Comments
Post a Comment