Wajibu wa Mwanamune
Uwe Mwaminifu
Baada ya mapatano ya ndoa maisha binafsi ya watu wawili yanalingana na kuwa maisha ya ushirika moja wa kijamii. Kiapo kitukufu cha ndoa kinamaanisha kwamba mwanaume na mwanamkie wanapeana ahadi kila moja kuwa pamoja katika maisha yao yote, kusaidiana wao kwa wao, kuwa mwema na mwelewa wakati wote, wakati wa neema na wakati wa shida, wakati wa ugonjwa na afya njema na huzuni na kadhalika.
Utu unadai kwamba mwanandoa anatakiwa kuwa mwaminifu kwa ahadi yake. Wanandoa hawatakiwi kusahau mkataba wao hata kwenye hali ngumu. Msichana mdogo ambaye huchagua mwanamume mmoja kuishi naye katika maisha yake yote hatarajii kuwa amekuwa mwanamke wa makamo ya utu uzima. Si haki kwamba mwanaume atafute starehe na mwingine na kumwacha mke wake.
Mwanamke ambaye hutoa mchango mkubwa katika kujenga familia madhubuti katika mazingira mazuri ya maendeleo ya uchumi, hatarajii mume wake kumpenda mwanamke mwingine.
Mwanamke anayefanya bidii nyumbani kwa kawaida anayo matumaini kwamba mume wake hatamnyima mapenzi na huba yake wakati wa ugonjwa na kutokuwa na uwezo wa kufanya kazi. Jambo la mwisho kabisa hatarajii mume wake kutafuta starehe ya kwake peke yake.
Baadhi ya wanaume kwa kweli hawashituki. Wakati wake zao ni vijana na maumbo ya kuvutia wanafurahia kuwa nao, lakini huwaacha wanapo zeeka.
Mwanaume alimtaliki mke wake kwa sababu ya kuwa na kisirani, kwani tangu walipooana baba yake alikufa na mjomba wake akafilisika.
Mwanaume aliye muoa mwanamke kijana kwa kumpenda, alimtaliki baadaye kwa sababu hakumpenda tena.
Mwanamke… alilalamika mahakamani: “Nimeishi na mume wangu kwa miaka mingi, lakini sasa nimepata maradhi anasema kwamba hataki mke mgonjwa!”
Bwana mpendwa! Wewe si hayawani ambaye maisha yake yote ni kula na kukidhi matamanio ya kimwili. Wewe ni binadamu mwenye mchomo wa moyo, dhamira na tabia ya kujitolea. Hivi ni haki kweli kwamba wewe unafuatilia starehe zako nje ya nyumba yako?
Kama ndio, basi wewe ni muonevu na kwa hali hiyo wewe utaadhibiwa hapa hapa duniani. Ukitumia muda wako na mwanamke mwingine, basi, kwa ajili ya starehe utulivu wa akili yako na utapata maradhi ya kuharibikiwa akili. Watoto wako hawatakubali na watajibu kwa kukukashifu.
Kama mke wako anaugua, chukua hatua muhimu za kumtibu, na kama anayo maradhi yasiotibika, basi endelea kuishi naye, jitolee kumsaidia na usioe mke mwingine akingali hai.
Usimuudhi wakati huo mgumu. Ungetarajia nini endapo wewe ungekuwa katika hali hiyo? Ni haki kabisa kwamba yeye angetegemea hivyo hivyo kutoka kwako.
Ni sahihi kwamba wewe unapo ugua mke wako atataka umtaliki? Je hujafedheheka mbele ya marafiki na ndugu? Kwa hiyo kama unakubali kwamba uaminifu na unyofu ni sifa nzuri, basi jaribu kuwa mwaminifu.
Elimu Na Mafundisho
Mwanamke kijana ambaye ndio kwanza kaolewa anao wajibu wa kuendesha mambo ya mume wake na katika hali hiyo atahitaji ujuzi wa kupika, usafi, kunyosha nguo, kushona, kupanga fenicha, kukaribisha wageni wake, kushirikiana na watu wengine, kumtunza mtoto wake na kadhalika.
Mume wake atatarajia mke wake kujua yote haya. Hata hivyo, mategemeo yake yanaweza yasifanikiwe takriban muda wote kwa sababu ujuzi wa mke wake kijana kuhusu utunzaji wa nyumba ama haupo kabisa au upo kidogo sana.
Mtu afanyeje? Hili ni tatizo katika jamii zetu. Wazazi hawajali, wala mfumo wa elimu hauna mipango ya kutosha kukidhi haja hii. Hata hivyo, mtu anatakiwa kupata ufumbuzi wa tatizo hili.
Kwa vile mwanaume anakusudia kuishi na mke wake kwa maisha yake yote lazima amsaidie kumuelimisha, kwa sababu kwa kawaida wanaume huwa na umri mkubwa kuzidi wa wake zao na hivyo wanao uzoefu zaidi.
Mwanaume kwa uvumilivu anaweza kumuelemisha mke wake na kumfundisha vitu ambavyo anavijua. Anweza hata kumuuliza mama yake, dada au shangazi zake kuhusu mambo ambayo hayajui, au anaweza hata kununua vitabu vinavyohusu masomo kama ya kupika, ushonsji, utunzaji wa nyumba na kadhalika.
Mwanaume vile vile lazima amhimize mke wake kusoma vitabu ambavyo vitaonesha kimaadili kuwa ni vyenye manufaa. Lazima asahihishe upungfu wake wa maadili kwa adabu nzuri na sio kwa upinzani, au vinginevyo atageuka dhidi yake.
Mwanaume, kwa kutumia uvumilivu wake, anaweza kumwelimisha mke wake kwa mujibu wa njia yake ya maisha katika kipindi cha miaka miwili ya mwanzo wa ndoa yao. Inawezekana asifaulu asili mia kwa mia lakini bila shaka atakaribia kutosheleza mahitaji.
Elimu ya aina hii inahitaji uvumilivu, muda na busara, lakini mwanaume lazima ajaribu kuipata. Hii ni kwa sababu mwenza mzuri ni mama mzuri kwa watoto wake ni neema kwa mwanaume.
Mojawapo ya mambo muhimu ambayo mwanaume Mwislam aliyeoa anatakiwa kukumbuka ni ukweli kwamba mke wake pia ni Mwislam, na inawezekana awe hatambui utaratibu wa maisha ya Kiislamu na sheria zake. Inawezekana asijue hata kuhusu wudhu, kusali na kadhalika.
Kwa kweli ni wajibu wa wazazi kuwafundisha watoto wao mambo yote muhimu ya Kislamu na maadili. Kwa bahati mbaya, hata hivyo, wazazi hawajui kabisa kuhusu ukweli huu, na bila kuwafundisha mabinti wao kitu chochote kuhusu Uislamu, wanawaozesha. Hivyo wajibu wao huangukia kwenye mabega ya waume wanaowaoa.
Bwana mpendwa! Ni wajibu wako kumzoeza mke wako maadili ya Kiislamu na kumfundisha mambo yaliyohalalishwa na yale yaliyo haramishwa katika dini. Mfanye ajifunze kuhusu tabia za Kiislam. Kama huwezi kufanya hivi, basi tafuta msaada kutoka kwa wengine au fanya mpango wa vitabu na makala zenye elimu ya Uislamu na mwambie asome na kufanya kwa vitendo. Unaweza hata kufanya mpango wa elimu na maelekezo yake kupitia kwa mtu mwaminifu na aliyeelimika.
Kwa ufupi, ni wajibu wa mwanaume kumtia moyo mke wake kumuamrisha kufanya mema na kumkataza kufanya mabaya. Kama mwanamume atafuata wajibu wake huu, basi atafurahia kuwa na mwenza mwenye tabia njema, mwema, muaduilifu na mke mwenye busara.
Hata hivyo, kama mwanamume anaamua kutojali wajibu wake atateseka kwa kuwa na mke mjinga ambaye imani yake ni dhaifu na ambaye hana kinga dhidi ya uovu. Pia mume ataulizwa na Mwenyezi Mungu huko akhera kuhusu uzembe wake huu.
Mwenyezi Mungu anasema kwenye Qurani Tukufu:
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا قُوا أَنْفُسَكُمْ وَأَهْلِيكُمْ نَارًا وَقُودُهَا النَّاسُ وَالْحِجَارَةُ
{6}
“Enyi mlioamini jiokoeni nafsi zenu na watu wenu (wa nyumbani – wake zenu watoto wenu nk.,) kutokana na moto ambao kuni zake ni watu na mawe…” (Quran 66:6)
Imamu Sadiq (a.s) alisema: “Aya hiyo hapo juu ilipoteremshwa mmoja wapo wa Waislamu alikuwa analia na kusema; ‘Mimi siwezi kujinusuru hata mimi mwenyewe kutoka kwenye moto wa Jahanamu na ninatakiwa kuwajibika kuinusuru pia familia yangu kutoka kwenye Jahanamu!’ Mtume (s.a.w.) alimwambia mtu huyu: “Ingetosha kama tu ungewaagiza kufanya mambo hayo ambayo wewe unayafanya na uwakataze wasifanye yale ambayo wewe mwenyewe unajizuia kuyafanya.”
Imamu Sadiq (a.s) alisema: “Aya hiyo hapo juu ilipoteremshwa mmoja wapo wa Waislamu alikuwa analia na kusema; ‘Mimi siwezi kujinusuru hata mimi mwenyewe kutoka kwenye moto wa Jahanamu na ninatakiwa kuwajibika kuinusuru pia familia yangu kutoka kwenye Jahanamu!’ Mtume (s.a.w.) alimwambia mtu huyu: “Ingetosha kama tu ungewaagiza kufanya mambo hayo ambayo wewe unayafanya na uwakataze wasifanye yale ambayo wewe mwenyewe unajizuia kuyafanya.”
Mtukufu Mtume (s.a.w.w) alisema: “Wanaume wameumbwa kuwa viongozi na kuwajibika kwa familia zao, na kwa namna hiyo wanawajibu kwa watu wanaowategemea.”
Mtukufu Mtume (s.a.w.) pia amewakumbusha wanawake: “Waambieni waume zenu wafanye matendo mema kabla hawajawashawishi nyinyi kufanya mabaya.”
Kupata Mtoto
Moja ya mambo ambayo huweza kuwa ni nukta zenye kuumiza kwa wanandoa ni kuhusu kupata mtoto.
Ni kwamba mwanamke atataka kupata mtoto lakini mume wake anakataa au kinyume chake. Tatizo hili wakati mwingine huwa kubwa sana na matokeo yake wanandoa wanaweza kuishia katika kutalikiana.
Bibi…alilalamika mahakamani na kusema: “Niliolewa nikiwa na umri wa miaka ishirini na saba ambapo mume wangu alikuwa amemaliza masomo ya Chuo Kikuu. Alikuwa mkufunzi kwenye mojawapo ya chuo kikuu na nilihisi kuwa nilikuwa mwanamke mwenye bahati. Hata hivyo mume wangu hataki kuzaa mtoto. Simwelewi kwa sababu sote afya zetu ni nzuri na tunazo fedha za kutosha kuwa na angalau watoto wawili. Si kwamba hawataki watoto, kwani anawatunza vizuri wapwa zake.
Nina umri wa miaka thelathini na kama ilivyo kawaida ningependa kuwa mama. Mume wangu anaelewa hisia zangu lakini husema kwamba mtoto atakuwa sababu ya usumbufu katika maisha yetu na kuendelea.” Mwanamke huyu, wakati anajizuia asilie, anakabiliwa na tatizo ambalo ni zito sana hivyo kwamba wanandoa hawa waliamua kutalikiana, ili yeye aweze kuolewa tena na mwanamume mwingine na yeye apate muda wa kutosha kufanya utafiti wake wa kisayansi.”
Kupenda watoto na kuzaa ni matamanio ya kawaida ya binadamu na hata ya hayawani. Watoto ni matunda ya maisha na urithi mzuri kuliko wote wa mwanadamu.
Maisha ya mtu mwenye watoto hayatasitishwa na kifo chake lakini, hakika yataendeshwa kama vile maisha yalivyo panuka. Mtu asiye na mtoto au watoto atahisi mpweke na aliye tupwa na atajihisi vibaya zaidi atakapo kuwa mzee.
Nyumba isiyo na watoto ni mahali panapo chosha na haitakuwa changamfu na upendo. Ndoa isiyo na watoto, wakati wowote ipo katika hatari ya kuvunjika. Hivyo watoto ni chanzo cha uchangamfu na kudumu kwa familia.
Imamu Sadiq (a.s) alisema: “Furaha ya mtu imo katika kupata watoto.”
Mtume (s.a.w.) wa Uislamu alisema: “Zaeni watoto wengi kwa sababu mnamo Siku ya Hukumu nitajivunia idadi yenu juu ya umma nyingine.”
Kumpenda mtoto ni matamanio ya kawaida, lakini baadhi ya watu hupotoshwa kutoka kwenye kawaida yao na wanaathirika na maradhi ambayo huwafanya kutafuta visingizio kama vile upungufu wa fedha, kuwa ndio sababu ya kuwafanya wasipende kuzaa. Hata hivyo, Mwenyeyzi Mungu amehakikisha kwamba atawaruzuku viumbe Vyake vyote.
Bakr bin Saleh alisema: “Niliandika barua kwa Hadrat Abu al-Hasan (a.s) nikisema kwamba nilikuwa nachukua hatua za kuzuia nisipate mtoto kwa muda wa miaka mitano; kwa sababu mke wangu alikuwa anasita kupata mtoto, na kwamba alikuwa anasema kwamba ukosefu wa fedha ungefanya kazi ya kulea mtoto kuwa ngumu.’ Nilimuuliza Hadrat Abu al-Hasan maoni yake kuhusu jambo hili.” Akajibu: “Usizuie kupata mtoto, kwa sababu Mwenyezi Mungu Mweza atampa riziki.”
Mwenyezi Mungu Anaweza hata kuongeza riziki ya familia kwa sababu ya neema za watoto. Wapo watu wengi ambao walikuwa na shida kabla ya kupata watoto, lakini walipata maisha ya raha baadaye.
Baadhi ya watu huona watoto kama usumbufu. Hii si kweli na kwa kweli watoto ni chanzo kizuri sana cha furaha na kiburudisho kwa wazazi.
Kama ilivyo, kutunza watoto si kazi rahisi na yenye matatizo, lakini maadam inaafikiana na kanuni ya asili, mtu anaweza kuvumilia matatizo na kwa hali hiyo inafaa kukubali usumbufu uliomo humo.
Ufinyu ulioje wa akili wa wanaume na wanawake ambao kwa sababu ya kutokupata watoto wanakimbilia kuachana! Je si kweli kwamba inashangaza mwanaume mwenye elimu, anakataa kukubali sheria za utaratibu wa jambo la asili kwa kung’ang’ania kiasi cha hata kuwa tayari kumpa talaka mke wake?
Wanandoa wengine hukubaliana kupata mtoto lakini hubishana kuhusu wakati wa kupatikana mtoto. Mwanamke au mwanaume wa aina hii angesema; ‘Mtu lazima awe huru wakati wa umri mdogo kwani mtoto atamnyima uhuru wa kustarehe.
Ni vema kungoja hadi baadaye kupata mtoto mmoja au wawili.’ Kama wote mume na mke wanatofautiana kwa maoni, basi mabishano yataanza ambayo yanaweza kuishia kwenye kutalikiana.
Na tukumbuke kwamba kama mtu anataka watoto, basi lengo hili lingetekelezwa katika kipindi cha mwanzo kabisa cha ndoa. Hii ni kwa sababu watoto wanaozaliwa na wazazi vijana kwa kiasi fulani huwa bora kuliko wale wanaozaliwa na wazazi wenye umri mkubwa zaidi. Kwanza, watoto hawa afya zao huwa njema zaidi na wanaonekana kuwa na nguvu nyingi zaidi. Pili, kwa kuwa wanatokana na wazazi vijana, wanaweza kuishi kwa muda mrefu zaidi na wazazi wao. Wanaweza kusomeshwa zaidi na kulelelewa vizuri zaidi. Lakini watoto walio zaliwa na wazazi wenye umri mkubwa hunyang’anywa uongozi na mafundisho ya wazazi wao kwa sababu ya kifo au kukosa uwezo. Tatu watoto wa wazazi wenye umri mdogo wangeweza kufika kwenye umri wa kuwa na familia zao na kuanza kufanya kazi, ambapo wazazi wao wakingali hai. Hivyo wanaweza kuwa msaada mkubwa sana kwa wazazi wao watakapo kuwa wazee.
Kwa ufupi, kuzaa watoto wakati wa ujana ni vema zaidi kuliko umri mkubwa. Lakini hiki si kipengele cha muhimu sana hivyo kwamba kisababishe ugomvi na kutalikiana. Ni vema kwa mwanaume au mke kukubaliana kwa maelewano wasiruhusu suala hili kutengeneza mwanya katika ndoa yao.
Baadhi ya wanandoa hushindwa kuelewana kuhusu idadi ya watoto ambao wangetaka kuzaa.
Mwanamke akiwa amemshikia mtoto mikononi mwake alisema: “Miaka minne baada ya kuoana, nilizaa watoto wa kike wawili na mume wangu, lakini kwa kuwa alitaka mtoto mwanaume, nilipata ujauzito kwa mara nyingine na tena nilijifungua mtoto mwanamke. Sasa ninao watoto watatu wanawake. Mume wangu anafanya kazi benki na mshahara wake hautoshi familia yetu. Hivi karibuni amekuwa akisisitiza kwamba nibebe mimba mara nyingi hadi nizae mtoto wa kiume. Lakini mimi sipo tayari kwa mpango huu kwa sababu kipato chake hakitoshi kuwasomesha watoto wetu kwa namna tunavyotaka. Nimemwambia mara nyingi kwamba watoto wanaume na wanawake wote ni wazuri. Nina hofia kwamba kama nikibeba ujauzito tena nitazaa mtoto mwanamke tena.
Nina uhakika kwamba atataka kusisitiza tupate mtoto mwingine. Hatutakubaliana katika jambo hili na hivyo tumeleta shauri letu mahakamani.”
Ni sahihi kwamba kusomesha na kuelekeza watoto wengi ni vigumu na hii hususan ni kweli wako ambao hawana kipato cha kutosha.
Kwa hiyo, ni vema wanandoa kuamua kuhusu idadi ya watoto kwa mujibu wa kimaadili na uwezo wa kifedha. Lazima waelewane na waweze kupata ufumbuzi wa matatizo yao kwa kutumia busara na wema. Si sahihi kwa yeyote miongoni mwao kusisitiza kitu kisicho na mantiki.
Zipo familia nyingi ambazo ama wanao watoto wengi au zinatosheka na mtoto mmoja au wawili.
Baadhi ya wanandoa hutofautisha kuhusu jinsia ya mtoto (watoto) wanaotaka kuzaa. Wanandoa wengine, wanaume na wanawake hupenda kuzaa mtoto mwanaume na hawapendi kuzaa watoto wanawake. Kuzaliwa kwa mtoto mwanamke ni tukio ambalo lingemfanya mzazi mwanamke ajihisi ana hatia na kwa hiyo angenyamaza kwa sababu ni yeye ndiye amezaa. Lakini mwanamume huenda akaonesha kutokuridhika kwake. Wanaume wapo tofauti. Baadhi yao hawaoneshi kutokuridhika kwao wazi wazi na huishia kuonesha tu uso wa kuogofya. hawatilii maanani kuwahudumia wake zao baada ya kujifungua. Huonekana na huzuni.
Baadhi ya wanamume, hata hivyo huwa wakali sana wanapopata taarifa ya kuzaliwa mtoto wa kike. Huwakasirikia wake zao na huanzisha shutuma za makosa yao. Hupinga na kuanzisha ugomvi. Wanaume wengine huamua hata kuwapiga wake zao au kuwataliki.
Mwanamke alisema mahakamani; “Niliolewa miezi kumi na tano iliyopita na nikapata ujauzito miezi sita baadaye. Hivi karibuni, muda wa kujifungua ulipokaribia, mume wangu aliniambia kwamba nizae mtoto mwanaume. Lakini nilihisi kwamba ningezaa mapacha au hata watatu. Siku chache zilizopita nilijifungua mapacha wa kike. Nilifurahi sana kuhusu jambo hili, alitibuka na akaondoka hapo chumbani. Baadaye nilimuomba awapeleke watoto nyumbani, alinikaripia na kunilaumu kwa kuzaa mapacha wanawake. Akaniambia niondoke kwake, kwa hiyo nilikwenda kwa wazazi wangu na sasa ninaomba anipe talaka.”
Bibi… alimwambia mwandishi wa habari mahakamani: “Baada ya miaka ishirini na moja ya ndoa na kuzaa watoto watano, ninalazimika kuyaacha maisha ambayo nimeyapatia mchango mkubwa sana, kwa kumpisha mwanamke mwingine ambaye ameweza kuzaa mtoto mwanaume.
“Ninao watoto wanawake watano wazuri ambao ni wenye vipaji na ambao si tatizo kabisa kwa baba yao. Ni ipi hatia yangu kama siwezi kuzaa mtoto wa kiume. Mume wangu ananilaumu kwa kutokuzaa mtoto wa kiume na anataka mimi nimruhusu kuoa mwanamke mwingine.”
Kwa bahati mbaya, sifa hii imeendelezwa na watu wengine tangu enzi za Ujahiliya (kipindi cha ujinga) kwamba hutilia shaka maumbile ya binadamu ya jinsia ya kike. Huoni aibu kuzaa watoto wa kike na huhisi wamedhalilishwa.
Katika zama zaa ujinga, watu walikuwa na desturi ya kuzika watoto wa kike wakingali hai! Qurani Tukufu imesema kuhusu matendo yao ifuatavyo:
وَإِذَا بُشِّرَ أَحَدُهُمْ بِالْأُنْثَىٰ ظَلَّ وَجْهُهُ مُسْوَدًّا وَهُوَ كَظِيمٌ
{58}
“Na mmoja wao akibashiriwa kwa msichana, uso wake unasawijika, naye kajaa chuki.” (Quran 16:58),
يَتَوَارَىٰ مِنَ الْقَوْمِ مِنْ سُوءِ مَا بُشِّرَ بِهِ ۚ أَيُمْسِكُهُ عَلَىٰ هُونٍ أَمْ يَدُسُّهُ فِي التُّرَابِ ۗ أَلَا سَاءَ مَا يَحْكُمُونَ
{59}
“Anajificha asionekane na watu kwa ubaya wa aliyo bashiriwa! Je, akae naye juu ya fedheha hiyo au amfukie udongoni? Tazama uovu wa wanavyohukumu!” (Quran 16:59).
Lakini Uislamu unapinga fikira hii isiyo sahihi na kuwaona wanawake na wanamume kuwa wapo sawa.
Mtume (s.a.w.) wa Uislamu alisema: “Miongoni mwa watoto wenu walio bora zaidi ni mabinti zenu.”
Mtume (s.a.w.w) wa Uislam pia alisema: “Ishara ya mwanamke mwenye bahati ni yule ambaye mwanaye wa kwanza ni mwanamke.”
Kwa nyongeza, Mtukufu Mtume (s.a.w.w) alisema: “Yeyote ambaye anawalea watoto wanawake watatu au dada watatu, Pepo itakuwa ya kwake.”
Kama mtoto mwanamke angekuwa duni, Mwenyezi Mungu hangefanya ukoo wa Mtume (s.a.w.) uendelee kupitia kwa Hadhrat Fatima Zahra (a.s).
Bwana mpendwa! Unadai kwamba wewe ni mstaarabu na binadamu wa kisasa, kwa hiyo acha fikira za aina hiyo. Kuna tofauti gani wewe ukiwa na mtoto mwanamke au mwanamume. Wote hawa ni watoto wako na wote waweza kuelekea kwenye ubora. Mtoto mwanamke pia anaweza kuwa mtu mashuhuri kwa malezi yako sahihi ya elimu. Mtoto mwanamke ni bora zaidi ya mtoto mwanamume kwa kiasi fulani:
Kwanza, mtoto mwanamke ana huruma zaidi kwa wazazi wake anapokua na kujitegemea. Watoto wanawake, kama wazazi hawawapi upendeleo wowote zaidi ya watoto wao wanamume, wangekuwa na mapenzi zaidi kwao.
Pili, mtoto mwanamke mahitaji yake hayana gharama kubwa kama ya mtoto wa kiume, kwa sababu kwa kawaida hadumu muda mrefu nyumbani kwa wazazi wake, kwani huolewa mapema katika umri wake na huwaacha wazazi wake akiwa na vitu vichache tu vya kuanzia maisha yake mapya. lakini, wavulana huwa wa makamo ya vijana ambao huweza kuishi na wazazi wao kwa muda mrefu. Wazazi watalipa gharama ya elimu yake, wtamtafutia kazi, watalipa gharama zake wakati wa miaka miwili ya kutumikia jeshi, kama upo umuhimu, na halafu kumuoza mke, baada ya hapo angehitaji kupewa nyumba, mabusati, samani, na kadhalika. Angehitaji hata msaada wa fedha kutoka kwa wazazi wake baada ya kuoa.
Tatu, kama wazazi hawatafanya ubaguzi baina ya mtoto wao mwanaume na mwanamke, na kama watamtendea wema mkwilima wao, mkwilima wao mara nyingi huenda akawasaidia wao wakati wa matatizo na kwa kawaida huwa mwaminifu zaidi kwao kulinganisha na mtoto wao wa kiume.
Kwa vyovyote vile, hivi huwa ni kosa la mwanamke inapotokea anazaa mtoto mwanamke?
Mume na mke wote wanahusika katika tendo la kuzaa na mwanaume hana haki ya kumlaumu mke wake kwa jambo hili. Vinginevyo ni sawa kabisa mwanamke naye kumlaumu mume wake kuhusu jambo hili. Hata hivyo, hapana yeyote kati yao anaye laumiwa kwa jambo hilo kwani ni utashi wa Allah pekee wenye kuamua jinsia ya mtoto.
Wapo baadhi ya wataalamu ambao wanaamini kwamba jinsia ya mtoto inaweza kuamuliwa kutokana na jinsi mama anavyopata lishe yake wakati wa ujauzito wake. kwa hiyo, kama wapo watu wanaopendelea mtoto wao awe na jinsia wanayotaka wao, wanaona wataalamu na kwa hiyo watazuia hali ya kuwalaumu wake zao.
Mtu mwenye akili si lazima afadhaike kwa kupata mtoto mwanamke, lakini lazima afurahi sana. Anatakiwa kuonesha furaha yake, huba yake kwa mke wake na anatakiwa hata kumpa mke wake zawadi.
Angeweza kusherehekea kupatikana kiumbe kipya na hata kuchukua hatua za kimantiki katika kumridhisha mke wake kwamba mtoto mwanamke ni bora kama alivyo mtoto mwanaume, iwapo mke wake atakuwa amefadhaika kwa sababu ya kupata mtoto mwanamke.
Baba mwenye busara hawezi kubagua baina ya mtoto wake mwanaume na mwanamke, hangemlaani yeyote kwa kupata mtoto mwanamke na kwa hiyo angepambana na fikira za kipindi cha ujahiliya.
Mwanaume alisikia habari ya kuzaliwa mtoto wa kike wakati alipokuwa na Mtukufu Mtume wa Uislamu (s.a.w.w). taarifa hiyo ilimvuruga. Mtume
(s.a.w.w) alisema: “Kwa nini umefadhaika?” Alisema: ‘nilipokuwa ninatoka nje ya nyumba yangu, mke wangu alikuwa katika uchungu wa kujifungua, na sasa nimeletewa taarifa kwamba nimepata mtoto mwanamke.’ Mtume (s.a.w.w) alisema; “Ardhi inayo nafasi ya kumtosha yeye, na mbingu inampa hifadhi na Mwenyezi Mungu atampa riziki. Yeye ni ua lenye kutoa harufu nzuri ambamo kutoka humo utapata furaha kubwa.”
Ujauzito Na Kuzaliwa Mtoto
Muda wa kudumu ujauzito ni kipindi nyeti chenye matukio ya majaliwa kwa maisha ya mtoto. Tabia ya lishe ya mama pamoja na harakati za kimwili na za kisaikolojia ni mambo ya muhimu kwake na maisha ya kimbe kilichomo kwenye tumbo lake la uzazi.
Afya au maradhi ya mtoto, nguvu au udhaifu, ubaya wa sura au uzuri wa sura na tabia yake nzuri au mbaya na sehemu ya akili na busara, huanzishwa kwenye tumbo la uzazi la mama. Mmoja wapo wa wataalamu ameandika: “Wazazi wa watoto ama wanaweza kukua kwenye ngome ya afya au kwenye uharibifu wa maradhi. Ni wazi kwamba uharibifu wa maradhi si sehemu inayofaa kuishi roho ya milele au mwanadamu. Hii ni sababu ambayo kwamba wazazi wanaaminika kubeba wajibu mkubwa sana ikilinganishwa na uumbaji wote.”
Kwa hiyo, kipindi cha mimba hakiwezi kufikiriwa au kufanywa kama cha kawaida. Mara tu mimba inapoanza, wazazi hupewa wajibu mkubwa.
Wazazi wanaweza bila kufahamu kusababisha matatizo ya aina nyingi, yaliyo mengi baina yao yanaweza kuwa magumu sana kurekebishwa, kwa sababu ya uzembe mdogo wakati wanapofanya kazi zao.
Yafuatayo ni mambo ambayoyanayofaa kuangaliwa: Chakula: Kilengwa kilichomo kwenye tumbo la uzazi la mama yake, hula chakula na kukua kwa lishe ya damu yake. Kwa hiyo, chakula cha mama kinatakiwa kuwa na virutubishi vya kutosha ili viweze kumpa mtoto vitu vya asili anavyo vihitaji, pia kwa ajili ya ustawi wa mama. Kwa hiyo, upungufu wowote wa vitamini, protini, mafuta, sukari au wanga katika ulaji wa mama inaweza kusababisha madhara katika afya ya mtoto. Imam Sadiq (a.s) alisema: “Chakula cha kilengwa kinapatikana kwenye lishe anayopata mama.” 256.
Tatizo kubwa ambalo linawapata wanawake wengi sana wajawazito ama katika kipindi fulani cha ujauzito au kipindi kikubwa cha ujauzito, hupungukiwa na ladha ya lishe bora, kwani hupatwa tabia ya tamaa ya vyakula fulani huku akisikia kinyaa kwa vyakula vingine.
Kwa sababu kawaida hula chakula kidogo wakati wa kipindi hiki, lazima wahakikishe kwamba chakula chao si kizito na wakati huo huo kiwe na virutubisho vya kutosha ili kiweze kumpa mtoto vitu vya msingi.
Ufuatiliaji wa mpangilio ya chakula katika kipindi hiki cha ujauzito ni mgumu sana, hususan kwa watu wasio na uwezo wa kifedha na wale ambao hawana ujuzi wa ubora wa vyakula mbali mbali. Wajibu mkubwa anao baba ambaye anatakiwa kufanya jitihada kubwa kutoa vyakula vya msingi kwa mke wake. Kutokujali kwa upande wa baba kungeweza kusababisha madhara kwa mtoto anayekua, ambapo yeye ndiye atakaye wajibishwa hapa duniani na akhera.
Hali ya kiakili: Mama, wakati wa ujauzito anahitaji utulivu na anatakiwa apate hisia ya uzoefu wa kupenda maisha. Hii ina faida kwa mama na mtoto wake. Baba akiwa ni mwenye wajibu wa kumpa mke wake mazingira ya amani na uchangamfu, lazima ajaribu kwa bidii zaidi wakati wa kipindi cha ujauzito wake. Mume kwa wema na upendo, anatakiwa kuwa na mwenendo kwa namna ambayo mke wake anaweza kujivuna na kufurahi kuhusu yeye kuwa na ujauzito, lazima aone fahari kwamba maisha ya kiumbe kingine yanategemea kwake na kwamba anawajibu wa ustawi wake.
Mjamzito aache miondoko ya kushtua. Mwanamke mwenye mimba anatakiwa kuepuka shughuli nzito na anatakiwa kupumzika sana. Kunyanyua kitu kizito au miondoko ya haraka ya mwili inaweza kusababisha madhara yasiyo rekebika kwake, mtoto au wote. Wanawake wajawazito wanatakiwa kuepuka kazi ngumu na waume zao wanatakiwa kujitolea kufanya kazi kama hizo.
Woga wa uchungu wa Kujifungua. Kujifungua mtoto mara nyingi huwa si kazi nyepesi. Maumivu ya uchungu wa kujifungua wakati mwingine huwa makali sana.
Wanawake wajawazito mara nyingi huwa na wasi wasi kuhusu maumivu yaliyomo na uwezekani wa hatari yanayohusishwa na kujifungua mtoto, inayofuatiwa na kipindi cha kupata ahueni baada ya kujifungua. Ingawa wanawake wanatakiwa kustahamili ujauzito, uchungu wa kujifungua na kulisha watoto wao, wanamume pia wanatakiwa kugawana wajibu wa kulea watoto wao.
Ingawa kiinitete kinatungwa kwenye tumbo la uzazi la mwanamke pia yupo baba wa mtoto ambaye amefanya kazi muhimu katika kutungwa mimba. Kwa hiyo, wanamume wanatakiwa kuhakikisha kwamba wake zao wanapata maliwazo wakati wa kujifungua na kuwa tayari kusaidia endapo chochote kitahitajika haraka.
Ni kazi ya kibinadamu na kiislamu kwa wanaume kufanya kila wawezalo kwa wake zao wajawazito kwa kuwapa matunzo ya kitabibu na mahitaji ya kurahisisha kujifungua. Mwanaume anatakiwa kuwa na mke wake baada ya kuzaliwa kwa mtoto, lakini kama hawezi kufanya hivyo anatakiwa ampigie simu au amtumie ndugu zake wakae naye. Anatakiwa kujaribu kumrudisha nyumbani yeye mwenyewe na amsaidie kufanya kazi za nyumbani ili mke wake apate mapumziko ya kutosha na kurudisha tena nguvu iliyopotea. mwanaume anaye mfanyia mke wake wema, atazawadiwa na Mwenyezi Mungu. Mtume (s.a.w.w) alisema: “Mwanaume aliye mbora sana miongoni mwenu ni yule anayemfanyia mke wake wema.
Na mimi miongoni mwenu ni mwanaume mbora sana kuhusu kuwafanyia wema wake zangu.”
Imamu Sadiq (a.s) alisema: “Mwenyezi Mungu na amrehemu mwanaume ambaye kufanya uhusiano mzuri na mke wake, kwa sababu Mwenyezi Mungu anamteua mwanaume kuwa mlezi wa mke wake.”
Mwanaume anaye mtendea mke wake wema, atafanya mazingira ya familia yake kuwa machangamfu na ataimarisha misingi yake. Mke wake, kwa upande wake, kamwe hatasahau mapenzi ya mume wake na huba yake. Matokeo yake mshikamano wa ndoa unakuwa imara zaidi.
Msaada wa kuwalea watoto
Mtoto ni tunda la ndoa. Wote wawili wanamume na wanawake wametoa mchango katika kupatikana kwa mtoto na lazima wagawane matatizo na starehe zinazohusishwa kuwapo kwake. Kumlea mtoto ni kazi ya wazazi wote na si mama peke yake. Ingawa mara nyingi zaidi ni mama ndio wanaolea watoto wao na kuwalisha kuwaweka katika hali ya usafi na kadhalika, baba wasidharau juhudi hizo. Sio sahihi kwa mwanaume kudhani kwamba kazi ya kutunza watoto ni ya wanawake tu na kwamba wanaume hawana wajibu katika jambo hili. Si haki kwamba baba aondoke na kumwacha mke wake na mtoto ambaye analia na aende kupumzika kwenye chumba kingine.
Mpendwa ndugu! Mtoto wako ni wajibu wako pia. Unadhani ni haki kumwacha mkeo na mtoto anayelia ambapo wewe unapumzika kwenye chumba kingine? Hii ni njia inayofaa kufanya mambo nyumbani mwako? Kama vile unavyofanya bidii nje ya nyumba, mkeo hufanya bidii ndani ya nyumba; na anahitaji usingizi kama vile unavyohitaji usingizi. Yeye pia hafurahii kilio cha mtoto, lakini huvumilia.
Ndugu yangu! Ubinadamu halikadhalika na Uislamu unakutaka wewe umsaidie mkeo katika kumlea mtoto wenu. Ama mnatakiwa msaidiane kwa pamoja au mpeane zamu. Kama mkeo anakosa usingizi kwa usiku wote na analala baada ya sala ya alfajiri, halafu usitegemee kwamba atakutayarishia staftahi kama siku zingine. Kwa kweli unatakiwa wewe mwenyewe utayarishe staftahi yako na ya mkeo ili pindi akiamka akute kila kitu tayari mezani. Mke wako hawajibiki kumlea mtoto wenu wakati wote unapokuwa haupo nyumbani au upo safarini. Kwa ufupi unatakiwa umsaidiea mkeo na mgawane wajibu wa kulea mtoto. Kwa njia hii, maisha ya familia yenu yataimarishwa.
Mwisho wanawake lazima pia wakumbuke kwamba waume zao hufanya bidii kupata riziki ya familia na wasitegemee kwamba wanaweza kuwadai zaidi ya uwezo wao. Wanawake wasitegemee waume zao ambao wamechoka kuanza kuwasaidia kulea watoto mara wanaporudi kutoka kazini.
Kikwazo Kikubwa Katika Kusuluhisha Tofauti
Kikwazo kikubwa sana katika kusuluhisha ugomvi wa kifamilia ni ubinafsi na kiburi. Kwa bahati mbaya, watu wengi huathiriwa na tabia hizi. Watu kama hawa hupungukiwa na sehemu fulani ya akili ambapo hukubali tabia zao tu na kukataa za wengine na hawataki kukubali makosa yao. Hususan ni hatari sana ambapo ghasia ya tabia inafanikishwa na mtu mwingine yaani, kuwakosoa wengine kwa makosa yao. Wakati mwingine mume na mke wote husumbuliwa na tatizo hili kwa maana hiyo, watagombana kila siku. Kila mmoja atamlaumu mwenzake na wakati huo huo kila mmoja wao atakataa kuhusika kabisa na makosa yote.
Wakati mwingine kama upande moja tu utaumia kutokana na dosari hii ya kukoseana, kila mmoja atamwona mwenzake analo kosa na kwa kufanya hivyo watakuwa wanajikomboa kabisa kutokana na kulaumiana.
Pale ambapo mume na mke wote wanakumbwa na usumbufu wa vurugu hii, ni vigumu sana kuwasuluhisha, kwa sababu hawatakuwa tayari kuzingatia ushauri wa mtu yeyote. Wakati ambapo kila mmojawao anasikiliza redio au anaangalia vipindi vya runinga vinavyohusu mambo ya familia, wataona dosari fulani ya tabia ambayo inaendekezwa na mwenza wake na kwa hiyo ataanzisha lawama zake hapo hapo. Lakini dosari yoyote ikizungumziwa inayogusa udhaifu wao watajifanya hawasikii na wataelekeza fikira zao kwenye mambo mengine. Wanaweza kununua kitabu kinachohusu maadili ya familia na kumpa mwenza wake, bila wao kuwa na hisia zozote za kuwa na hamu ya kusoma yaliyomo humo.
Ubinafsi unaweza kuwa mkali sana hivyo kwamba muathirika hataweza hata kutambua tatizo hilo. Katika hali kama hiyo, uhusiano baina ya wanandoa unaharibika na hata usiwezekane kuendelea. Matokeo yake ni, ama maisha yataendelea katika hali ya ugomvi, huzuni, kutokuwa na furaha au hata kutalikiana.
Kwa hiyo, inashauriwa kwamba wanandoa wote waache tabia ya ubinafsi na kiburi. Wanandoa ambao wanatatizwa na hali hii, wanatakiwa wapate muda wakae pamoja, na wawe kama majaji wawili waaminifu wazungumzie matatizo yao. Kila mmoja amsikilize mwenzake kwa umakini na bila upendeleo wowote. Kila mmoja wao anatakiwa kufahamu dosari zake bila kusahau hata iliyo ndogo sana pamoja na nia ya kuzirekebisha. Halafu wote wawili wanatakiwa waamue kujisahihisha wao wenyewe; lakini ni hapo tu ambapo wanahisi umuhimu wa uelewano wa kina na ambapo wote wanatamaani kufufua mapenzi yao na utulivu ambao ulikuwapo baina yao.
Hata hivyo, inapokuwa hakuna uwezekano wa kupatikana suluhu, wanandoa wanatakiwa kuwasilisha matatizo yao kwa mtu mwenye uzoefu, mwaminifu, mtambuzi wa kutegemewa na mwema. Kama mtu kama huyo ni rafiki au ndugu, hiyo itakuwa nafuu yao kwa sababu wanaweza kumwambia kila kitu na kungoja hukumu yao. Lazima wamsikilize na kuupokea ushauri wake na kutia nia ya kuutekeleza kwa vitendo.
Kama ilivyo, kuamini ushauri wa jaji si rahisi, lakini mtu ambaye anajali familia yake na uimara wake, amani kudumu kwake anatakiwa kuvumilia na baadaye afurahie matokeo yake yenye manufaa.
Wazazi wa wanandoa wa aina hiyo, kama wanatambua matatizo ya kifamilia ya watoto wao, wanatakiwa kuwashauri wamuone Kadhi mwenye uzoefu, mwaminifu na nia njema. Wazazi hawatakiwi kuonesha upendeleo kwa mume au mke., Kwa njia hii, kwa msaada wa Mwenyezi Mungu, matatizo yao yanaweza kutatuliwa.
Mwenyezi Mungu anasema kwenye Qurani Tukufu:
وَإِنْ خِفْتُمْ شِقَاقَ بَيْنِهِمَا فَابْعَثُوا حَكَمًا مِنْ أَهْلِهِ وَحَكَمًا مِنْ أَهْلِهَا إِنْ يُرِيدَا إِصْلَاحًا يُوَفِّقِ اللَّهُ بَيْنَهُمَا ۗ إِنَّ اللَّهَ كَانَ
عَلِيمًا خَبِيرًا
{35}
“Na mkichelea kutakuwepo mfarakano baina ya mume na mke basi pelekeni muamuzi kutokana na jamaa za mume, na muamuzi kutokana na jamaa za mke, wakitaka mapatano mwenyezi Mungu atawawezesha. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi Mwenye Khabari.”(Quran 4:35)
Talaka
Licha ya kwamba talaka ni kitendo halali, ni kitendo kinacho chukiza na ni kibaya kuzidi vitendo vyote.
Imam Sadiq (a.s) alisema: “Oeni lakini msitalikiane, kwa sababu talaka inaweza kutetemesha Arsh ya Mwenyezi Mungu.”
Imam Sadiq (a.s) pia alisema: “Mwenyezi Mungu huipenda nyumba ambayo inakaliwa na wanandoa na huchukia nyumba ambayo wanandoa wametalikiana. Hakuna kitendo kinacho mchukiza Mwenyezi Mungu kuliko kutalikiana.”
Ndoa si kama kununua jozi ya viatu au soksi ambapo vitu hivi vikichujuka kwenye matamanio ya mmiliki wake, huvitupa na kununua jozi nyingine ya viatu. Ndoa ni makubaliano ya kiroho ambayo hufanywa na watu wawili kwa lengo la kuishi pamoja kama marafiki wa kuliwazana, na wapenzi hadi kifo chao. Makubaliano haya yameegemezwa kwenye matumaini haya hivyo kwamba msichana huwaacha wazazi wake na kuungana na mume wake.
Mwanaume hufanya jitihada na kufanya bidii kwa msingi wa makubaliano hayo ya kimungu. Hulipa gharama za harusi yake na hununua vitu muhimu kwa ajili ya maisha yake mapya na hufanya kazi kwa ajili ya faraja ya familia yake.
Ndoa si jambo la kukata kiu cha tamaa ya kimwili na wanandoa hawawezi kuiharibu kwa visingizio vidogo. Licha ya kwamba kutalikiana ni tendo halali, linachukiza sana na watu wanashauriwa kuepukana nalo kadiri iwezekanavyo.
Bahati mbaya, tendo hili ambalo linachukiza sana, limekuwa jambo la kawaida sana kwenye nchi za kiislamu na misingi ya familia imetikisika sana, hivyo kwamba kwa ujumla watu hawana imani tena kuhusu ndoa.
Kuvunja ndoa inaruhusiwa hapo tu ambapo hali si ya kawaida na inalazimu iwe hivyo.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) alisema: “Malaika Jibril aliniusia kuhusu wanawake sana hivyo kwamba nilifikiri kwamba wanamume wasiwataliki isipokuwa kama wanazini.”
Kesi nyingi za kutalikiana hazina sababu za msingi, isipokuwa visingizio visivyo komaa. Yaani, sababu za kesi nyingi zaidi za talaka ni hafifu na hazifai kuwaathiri na kuwatenganisha wanandoa. Mume au mke, kwa sababu ya ubinafsi, anaweza kukuza jambo dogo na kuamua kwamba maisha yao ya ndoa lazima yakome.
“Bibi fulani mwenye umri wa miaka ishirini na nne, alimwambia mumewe awaalike wazazi wake kwenye chakula cha jioni chenye gharama kubwa. Kwa kuwa hakutekelezewa ombi hilo, alidai talaka.”
“Mwanaume alimtaliki mke wake kwa sababu alikuwa anazaa watoto wanawake tu. Wanandoa hawa walikuwa na watoto wanawake watano.”
“Mwanamke aliomba talaka kwa sababu mume wake aliamini mafundisho ya kumfikiri Mungu kwa njia ya tafakuri na hakuonesha kupenda maisha.”
“Mwanamume alidai talaka kwa sababu alitaka kumuoa mwanamke tajiri.”
“Mwanamke aliomba talaka kwa sababu mume wake alikuwa na tabia ya kuficha fedha zake kwenye mikono ya shati.”
“Mwanaume alimtaliki mke wake kwa madai kwamba ana balaa tangu walipooana baba wa mume alifariki na ami yake alifilisika.”
Wanandoa ambao hawana heshima na busara, wanaweza wakanasa kwenye mtego wa mambo madogo kama hayo na kudai talaka.
Wanandoa wanaotaka kutengana, wasifanye haraka kutelekeza jambo hilo. Wanashauriwa wafikiri kwa uangalifu kuhusu athari na maisha yao ya baadaye kwa makini na halafu waamuwe. Hususan lazima watafakari kuhusu mambo mawili:
Jambo la kwanza: wanandoa wanaotaka kutalikiana kwa kawaida hutaka kuoa au kuolewa tena. Lakini lazima wakumbuke kwamba baada ya kutalikiana, watu wanaojulikana kama watalaka hawatakuwa na sifa nzuri kuhusu ndoa. Watu huwafikiria kuwa wenye ubinafsi na si waaminifu.
Baada ya kupata taarifa ya maisha ya ndoa ya siku za nyuma ya mwanamume na kutaliki, mwanamke anaweza kuwa na shaka kuhusu uaminifu wa mwanaume au tabia yake.
Mwanamke mtalaka ni nadra sana kupata fursa ya kuolewa tena. Kwa sababu wanaume kwa kawaida hawaoneshi kuvutiwa sana kuoa mwanamke mtalaka na hutilia shaka kuhusu uaminifu wake.
Kwa hiyo, mtalaka anawezekana akaishi peke yake kwa muda wote wa maisha yake na atateswa na upweke pia.
Kuwa mpweke ni hali ngumu sana na watu wengine wapweke hupendelea zaidi kifo kuliko maisha ya aina hiyo yasiyovumilika.
Mwanamke wa miaka ishirini na mbili ambaye aliachika, alijaribu kujiua mnamo usiku wa siku ya harusi ya dada yake. Alikuwa na mtoto mmoja.
Hata kama mwanaume anafaulu kuoa tena, haitajulikana kabisa kwamba maisha yake mapya yatakuwa mazuri zaidi kuliko ya mke wake wa mwanzo. Mke wake wa pili anaweza kuwa mbaya zaidi. Mwanaume wa aina hii hupendelea kumtaliki mke wa ndoa ya pili na kurudi kumuoa mke wa kwanza. Lakini kwa kawaida huwa wamechelewa sana.
Mwanaume wa miaka themanini alisema mahakamani; “Nilikuwa na maisha mazuri nilipomuoa mke wangu wa ndoa ya kwanza, takriban miaka sitini iliyopita. Lakini baada ya muda alianza kunifanyia ubaya kwa hiyo nikamtaliki. Nilioa wanawake wachache baada ya hapo lakini nilihisi kwamba mke wangu wa kwanza alikuwa mwaminifu zaidi miongoni mwao. Nilimuona na nikampa rai ya kurudiana naye. Yeye, ambaye pia alichoka maisha ya upweke alikubali na sasa tunataka kuoana tena.”
Mwanaume alimtaliki mke wake wa pili kwa sababu hakutaka kuwalea watoto wawili aliozaa kwenye ndoa yake ya kwanza. Halafu akaamua kumuoa tena mke wake wa kwanza ambaye alimtaliki miaka mitano ya nyuma.’ Jambo la pili: Wanandoa ambao wanataka kutengana lazima wafikirie pia suala la watoto wao. Faraja ya watoto imo kwenye familia yenye wazazi wote wanao ishi pamoja na wanawalea kwa pamoja.
Baada ya kuvunjika kwa maisha ya familia, watoto hufadhaika sana. Kama ni baba yao tu anaye watunza, hawatakuwa na maisha na mama yao wa kambo. Mama wa kambo si tu kwamba wanashindwa kutekeleza kama mama halisi, lakini wanaweza kufikiri watoto wa kambo ni mzigo. Mama wa kambo wengine huwanyanyasa watoto wa kambo na kuwafadhaisha kwa kukusudia na baba zao hunyamaza kimya.
Bibi harusi wa miaka kumi na nne ambaye alitaka kujiua alisema akiwa hospitalini. Wazazi wangu walitengana nilipokuwa na mwaka mmoja.
Baba yangu alioa tena baada ya mwaka mmoja na nusu na sasa tunaishi wote. Mama yangu wa kambo alikuwa na desturi ya kunipiga na hata alinichoma moto kwa chuma mara kadhaa. Baba yangu licha ya kuwa na uwezo wa kifedha alinikataza nisisome. Takriban mwezi mmoja uliopita baba yangu alinioza kwa mtu mwenye umri wa miaka arobaini na tano.
Msichana wa miaka kumi na tatu alijinyonga. Msichana huyu aliishi na kaka zake wawili. Mmojawapo wa hao kaka zake alisema; “Wazazi wetu walitengana miaka takriban mitatu iliyopita. Mama yangu aliolewa tena na mwanamume mwingine na baba alikufa miezi miwili iliyopita. Ilikuwa saa 12:30 jana jioni nilikuja nyumbani nikamkuta dada yangu amejinyonga.”
Pia, kama mama anachukua wajibu wa watoto wake, basi watakosa baba halisi ambaye angewatunza. baba wa kambo mara nyingi ndiye sababu ya kukosekana furaha kwa watoto wake wa kambo.
Mwanamke alimsaidia mume wake wa ndoa ya pili kumfunga mtoto wa kambo mwenye umri wa miaka nane kwenye kitanda. Halafu wakafunga mlango na wakaondoka kwenda matembezini. Waliporudi nyumbani,walikuta mtoto wao ameungua moto hadi kufa kwa sababu ya moto uliounguza nyumba.
Talaka huharibu familia na huwaacha watoto wanatangatanga hawana hifadhi. Watoto mara nyingi huteseka kwa sababu ya ubinafsi wa wazazi wao.
Watoto wanne wenye umri wa miaka kumi na mbili, tisa, sita na minne walikwenda kwenye kituo cha polisi. Mtoto mwanamme mwenye umri mkubwa zaidi alisema: “Wazazi wetu walitengana muda fulani uliopita. Wakati wote walikuwa wanabishana na walikuwa na tabia ya kugombana kila siku mchana na usiku. Sasa wametalikina, hapana mmojawao ambaye yupo tayari kutulea sisi.”
Watoto ambao hawana mlezi anayefaa na mazingira ya familia, mara nyingi hukengeuka. Kutokupata elimu ya kutosha na mtu mwenye huruma katika maisha yao, huwafanya wasumbuliwe na hisia za udhalili. Wanaweza hata kufanya uhalifu wa viwango mbali mbali, wakati wa utoto au utu uzima.
Mtu anaweza kutambua jambo hili na kusoma matukio kwenye magazeti kila siku.
Kwenye utafiti uliofanywa kwenye kituo cha kurekebisha vijana, ni wazi kwamba katika vijana wahalifu mia moja kumi na sita wa kituo hiki, watu themanini walithibitisha kwamba mama zao wa kambo waliwanyanyasa ndio sababu wakafanya uhalifu.”
Mpendwa bibi na bwana! Kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, kwa ajili ya watoto wako wasio na kosa, kuweni wasamehevu nyinyi kwa nyinyi wanandoa. Msikuze matatizo madogo na msipende kung’ang’ania ubishi. Msitafutane makosa nyinyi kwa nyinyi. Fikirieni mambo yenu ya siku zijazo na watoto wenu.
Kumbukeni watoto wenu wanawategemeeni nyinyi na wanatumaini kupata furaha yao kutoka kwenu. Wahurumieni na msiharibu maisha yao.
Kama mkidharau matamanio yao ya ndani na kama mkivunja nyoyo zao ndogo, hamtaweza kuepuka athari ya masikitiko yao. Kwa hiyo, hamtaweza kuwa na maisha yenye faraja pamoja.

Comments
Post a Comment