Wajibu wa Mwanamune

Mlezi wa Familia

Mwanaume na mwanamke ni nguzo mbili za msingi wa familia, lakini kwa kuwa wanaume wamepewa sifa maalum kwa amri ya uumbaji, na kwa sababu ya uwezo wao wa mantiki ni imara zaidi ya ule wa wanawake, wao huchukuliwa kama walezi wa familia zao.
Mwenyezi Mungu Mweza wa yote amewaweka wanaume kuwa walezi wa familia zao na anasema kwenye Qur’ani:
الرِّجَالُ قَوَّامُونَ عَلَى النِّسَاءِ بِمَا فَضَّلَ اللَّهُ بَعْضَهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ {34}
“Wanaume ni wasimamizi wa wanawake, kwa kufadhiliwa na Mwenyezi Mungu baadhi yao juu ya baadhi … (Quran 4:34)”
Kwa hiyo, wanaume wana jukumu kubwa na zito zaidi katika kuzisaidia familia zao.
Ni mwanaume ambaye kwa kutumia busara yake, anaweza kuisadia familia yake na kutayarisha mazingira kwa ajili ya furaha yao, na ni yeye ambaye anayeweza kuigeuza nyumba kuwa Pepo na mke wake kuwa kama Malaika.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) alisema: “Mwanaume ni mlinzi wa familia yake na kila mlezi anao wajibu kwa hao waliopo kwenye ulinzi wake.”
Mwanaume ambaye anaisaidia familia yake, lazima atambue kwamba mwanamke pia ni binadamu kama mwanaume. pia mwanamke anayo matamanio na haki ya uhuru na maisha. Kumuoa mwanamke si kukodisha mtumishi, lakini ni chaguo la mwenza na rafiki ambaye atakuwa tayari kuishi pamoja katika maisha yote. Mwanaume lazima amtunze na amtimizie matakwa yake. Mwanaume si mmiliki wa mke wake, kwa kweli mwanamke anazo haki fulani kwa mume wake. Mwenyezi Mungu anasema kwenye Qurani Tukufu:
وَلَهُنَّ مِثْلُ الَّذِي عَلَيْهِنَّ بِالْمَعْرُوفِ ۚ وَلِلرِّجَالِ عَلَيْهِنَّ دَرَجَةٌ ۗ وَاللَّهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ {228}
“...Nao wanawake wanayo haki kwa sharia kama ile haki iliyo juu yao. Na wanamume wana daraja zaidi kuliko wao…” (Quran 2:228)

Utunzaji Wa Mke Wako

Siri ya ustawi wa familia inategemea na jinsi mtu anavyomtunza mke wake, na hii ni kama ilivyowajibu wa mke kwa mume wake ambao unaeleweka kuwa katika kiwango sawa na Jihadi, pia unatambua kama tendo jema na lenye thamani sana. Lakini mwanaume ajifunze namna ya kumshughulisha mke wake, katika namna ambayo atageuka kuwa na tabia kama Malaika.
Kuhusu jambo hili, mwanaume lazima atafiti kuhusu tabia na matakwa ya mke wake. Lazima apange maisha yake kufuatana na matakwa ya mke wake na mahitaji sahihi. Mwanaume anaweza kwa tabia na msimamo wake kumshawishi mke wake katika njia ile ambayo inampendeza yeye (mke wake), kwake yeye mume na nyumba yake.
Hili ni somo ambalo linahitaji maelezo zaidi na mazungumzo ya kina yatawasilishwa baadaye kwenye kitabu hiki.

Mpende Mkeo

Mwanamke ni kituo cha wema na ni kiumbe chenye hisia kubwa sana. Kuwepo kwake hutegemea huruma na upendo. Huwa na shauku ya kupendwa na wengine na jinsi anavyopendwa zaidi ndivyo anavyofurahi zaidi. Hujitolea sana ili apendwe na wengi. Tabia hii ina nguvu sana ndani mwake hivyo kwamba akigundua kwamba hakuna mtu anaye mpenda, basi atajitambua kama ameshindwa. Atakasirika na atahisi kuvunjika moyo.
Kwa hiyo, kwa hakika mtu anaweza kudai kwamba siri ya mwanamume aliyefuzu katika maisha ya furaha ya ndoa ni jinsi anavyo onesha mapenzi kwa mke wake.
Bwana mpendwa! Mke wako kabla ya kuolewa na wewe, alikuwa anafaidi mapenzi ya wazazi wake na wema wa wazazi wake. Sasa ameingia kwenye mkataba wa ndoa na wewe na sasa amechagua kuishi na wewe katika maisha yake yote, anatarajia wewe umtimizie matakwa yake ya mapenzi na huba. Anatazamia wewe kuonyesha mapenzi zaidi kwake kuliko alivyopokea kutoka kwa wazazi wake na marafiki zake. Amekuamini wewe sana na ndio sababu amekupa udhamini wa maisha yake.
Siri ya ndoa yenye furaha hutegemea jinsi unavyodhihirisha mapenzi yako kwa mkeo.
Ukitaka kuuvutia moyo wake, ukitaka awe mtiifu kuhusu matakwa yako kama kuimarisha ndoa yenu, ukitaka mkeo akupende wewe, au adumishe uaminifu kuliko au… basi lazima kila mara uoneshe mapenzi na huba yako kwake.
Usipokuwa mwema kwa mke wako, basi anaweza kupoteza mvuto kwenye nyumba yake, halikadhalika na watoto pia. Na zaidi ya yote kwako wewe mwenyewe. Wakati wote nyumba yako itakuwa katika hali machafuko. Hatakuwa tayari kufanya juhudi kwa ajili ya mtu asiyempenda.
Nyumba ambayo ndani yake haina mapenzi, hufanana na jahanamu inayowaka moto, hata kama ni nadhifu sana na iliyojaa vitu vya anasa.
Mke wako anaweza kuugua au kupatwa na mfadhaiko. Anaweza kutafuta kupendwa na wengine kama hatoshelezwi na wewe. Anaweza asikuthamini wewe na nyumba yako pia, kiasi kwamba anaweza hata kuomba talaka!
Unawajibika kwa yote haya kwa sababu umeshindwa kumtosheleza mkeo. Kwa hakika ni kweli kwamba taratibu zingine za kutalikiana hutokea kwa sababu ya ukatili wa mume au kinyume chake.
Angalia takwimu zifuatazo. Mahitaji ya saikolojia ya mapenzi, uzembe wa waume kuhusu matakwa ya wake zao na kutokuzingatia umuhimu wa hadhi ya kiakili ya wanawake, ni vipengele ambavyo vimekuwa sababu ya kesi nyingi za kutalikiana.
Mnamo mwaka 1969 miongoni mwa kesi za kutengana 10372, katika kesi 1203 wanawake walionesha sababu ya kutaka kutalikiana kuwa ni kuvunjwa moyo kimaisha, kujihisi hathaminiwi na upungufu wa waume kutokujali matakwa na hisia kubwa za wake zao.” 146
Mwanamke alisema mahakamani; “Nipo tayari kuacha mahari yangu na hata kumlipa mume wangu fedha ili akubali kunipa talaka. Mume wangu anawapenda zaidi kasuku wake ndio sababu sitaki kuishi naye zaidi ya sasa.”
Mapenzi na urafiki wa familia ni thamani kubwa zaidi kuliko chochote na ndio sababu Mwenyezi Mungu ameiona hiyo kama mojawapo ya alama za uwezo na neema kubwa ambayo mwanadamu amepewa. Qurani Tukufu inasema:
وَمِنْ آيَاتِهِ أَنْ خَلَقَ لَكُمْ مِنْ أَنْفُسِكُمْ أَزْوَاجًا لِتَسْكُنُوا إِلَيْهَا وَجَعَلَ بَيْنَكُمْ مَوَدَّةً وَرَحْمَةً ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِقَوْمٍ يَتَفَكَّرُونَ {21}
“Na katika ishara zake ni kuwa amekuumbieni wenza kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao. Naye amejaalia mapenzi na huruma baina yenu. Hakika katika haya bila ya shaka zipo ishara kwa watu wanaofikiri (Quran 30:21).”
Imamu Sadiq (a.s) alisema: Yeyote ambaye ni rafiki yetu huonesha wema zaidi kwa mke wake.”
Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) alisema: “Jinsi mtu anavyozidi kuwa mwaminifu ndivyo anavyozidi kuonesha wema kwa mke wake.”
Imamu Sadiq (a.s) alisema: “Mmojawapo ya sifa bainifu ya Mitume wa Mwenyezi Mungu ni kwamba wote ni wema kwa wake zao.”
Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) alisema: “Maneno ya mwanaume anaye mwambia mke wake; ‘Ninakupenda kweli’ kamwe hayaondoki moyoni mwake.”
Kama mambo yalivyo, mapenzi na huba lazima yawe halisi na kuvutia kwenye moyo wa mwingine, lakini hata kupenda sana kwa mtu haitoshi, kwa kuwa ni muhimu kuonesha huba. Kwa kuonesha hisia zako kwa maneno na vitendo vyako, mapenzi unayoonesha, yatapata jibu zuri kutoka kwa mkeo na nyoyo zenu zitaimarisha muungano wa mapenzi.
Uwe wazi na udhihirishe mapenzi yako kwako bila kusita. Wakati yupo au hayupo, msifie. Mwandikie barua unapokuwa safarini na mtaarifu kwamba kutokuwa karibu naye unajihisi mpweke sana. Mara kwa mara mnunulie kitu kama zawadi. Mpigie simu unapokuwa ofisini au shughuli zako na umuulize hali yake.
Kitu kimoja cha muhimu sana kwenye akili ya mwanamke ni namna hizi za kuonesha mapenzi kwake.
Bibi fulani wakati analia kwa masikitiko alisema. “Niliolewa na mume wangu usiku mmoja wa majira ya kupukutika kwa majani. Tuliishi pamoja kwa amani kwa muda fulani. Nilihisi kuwa nilikuwa mwanamke mwenye bahati kubwa sana hapa duniani. Niliishi kwenye nyumba yake ndogo kwa miaka sita. Nilihisi ninayo furaha mara mia moja nilipogundua kwamba nilikuwa mja mzito.
Nilipomtaarifu mume wangu alidondokwa na chozi la furaha wakati amenikumbatia mikononi mwake. Alilia sana hivyo kwamba karibu angeshindwa kujizuia. Halafu akatoka nje na akaninunulia mkufu wa almasi kwa fedha yake ya akiba. Alinipa mkufu na akasema: ‘Ninatoa hii kwa mwanamke bora kuliko wote ambao ninewaona hapa duniani.’ Lakini baada ya muda mfupi alikufa kwenye ajali ya gari.”

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU