Uwe Mtu Wa Kuonesha Shukrani

Kama mtu ni mwema na mpaji wa utajiri wake ambao ameupata kutokana na kazi ngumu, shukrani na kuoenasha kufurahia kwako kwa matendo kama hayo ni hali ambayo itachangamsha hisia zake za ndani na kumfanya ahisi amefanikiwa.
Matendo ya ukarimu yanaweza kuwa kawaida ya mtu ambapo hujenga mazoea kutumia na kugawana utajiri wake na wale wanao hitaji. Hata hivyo, kama matendo ya ukarimu yanapuuzwa na hayafurahikiwi, mhusika anaweza akapoteza utashi na msukumo wa kufanya wema. Itakuwa ni kawaida kwa mtu kuhitimisha kwamba ilikuwa ni kutumia vibaya kutoa fedha yake aliyoipata kwa jasho ambapo hakuna shukrani inayotolewa.
Shukrani na kufurahishwa ni tabia za kuvutia akiwa nazo mtu na ni siri ambayo kwayo mtu anaweza kuvuta matendo ya msaada.
Hata Mwenyezi Mungu ametaja kwamba shukrani kwa neema Zake ni sharti ambalo husababisha neema Zake kuendelea kutolewa kwa wanadamu:
وَإِذْ تَأَذَّنَ رَبُّكُمْ لَئِنْ شَكَرْتُمْ لَأَزِيدَنَّكُمْ ۖ وَلَئِنْ كَفَرْتُمْ إِنَّ عَذَابِي لَشَدِيدٌ {7}
“Na alipotangaza Mola wenu : Mkishukuru nitakuzidishieni; na mkikufuru, basi adhabu yangu ni kali.” (Qur’ani 14:7).

Mpendwa Bibi! Mumeo naye pia ni binadamu. Kama mtu mwingine yeyote yule. Yupo tayari kusaidia familia yake na anaiona kama wajibu wa uadilifu na kisheria. Anapopewa shukrani na kufurahikiwa kwa kutekeleza kazi yake, kazi hizo haziwi tena mzigo kwake.
Wakati wowote anaponunua vitu vya nyumbani au kitu kama nguo na viatu kwa ajili yako na watoto, furahi na umshukuru yeye. Onesha shukrani zako kwa vitu vidogo anavyofanya kama kununua bidhaa za vyakula, kusafiri na familia na kukupa wewe fedha. Unapoonesha shukrani, unamfanya mumeo ajihisi kuwa mwema na kuzawadiwa kwa usumbufu uliompata. Uwe mwangalifu kwamba usizipuuze kazi zake na kuwa mtu asiyejali mchango wake kuhusu ustawi wa familia.
Anaweza akaanza kutumia fedha yake kwingineko au kwake yeye mwenyewe.
Ikiwa tu rafiki au ndugu amekupa zawadi ya jozi ya soksi au shada la maua, unatakiwa kumshukuru mara nyingi, hivyo, ni kawaida tu na ni haki kumfurahia mumeo kwa kukupendelea na kukufikiria. Usidhani kwamba utakuwa unajidhalilisha kwa kuonesha shukrani zako. Kinyume chake, utapendwa na kujaliwa kwa vitu vingi zaidi kwa sababu unafurahia juhudi ya mumeo ambapo dharau na ubinafsi ni tabia ambazo zinaweza kuipeleka familia kwenye mabalaa.
Zifuatazo ni Hadith zinazozungumzia tabia za shukrani: Imam Sadiq (a.s) alisema: “Wanawake bora zaidi miongoni mwa wanawake wenu ni hao ambao huonesha furaha wakati waume zao huleta kitu nyumbani na hawaoneshi kutokuridhika kama hakuna kilicho letwa nyumbani.”
Imam Sadiq (a.s) alisema: “Mwanamke yeyote ambaye husema kwa mumewe kwamba hajaona vitu vyovyote vizuri kutoka kwake basi anakuwa amekosa uaminifu na anavuruga ibada yake.”
Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) alisema: “Yeyote asiye washukuru watu wanaomsaidia, kwa kweli, haoneshi shukrani zake kwa Mwenyezi Mungu kwa neema Zake.”

Usitafute Dosari Za Mwenzio

Hakuna mtu aliyekamilika. Watu wengine ni warefu sana au wafupi sana au wanene sana au wembamba sana, wanapua kubwa au pua ndogo, wanasema sana au wakimya sana, wana hasira zana au wanaelewana na watu haraka sana weusi sana rangi ya wastani au wanakula sana au wanakula kidogo na orodha inaweza kuendelea. Wanaume na wanawake wengi sana wanazo dosari hizi. Ni matumaini ya kila mwanaume na kila mwanamke kutafuta mwenzi aliyekamilika, lakini matumaini ya aina hiyo si sahihi. Hakuna uwezekano wa kumpata mwanamke anaye muona mumewe kama mtu aliye kamilika.
Wanawake hao ambao hutafuta makosa ya waume zao bila shaka watayapata.
Wanaweza wakaona dosari ndogo na kuzikuza kwa kushughulikia jambo hilo hadi kiwango cha kuwa kipingamizi kisichovumilika. Dosari hii huchukua nafasi ya sifa zingine zote za mume. Kila mara huwalinganisha waume zao na wanaume wengine. Wameanzisha kitu kinachoitwa mwanaume anayefaa katika dhana yao kiwango ambacho hakiafikiani na waume zao. Kwa hiyo, kila mara wanalalamika kuhusu dosari ndani ya ndoa zao. Wanawake hao hujifikiria kuwa na bahati mbaya na kushindwa na maisha na pole pole huwageuza kuwa wanawake |wenye chuki.
Tabia ya aina hiyo ya mwanamke humfanya nini mumewe? Anaweza kuwa ni mtu mvumilivu sana ambaye anaweza kustahamili ujeuri lakini upo uwezekano mkubwa atafedheheshwa na atakuwa na kinyongo kwa mkewe.
Hali hii inawezekana ikawatumbukiza wanandoa husika kwenye mabishano na kuelezana dosari za kila mwanandoa. Wote wawili watadharauliana na maisha yao yatageuka kuwa na mlolongo wa ugomvi na mabishano. Hivyo, ama wataishi katika mateso wakiwa pamoja au wataamua kutalikiana. Katika hoja zote mbili, wote watahasarika, hususan ambapo hakuna uhakikisho kwamba ndoa nyingine inaweza kuthibitisha vinginevyo.
Inasikitisha kwamba wapo wanawake wasiojua na wanakaidi katika huo ujinga wao. Inawezekana kwamba wanaweza kuharibu maisha ya familia zao kwa jambo dogo. Ifuatayo ni mifano ya wanawake wa aina hiyo: “Mwanamke alimwacha mume wake na akaenda nyumbani kwa baba yake kwa sababu mume wake alikuwa ananuka mdomo. Mwanamke huyo hakuwa tayari kurudi kwa mumewe hadi atatue tatizo lake. Kufuatana na malalamiko ya mume, mahakama iliwasuluhisha wana ndoa hao na mke akarudi kwa mumewe. Walipokwenda nyumbani, mke aligundua kwamba pumzi ya mumewe ilikua bado inanuka, kwa hiyo alihamia chumba kingine.”
“Daktari wa meno mwanamke alimtaliki mume wake kwa sababu hakuwa katika kiwango kinacholingana na cha kwake; mwanaume alifuzu na kupata taaluma hiyo miaka mitatu baada ya mke wake.”
“Mwanamke aliomba kumtaliki mume wake kwa sababu alikuwa na desturi ya kuketi chini na kula kwa kutumia vodole vyake, alikuwa hanyoi kila siku na hakujua jinsi ya kuishi na watu.”
Kama mambo yalivyo, si kwamba wanawake wote wapo hivi. Wapo wanawake wenye akili, wa kweli, na wanao utambuzi wa kutosha kwamba hawa hatarishi ndoa na furaha kwa kukuza dosari za waume zao. Mpendwa Bibi! Mumeo ni binadamu kama wewe. Hakukamilika, lakini anaweza kuwa na sifa nyingi. Kama unapendezwa na ndoa yenu na familia yenu basi usitafute udhaifu wake.
Usifikirie dosari zake ndogo kuwa muhimu. Usimlinganishe na mwanaume huyo ambaye umembuni akilini mwako. Inawezekana mumeo awe na udhaifu fulani ambao haupo kwa wengine. Lakini kumbuka kwamba wanaume wengine wanaweza kuwa na kasoro ambazo hazipo kwa mumeo. Ridhika na sifa zake. Hatimaye, utaona kwamba sifa zake zinazidi dosari zake. Zaidi ya hayo kwa nini utarajie kumpata mume mkamilifu ambapo wewe mwenyewe si mkamilifu. Kama wewe unajivuna kiasi cha kutosha kujiona wewe ni mkamilifu, basi waulize watu wengine:
Mtume (s.a.w.w) alisema: “Hakuna kitu kibaya zaidi kwa binadamu kuliko kutafuta dosari za watu wengine, ambapo hawajali mapungufu yao.”
Kwa nini ukuze dosari ndogo? Kwa nini uharibu maisha yako kwa kitu kisichokuwa maanani?
Uwe na busara, acha upuuzi! Puuza dosari za mumeo na usizitaje mbele yake au nyuma yake. Jaribu kutengeneza hali ya hewa ya uchangamshi katika familia yako na ufurahie neema za Mwenyezi Mungu.
Hata hivyo, inawezekana pawepo dosari katika tabia ya mumeo ambazo unaweza kuzirekebisha. Kama ni hivyo, unaweza kufaulu kufanya hivyo hapo tu ambapo utakuwa na busara na uvumilivu. Hutakiwi umlaumu au kuanza kumgombeza, lakini mwendee kwa njia ya kirafiki.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU