Usimwangalie Mtu Yeyote Isipokuwa Mumeo

Usimwangalie Mtu Yeyote Isipokuwa Mumeo

Mpendwa Bibi! Kabla hujaolewa inaewezekana ulikwisha chumbiwa na watu wengine. Posa za uchumba huu inawezekana zilitoka kwa watu matajiri, wasomi, wenye sura nzuri na kadhalika ambao ungependa wakuoe.
Matarajio ya aina hiyo yalikuwa ni jambo la kawaida kabla ya kuolewa. Lakini sasa umechagua mwenzi wako na kuwekeana mkataba wa dhati naye kuwa wapenzi katika maisha yenu yote, hivyo, sahau yaliyopita kabisa. Lazima uyaweke pembeni matamanio yako ya zamani na usahau ofa hizo za zamani. Usimfikirie mwamanume mwingine yeyote isipokuwa mumeo na utafute amani naye. Kama ukifanya vinginevyo, utajiweka katika hali ya mashaka.
Sasa basi, umekubali kuishi na mumeo, kwa nini wakati wote uendelee kuwatilia maanani wanaume wengine? Kwa nini umlinganishe mumeo na wanaume wengine? Unapata manufaa gani unapowatazama na kuwatilia maanani wanaume wengine isipokuwa kujiweka katika hali ya mateso yasiyo na mwisho na kusababisha upate maumivu makali ya akili?
Imam Ali (a.s) alisema: “Yeyote anayeyaacha macho yake huru, kila mara atapata maumivu ya neva na atanasa kwenye mtego wa wivu wakati wote.”
Kwa kuwatazama waume wengine na kuwatilia maanani na kuwalinganisha na mumeo, utamuona mwanaume ambaye hana dosari za mumeo. Unaweza kudhani kwamba labda mwamaume huyo amekamilika kwa sababu huzijui dosari za mwanaume huyo. Utafikiria kuwa ndoa yako ina mushkeli, na fikira hii inaweza ikawafikisheni mahali penye mwisho wenye hatari.
Mke wa mtu, umri wake miaka 18 ambaye alitoroka nyumbani kwake alikamatwa na polisi usiku wa jana. Akiwa kituo cha polisi mwanamke huyu alisema kwamba baada ya miaka mitatu ya ndoa, pole pole alihisi kwamba hampendi mume wake. Alisema: “Nilikuwa na tabia ya kulinganisha uso wa mume wangu na nyuso za wanaume wengine na nikajuta kwa nini niliolewa naye.”
Mpendwa Bibi! kama unataka ndoa ya kudumu daima milele, kama hutaki mateso ya kiakili, na kama unataka muendeshe maisha ya kawaida, basi acha kuwa mbinafsi na sahau hayo matarajio yako yasiyofaa. Usiwapongeze wanaume wengine. Usimfikirie mwanaume yeyote isipokuwa mumeo. Usiendekeze fikira hizi:
‘Afadhali ningeolewa na fulani’
‘Ningependa mume wangu aonekane kama . . . . . .’
‘Natamaani mume wangu angefanya kazi ya. . .. . . . . .’
‘Natamaani….. Natamaani……. Natamaani….’
Kwa nini ujifunge jela kwa kuendekeza mawazo hayo? Kwa nini utibue misingi ya ndoa yako? Kama lolote kati ya matakwa hayo yangefanikiwa kwa kweli, ungejuaje kwamba ungefanikiwa kuridhika zaidi? Unao uhakika kwamba wake za waume wajulikanao kama ‘hawana dosari; wanaridhishwa nao?
Mpendwa Bibi! Kama mumeo anashuku kwamba unaonesha kuvutiwa na wanamume wengine, atakata tamaa na kuacha kuvutiwa na wewe. Usitaniane na wanamume wengine au kufuatana nao. Wanamume ni wepesi kuhisi hivyo kwamba hawawezi hata kuvumilia wake zao kuonesha kuvutiwa na picha ya mwanamume mwingine.
Mtukufu Mtume (s.a.w.w) alisema: “Mwanamke yeyote aliyeolewa ambaye huwatazama wanamume wengine atakabiliwa na adhabu kali ya Mwenyezi Mungu.”

Vazi La Hijabu La Kiislamu

Wanaume na wanawake, licha ya kwamba wanavyo vipengele vingi vinavyofanana, pia wanazo tabia za pekee. Mojawapo ya tabia hizi ni kwamba wanawake ni viumbe wa kuvutia, wazuri, na wanaopendwa. Ni wachangamfu, wanavutia na wanapendwa; ambapo wanaume huchangamshwa, huvutiwa na huwapenda wanawake kwa sifa zao.
Mwanaume anapomuoa mwanamke, hutamani uzuri wote na mapenzi yote ya mke wake visitiriwe kwa ajili yake tu.
Hutumaini kuwa ni yeye peke yake ndiye anayefaidi uchangamfu, mapenzi, kujishaua, uzuri, ukunjufu na kadhalika na kuwaepuka wanaume wengine kabisa. Mwanaume kimaumbile yu moto moto sana na hamvumilii mwanaume mwingine kumtazama mke wake au kuanzisha aina fulani ya uhusiano naye. Mwanaume ataona uhusiano wa karibu na mke wake na wanaume wengine kuwa ni kukiukwa kwa haki yake ya kisheria. Mume anatarajia mkewe kufuata kanuni ya vazi la kiislamu la Hijab na kwa kuwa mwepesi wa kubadilika kufuatana na tabia na maadili ya Kiislamu atashiriki katika kutunza haki yake ya kisheria.
Mwanaume yeyote aliye mwaminifu na hamasa lazima atakuwa na hamu hiyo. Tabia ya kijamii ya mwanamke ambayo imeegemezwa kwenye maadili ya Kiislamu, itaweka akili ya mume katika hali ya utulivu; kwa hiyo atafanya kazi kwa shauku kubwa ili aweze kutunza familia yake, na mapenzi kwa mke wake yataongezeka. Mwanaume wa namna hii hatavutiwa na wanawake wengine. Kinyume chake mwanaume ambaye mkewe havai Hijab ambayo ni vazi linalovaliwa na mwanamke Mwislamu na badala yake huonesha uzuri wake kwa wanaume wengine au anachanganyika nao, atatibuliwa sana. Atamuona mke wake kuwa anahusika na kukandamiza haki zake. Mume wa aina hiyo kila mara atapitia kwenye mateso na taabu na mapenzi kwa mkewe yatapungua pole pole.
Kwa hiyo, ni kwa manufaa ya jamii, na wanawake kwamba wanatakiwa kuvaa inavyostahiki na kuwa na tabia ya unyenyekevu, wanatakiwa kuonekana hadharani bila urembo na kuacha kuonesha uzuri wao kwa wengine.
Kuvaa Hijab ni wajibu wa Kiislamu. Mwenyezi Mungu Mweza wa yote anasema kwenye Qur’ani Tukufu:
وَقُلْ لِلْمُؤْمِنَاتِ يَغْضُضْنَ مِنْ أَبْصَارِهِنَّ وَيَحْفَظْنَ فُرُوجَهُنَّ وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا مَا ظَهَرَ مِنْهَا ۖ وَلْيَضْرِبْنَ بِخُمُرِهِنَّ عَلَىٰ جُيُوبِهِنَّ ۖ وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا لِبُعُولَتِهِنَّ أَوْ آبَائِهِنَّ أَوْ آبَاءِ بُعُولَتِهِنَّ أَوْ أَبْنَائِهِنَّ أَوْ أَبْنَاءِ بُعُولَتِهِنَّ أَوْ إِخْوَانِهِنَّ أَوْ بَنِي إِخْوَانِهِنَّ أَوْ بَنِي أَخَوَاتِهِنَّ أَوْ نِسَائِهِنَّ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُنَّ أَوِ التَّابِعِينَ غَيْرِ أُولِي الْإِرْبَةِ مِنَ الرِّجَالِ أَوِ الطِّفْلِ الَّذِينَ لَمْ يَظْهَرُوا عَلَىٰ عَوْرَاتِ النِّسَاءِ ۖ وَلَا يَضْرِبْنَ بِأَرْجُلِهِنَّ لِيُعْلَمَ مَا يُخْفِينَ مِنْ زِينَتِهِنَّ ۚ وَتُوبُوا إِلَى اللَّهِ جَمِيعًا أَيُّهَ الْمُؤْمِنُونَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ {31}
“Na waambie Waumini wanawake wainamishe macho Yao, Na wazilinde tupu zao, na wala wasioneshe uzuri wao isipokuwa unaodhihirika. Na waangushe shungi zao juu ya vifua vyao, wala wasioneshe uzuri wao ila kwa waume zao, au baba zao au baba wa waume zao, au watoto wao, au watoto wa waume zao, au kaka zao, au watoto wa kaka zao, au wana wa dada zao, au wanawake wenzao, au iliyowamiki mikono yao ya kuume, au wafuasi wanamume wasio na matamanio, au watoto ambao hawajajua mambo yanayohusu uke. Wala wasipige chini miguu yao ili yajulikana mapambo waoliyoyafisha. Na tubuni vyote kwa Mwenyezi Mungu, enyi Waumini, ili mpate kufanikiwa. (Quran 24:31)
Kuchunga vazi la Kiislamu la Hijab na kuizingatiwa matumizi yake katika jamii kuna manufaa kwa wanawake katika vipengele vingi: Kwa kutumia vazi la Hijab, wanawake wanaweza kulinda uzuri wao wa kijamii na maadili ya ndani kwa ubora zaidi, na kujilinda dhidi ya kuwa tu kitu kilichopo kwenye maonesho.
Wanaweza kuthibitisha imani na mapenzi yao kwa waume zao, kwa ukamilifu zaidi na kwa hiyo kusaidia kutengeneza na kutunza familia yenye uchangamfu na kuzuia hisia mbaya na ugomvi wa kifamilia. Kwa ufupi, wanaweza kuvutia nyoyo za waume zao na kujiimarisha kwenye familia zao.
Kwa kuzingatia matumizi ya Hijab ya Kiislamu mitazamo isiyo ya kisheria yenye dokezo ya kutamani kutoka kwa watu wenye udhaifu huo, itakoma na kusaidia kupunguza idadi ya ugomvi, kuimarisha mizizi ya familia, na matokeo yake kutengeneza mazingira ya utulivu ndani ya familia.
Hijab ya Kiislamu ya wanawake pia itasaidia vijana wa kiume ambao hawajaoa, kutokana na kujiingiza kwenye vitendo viovu. Hivyo, kuwaepusha vijana dhidi ya mazingira yanayoamsha hisia za kutamaani mwanamke aliyevaa nguo isiyo sitiri umbo lake hali ambayo pia itawanufaisha wanawake katika jamii.
Kama wanawake wote wangefuata utaratibu wa Hijab ya Kiislamu basi, wanawake wote wangekuwa na uhakika kwamba waume zao wanapokuwa nje ya familia zao, hawangekutana na mwanamke asherati ambaye angewavutia na kumtoa nje ya familia yake.
Uislamu unatambua lengo mahususi ambalo limesababisha kuumbwa kwa mwanamke na humuona yeye kama msingi muhimu wa jamii na kupewa wajibu kwa jamii. Jamii humtaka mwanamke ajitolee katika kutekeleza wajibu wake wa kuvaa Hijab ya Kiislamu, ambayo ingeepusha uovu na upotofu wa jamii na kutengeneza uimara, usalama na kutukuza taifa lake. Lakini kwa wazi wazi thawabu kubwa zaidi ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mweza wa yote kwa kutekeleza wajibu wake kwa dini.
Mpendwa Bibi! Kama unapenda uimara na amani kuwepo kwenye familia yako, na mumeo aendelee kukuamini wewe siku zote, kama unajihusisha na haki za wanawake katika jamii; kama unavutiwa na afya ya vijana kiakili na unao wasi wasi kwamba wanaweza wakaacha maadili mema, kama unataka kuchukua hatua za uhakika za wanaume waovu kuacha kuwatongoza wanawake; na kama unatafuta radhi ya Mwenyezi Mungu kwa kuwa Muislamu muaminifu na mwenye kujitolea, basi tumia vazi la Hijabu ya Kiislamu.
Usioneshe uzuri wako na urembo wako kwa wageni, ama uwe ndani nyumbani kwako ukiwa na ndugu zako wa karibu, au kwenye mikusanyiko mingine ya kijamii nje ya nyumbani kwako. Lazima uvae ushungi mbele ya shemeji zako na watoto wao, waume wa wifi zako, waume wa shangazi zako, na binamu zako.
Usipovaa Hijabu ya Kiislamu mbele ya watu waliotajwa ni dhambi na pia unaweza kusababisha mateso makubwa kwa mumeo, hata kama hatasema.
Mwanamke halazimiki kuvaa Hijabu kwa kiwango kile kile mbele ya baba mkwe, kaka yake, na watoto wa kiume wa kaka au dada yake, ingawa ni vema kwa kiwango fulani kuvaa Hijabu mbele ya watu hawa pia. Kwa usemi mwingine, wanawake wasionekane mbele ya watu hawa- ndugu zake- kama ambavyo anaweza kuvaa kwa kumvutia mumewe. Hii ni kwa sababu wanaume wengi sana hawapendi wake zao waonekane katika hali ya kuvutia kwa kuvaa nguo au urembo mbele ya wanaume wengine, na kama mambo yalivyo isisahaulike kwamba utulivu wa akili na imani ya mume kwa mke wake ni muhimu sana kwa kudumu na usalama wa familia yote.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU