UNYENYEKEVU KATIKA SWALA

Unyenyekevu ndani ya swala ndio hasa swala yenyewe, na ndio msingi wake. Maana yake ni moyo wangu kutambua kuwa nipo mbele ya Allah ndani ya swala kwa kuhisi unyenyenyekevu na udhaifu, nikizitilia maanani aya, dua na nyiradi ninazozisema.
Unyenyekevu ni katika ibada bora kabisa na ni katika utii uliotukuka sana. Kwa sababu hii, Allah ametilia mkazo ndani ya kitabu chake kuwa unyenyekevu ni katika sifa za waumini, kama alivyosema kuwa: «Hakika, Waumini wamefaulu, ambao wao katika swala zao ni wanyenyekevu». (Sura Almuuminuun, aya 1-2).
Mwenye kuwa na na unyenyekevu katika swala ataonja ladha ya ibada na iman. Kwa sababu hiyo, Mtume wa Allah,swallalahu alayhi wasalam, alikuwa akisema kuwa: «Na burudani yangu imewekwa katika  swala». (Annasai, Hadithi Na. 3940). Burudani ina maana ya kiwango cha juu cha furaha, faraja, kuliwazika na kustareheka.
Thawabu katika swala zinapatikana kwa kadiri ya unyenyekekevu ndani yake.

Nyenzo zinazosaidia kuwa na unyenyekevu ndani ya swala

Kuna nyenzo nyingi zinazosaidia kupata unyenyekevu wakati wa kuswali. Miongoni mwa nyenzo hizo ni hizi: 
  1. Kujiandaa na kujitayarisha kwa ajili ya swala: 
Hilo linatimia kwa kwenda mapema msikitini kwa wanamume, kufanya ibada za sunna zilizo kabla ya swala, kuvaa nguo nzuri za heshima, kwenda msikitini katika hali ya utulivu na unyenyekevu.
  1. Kujiepusha na vitu vyote vyenye kushughulisha na kusumbua:
Mtu hatakiwi kuswali hali ya kuwa mbele yake kuna picha au vitu vinavyoshughulisha, na wala asiingie katika swala hali ya kuwa anasikia sauti zinazomshughulisha. Pia hatakiwi kuingia katika swala huku akiwa amebanwa na haja, au akiwa na njaa au kiu na mbele yake kuna chakula au kinywaji. Hatua zote hizo zimewekwa ili akili ya anayeswali iwe safi na aweze kushughulika na jambo kubwa lililoko mbele yake na ambalo ni swala yake na kuzungumza kwake na Mola wake. 
  1. Utulivu katika swala:
Mtume,swallalahu alayhi wasalam, alikuwa mtulivu wakati akirukuu na kusujudu mpaka kila kiungo kinakaa mahali pake. Alimuamrisha mtu ambaye alikuwa hajui kuswali vizuri awe mtulivu katika vitendo vyote vya swala. Amekataza kuharakisha na akafananisha kitendo hicho na papara ya kunguru.  
Mtume,swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwizi mbaya kabisa kuliko watu wote ni yule anaye iba katika swala yake. Swahaba wakauliza: Ewe Mtume wa Allah: Vipi mtu anaiba katika swala yake? Mtume akajibu: Ni yule mtu asiyetimiza rukuu yake na sijida yake». (Ahmad, hadithi Na. 22642).
Mtu ambaye hana utulivu katika swala yake hawezi kuwa na unyenyekevu, kwa sababu haraka huondosha unyenyekevu, na papara ya kunguru huondosha thawabu.
  1. Mtu kuchunga heshima mbele ya Mola wake:
Mtu anatakiwa akumbuke ukubwa na utukufu wa Muumba, na pia akumbuke udhaifu na udhalili wake, na kwamba anasimama mbele ya Mola wake akizungumza naye na akimuomba kwa unyenyekevu, unyonge na udhalili. Anatakiwa akumbuke thawabu ambazo Allah amewaandalia Waumini, na adhabu ambazo amewaandalia Makafiri huko Akhera. Pia akumbuke jinsi atakavyo simama mbele ya Mola wake huko Akhera.
Muumini akiwa katika hali hii ndani ya swala yake atakuwa kama wale ambao Allah amewasifu katika kitabu chake kwamba wanaamini kuwa watakutana na Mola wao. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Na kwa yakini kabisa, hiyo swala ni jambo kubwa (zito) isipokuwa kwa wenye unyenyekevu. Ambao wanadhani (wanaamini) kuwa  watakutana na Mola wao, na kwamba wao watarejea kwake». (Sura Albaqara, aya 45-46)
Mwenye kuswali akitambua kuwa Allah anamsikia, anampa (neema mbali mbali) na anamjibu (maombi yake) atapata unyenyekevu kwa kiasi cha kutambua kwake.
  1. Kuzingatia aya zinazosomwa na nyiradi nyingine za swala, na kuzifanyia kazi:
Qur`ani imeshushwa ili izingatiwe. «(Hiki) Ni kitabu chenye baraka, tumekiteremsha kwako ili watu wazizingatie aya zake, na wenye akili wapate onyo».(Sura Saad, aya 29). Uzingatiaji haupatikani isipokuwa tu kwa kujua maana ya aya, nyiradi na dua zinazosomwa.  Hapo, itawezekana kwake kufikiria hali yake na uhalisia wake kwa upande mmoja, na kufahamu maana ya aya na nyiradi hizo kwa upande mwingine. Kutokana na hilo, utapatikana unyenyekevu na kuguswa, na pengine hata macho yake yakabubujikwa na machozi. Haziwezi kumpitia aya bila ya kuguswa nazo, kama kwamba hasikii wala haoni.  Allah Mtukufu amesema kuwa: «Na wale ambao wakikumbushwa aya za Mola wao hawajifanyi hamnazo (hawazipuuzi)». (Sura Alfurqan, aya 73).

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU