Umama (Utunzaji Wa Watoto) KAtika uislam

Umama (Utunzaji Wa Watoto)

Mojawapo ya wajibu wa wanawake ni kutunza watoto wao. Hii si kazi rahisi lakini ni nyeti na muhimu. Ni wajibu wenye heshima na thamani kubwa uliowekwa kwa wanawake kwa amri ya muumbo. Yapo mambo machache ambayo yametajwa hapa kuhusu suala hili:
Tunda la Ndoa - licha ya kwamba mwanaume na mwanamke wanaoana kwa sababu chache kama vile kwa sababu ya ushawishi wa kijinsia, mapenzi na kadhalika, kupata mtoto si sababu mojawapo muhimu ya ndoa.
Lakini huwa haipiti muda mrefu kabla ya nia ya kweli ya maumbile ya asili kudhihirika na mapenzi ya kupata mtoto hukua ndani ya nyoyo zao. Kuwepo kwa mtoto ni tunda la mti wa ndoa na matamanio ya asili ya wanaume na wanawake. Ndoa isiyokuwa na mtoto ni sawa na mti usiokuwa na tunda. Mtoto huimarisha mfungamano wa mapenzi baina ya wanandoa. Huwa kama msukumo kwa maisha ya mwanamume kufanya kazi na hutia moyo wazazi kutunza familia yao.

Wakati mwingine ndoa hutokana na matamanio ya kijinsia ya papo kwa papo. Msingi wa aina hiyo si sahihi na haudumu na kila mara huelekea kwenye uharibifu. Kipengele kinachoimarisha msingi huu ni kuwepo kwa mtoto. Matamanio na msukumo wa kijinsia hufifia haraka sana. Kumbukumbu moja tu inayoendelea kuwepo kuhusu matamanio ya kijinsia ingekuwa watoto, ambao kuwepo kwao huchangamsha nyoyo za wazazi.
Imamu Sajjad (a.s) alisema: “Furaha ya mtu ni kupata watoto wachamungu ambao anaweza kupata msaada kutoka kwao.”
Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) alisema: “Mtoto mcha Mungu ni mmea unao nukia harufu tamu kutoka miongoni mwa mimea ya Peponi.”
Mtume (s.a.w.w) alisema: “Ijumlishe kwenye idadi ya watoto wenu, kwa sababu mimi, Siku ya Hukumu, nitahisi nimeheshimiwa kuhusu ukubwa wa idadi yenu kuzidi umma zingine.”
Ni wajinga kiasi gani wale ambao, wakiwa na udhuru mbali mbali hukataa kupata watoto, na hivyo hupinga kanuni ya uumbaji!
Kumwelimisha mtoto: Wajibat ambazo ni nyeti kuliko zote za mama ni kazi ya kumwelimisha mtoto na kuwaelekeza. Licha ya kwamba wazazi wote wawili wanatakiwa kugawana wajibu huu, uzito mkubwa zaidi upo kwa mama. Hii ni kwa sababu mama anao uwezo wa kumlinda na kumfuatilia mtoto wakati wote. Kama mama, kwa kupitia kwenye utaratibu ulio sahihi hujaribu kulea watoto wao, halafu taifa lote na hata dunia ingepita kwenye mabadiliko ya kimapinduzi.
Hivyo, maendeleo au kutokuendelea kwa jamii ni mambo ambayo yapo mikononi mwa wanawake. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) alisema: “Pepo iko chini ya nyayo za mama.” Watoto wadogo wa leo ndio wanaume na wanawake wa kesho. Masomo yoyote wanayo jifunza sasa, watayafanyia mazoezi katika jamii zijazo. Kama familia zinaendelea, jamii itaendelea kwa sababu jamii itaendelea kwa sababu jamii ni mkusanyiko wa familia nyingi. Dunia ya kesho itaumia kwa sababu ya kuwepo watoto wenye hasira, jeuri, wajinga, woga, wapenda dunia, wabaya, wazembe, wachoyo na katili.
Kinyume chake dunia ya kesho itafaidika kwa sababu ya kuwepo leo watoto ambao ni waaminifu, wenye tabia njema, wema, jasiri, wapenda haki, wa kutegemewa na kadhalika.
Kwa hiyo, kwa ujumla, wazazi na hasa zaidi mama wanao wajibu kwa jamii zao. Wanaweza kuhudumia jamii zao kwa kulea na kukuza watoto wachamungu. Kwa upande mwingine, uzembe katika utekelezaji wa wajibu wao utahojiwa Siku ya Hukumu.
Imamu Sajjad (a.s) alisema: “Haki ya mtoto wako ni kwamba unatakiwa kutambua kwamba anatoka kwako.
Awe mzuri au mbaya anao uhusiano na wewe. Wewe unawajibika kumlea, kumsomesha na kumuonesha njia inayo elekea kwa Mwenyezi Mungu na kumsaidia awe mtiifu.
Unatakiwa kumshughulikia kwa namna ambayo kwamba ukimtendea wema, utakuwa na uhakika wa kupata thawabu na kama ukimfanyia ubaya, uwe na uhakika wa kuadhibiwa.”
Kama mambo yalivyo, si mama wote ambao wanatambua umuhimu wa stadi za kumwelekeza mtoto na ndio sababu wanatakiwa kujifunza na kuzijua stadi hizo.
Si katika eneo la kitabu hiki kuweka maelezo ya kina kuhusu malezi ya mtoto. Kwa bahati nzuri, vipo vitabu vingi ambavyo vimeandikwa na waandishi na wasomi kuhusu somo hili. Wanawake wanaweza kununua vitabu hivi na kwa msaada wa uzoefu wao wenyewe, wanaweza kuwaelimisha watoto wao na hata kuwa mabingwa katika fani ya malezi ya mtoto. Mama mmoja bingwa anaweza kuwasaidia mama wengine katika kazi zao kuhusu watoto wao.
Hapa linatakiwa kutajwa jambo moja. Watu wengi hufanya kosa kuhusu maneno mawili: ‘elimu’ na ‘maelekezo,’ au hudhani yana maana moja. Lakini mtu anatakiwa kujua kwamba kumfundisha mtoto masomo mbali mbali kama vile hadith zinazo faa, mashairi, Qur’ani, Hadith za Mtume
(s.a.w.w) na Maimamu (a.s) si kumwelimisha. Masomo kama haya yanafaa lakini mtoto si tu ajifunze kuhusu watu waaminifu, lakini yeye mwenyewe anatakiwa kuwa mwaminifu.
Hivyo, lazima tutengeneze hali ya mazingira ya maisha ambayo mtoto kwa kawaida atakuwa mtu mwaminifu na mchamungu. Kama mtoto atakuwa mtu mwaminifu na mchamungu. Kama mtoto atakuwa kwenye mazingira ya uaminifu, ukweli, ujasiri, nidhamu, usafi, wema, upendo, uhuru, haki, uvumilivu kutegemewa, utiifu na kujitoa muhanga, basi hujifunza yote hayo. Kwa upande mwingine, mtoto anayepata makuzi akiwa katika mazingira ya uovu, udanganyifu, hasira, chuki, uaminifu na uasi hataepuka kuathiriwa na mambo hayo. Mtoto kama huyu anaweza kujifunza hadith nyingi, lakini hatanufaika nazo.
Wazazi wasio waaminifu kulea na kukuza watoto waaminifu kwa kuwafundisha Qur’ani na Hadith.
Mama na baba waovu kwa kweli humfundisha mtoto wao kuwa muovu. Mtoto huzingatia zaidi matendo ya wazazi wake na si maneno yao.
Kwa hiyo, wale miongoni mwetu ambao wapo makini kulea watoto waaminifu na wema, lazima kwanza warekebishe tabia zao wenyewe. Hii ndio tu njia ya kumwelimisha mtoto anufaike yeye mwenyewe na jamii yake.

Lishe Na Afya

Wajibu mwingine muhimu wa mwanamke aliye olewa ni kuwapa chakula watoto. Afya nzuri au ugonjwa, uzuri au ubaya, hata tabia njema au mbaya na ujanja wa watoto, vyote hivi vina uhusiano na lishe wanayopewa.
Watoto wana mpangilio tofauti wa kula kulinganisha na watu wazima.
Watoto wanayo mahitaji mbali mbali katika umri tofauti na kwa hiyo mama wanatakiwa kulifikiria jambo hili wanapo wapa chakula watoto wao.
Chakula kizuri sana na chenye kurutubisha sana ni maziwa. Maziwa yana kila kitu kinachohitajiwa kwa ajili ya mwili wenye afya. Hivyo, hakuna chakula kinachomfaa mtoto mchanga isipokuwa maziwa ya mama yake. Kwa kuwa maziwa yana viambato ambavyo vinafaa kwenye mfumo wa mmeng’enyo wa chakula wa mtoto mchanga, kwa hiyo hakuna matatizo ya kumlisha mtoto mchanga maziwa ya mama yake. Zaidi ya hayo, mama hahitaji kuchemsha, kuondoa, vijidudu au kuyasafisha kabisa maziwa hayo. Hakuna wasi wasi wa uhalisi wake.
Imamu Ali (a.s) alisema: “Hakuna chakula kizuri zaidi na kingi zaidi kuliko mazia ya mama kwa mtoto mchanga.”
Daktari A.H. Mkuu wa Eastern Maditeranean Region of World Health Organization wa zamani alisema: “Mojawapo ya kipengele muhimu ambacho husababisha mtoto apatwe na maradhi mengi ni kutokupata maziwa ya mama yake ambayo ndio tu bima ya maisha ya mtu.”
Hivyo, mama wanao nyonyesha watoto wao maziwa yao lazima wakumbuke lishe muhimu kwa watoto wao imo kwenye maziwa hayo.
Lakini maziwa yenye lishe bora ni yale tu yanayotokana na lishe bora ya mama, ubora wa maziwa yake yanahusiana na ubora na wingi wa chakula cha mama. Mama akipata chakula bora zaidi ndivyo na maziwa yake yatakavyokuwa. Mama wanao wanyonyesha watoto wao maziwa yao, kutokana na uzembe wao kuhusu lishe bora wanaweza kuharibu afya zao na zile za watoto wao.
Baba wanaolea watoto wachanga pia wanao wajibu wa kuwapa wake zao chakula cha kutosha na kilicho bora. Utapiamlo ni tatizo kubwa kwa watu wengi kuboresha na mtu hatakiwi kudharau jambo hili au vinginevyo awe tayari kulipa, kugharamia tiba ya maradhi yanayosababishwa na hali hii.
Unaweza kupata taarifa ya kutosha kuhusu somo hili kutoka kwa daktari wako wa tiba au vitabu vinavyo husiana nalo. Lakini kama sharti la ujumla mama anaye nyonyesha anatakiwa kula aina zote za vyakula kuanzia nyama, matunda, vyakula vitokanavyo na maziwa… mpaka mboga za majani.
Ukweli ulio muhimu ni kwamba maziwa ya mama huathiri tabia ya mtoto na ndio sababu Imamu Ali (a.s) alisema: “Msichague wanawake wapumbavu kunyonyesha watoto wenu maziwa yao, kwa sababu maziwa hufanya asili ya ubora wao kupenyezwa kwa mtoto.”
Imam Baqi (a.s) alisema: “Chagueni wanawake waungwana kunyonyesha watoto wenu maziwa yao, kwa sababu asili ya ubora wa maziwa unapitishwa kutoka kwa mnyonyaji hadi kwa mtoto.”
Lazima umnyonyeshe mtoto kwa vipindi. Mtoto wako hupata mazoea kutokana na ulinganifu huu na kumsaidia kuwa mvumilivu. Pia humsaidia kuhusu kuboresha mpangilio wa mmeng’enyeo wa chakula na tumbo. Kwa upande mwingine, kama utamnyonyesha mtoto kila anapolia basi, hatajifunza kuwa na nidhamu. Kama mtoto akizoea kupata atakacho kwa njia ya kulia basi ataichukua tabia hii na kuutumia hata atakapokuwa mtu mzima.
Hatakuwa na umuhimu wa kuvumilia atakapo kabiliwa na shida. Ama atatumia nguvu ili afanikishe matamanio yake au atafadhaika akipatwa na matatizo.
Usidhani kwamba kumfundisha mtoto nidhamu ni kazi ngumu. Lazima uwe mvumilivu na utaratibu unaofaa wa kumwelekeza kufuatana na kiwango chako. Wataalam wa lishe ya mtoto wanasema kwamba mtoto mchanga lazima anyonyeshwe kila baada ya saa tatu au nne.
Mpakate mtoto unapomnyonyesha. Kwa kumkumbatia mtoto anahisi mapenzi yako na inaweza kuathiri hata utu wake. Usimnyonyeshe mtoto mchanga wakati umelala chini kwa sababu imeonekana kwamba mama wengine hulala usingizi wakati wa kunyonyesha na matokeo yake watoto wengine wamekosa hewa kwa sababu matiti ya mama zao yaliwazuia kupumua.
Kama wewe mwenyewe huna maziwa kabisa unaweza kutumia maziwa ya ng’ombe ni mazito zaidi ya binadamu, pia lazima uongeze maji kiasi fulani. Pia unaweza kutumia maziwa yaliyosafishwa, ambayo lazima uyachemshe kwa muda wa dakika ishirini au hadi yanapokuwa salama kutumiwa na mtoto.
Usimnyonyeshe mtoto mchanga maziwa ya baridi au moto, lakini yanatakiwa yawe na joto sawa na yale ya binadamu.
Kila baada ya kunyonya lazima chupa na nyonyo zichemshwe kwenye maji na uangalifu wa ziada lazima ufanywe wakati wa majira ya joto. Uwe mwangalifu usitumie maziwa yaliyobakia au yaliyochacha. Ni vema kupima wingi wa maziwa katika kila kipindi cha kunyonya ili kuhakikisha kwamba mtoto wako anapata maziwa ya kutosha.
Katika kutumia maziwa ya unga unatakiwa upate ushauri kutoka kwa bingwa wa magonjwa ya watoto. Kila mara lazima utumie maziwa ya unga mapya.
Baada ya mwezi wa nne wa umri wa mtoto, unaweza kuanza kumyonyaesha maji ya matunda. Baada ya umri wa miezi sita, pia unaweza kuanza kumlisha vyakula vikavu na supu. Unaweza kumlisha bisikuti na mkate mtamu. Maziwa mtindi na jibini hufaa. Pole pole unaweza kuanza kumpa mtoto kiasi kidogo cha chakula chako.
Kumbuka kwamba mtoto wako mchanga huhisi kiu mara nyingi kama wewe. Kwa hiyo, mnyweshe maji, lakini sio chai au kahawa. Matunda, mboga na supu ni vyakula vyenye manufaa maalum kwa mtoto mchanga anayekua.
Usisahau kuwa safi kuhusu malazi ya mtoto, nguo zake na nepi zake. Mnawishe uso na mikono yake mara nyingi. Muogeshe katika vipindi vya kawaida, kwa sababu watoto wachanga ni rahisi sana kuugua kwa sababu ya uchafu na vijidudu.
Lazima watoto wapate chanjo ya kinga dhidi ya maradhi ya ndui, tetekuwanga, kifadulo, kiharusi cha watoto (polio), homa ya vipele
vyekundu, surua, dondakoo. Kwa bahati nzuri chanjo zipo zinapatikana kwenye hospitali na vituo vya afya kwa urahisi. Unaweza kuwa na watoto wenye afya njema kwa kushika kanuni za elimusiha na usafi.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU