Uislamu unautazama vipi Ubaguzi wa Kimbari?

Dear Brother / Sister,
Aya ifuatayo inakataza ubaguzi wa kimbari:
Enyi watu! Hakika Sisi tumekuumbeni kutokana na mwanamume na mwanamke. Na tumekujaalieni kuwa ni mataifa na makabila ili mjuane. Hakika aliye mtukufu zaidi kati yenu kwa Mwenyezi Mungu ni huyo aliye mchamngu zaidi katika nyinyi. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua, Mwenye khabari. (Surah Al-Hujuraat, 13)
Katika surah hiyo hiyo, yanaelezwa yafuatayo:
“Waumini ni ndugu: Basi fanyeni amani na upatanishi baina ya ndugu wawili (wanaopingana).”
Kama inavyofahamika kutokana na aya za hapo, Allah anawachukulia waumini tu ndio ndugu na si watu wa mataifa mengine. Kwa mujibu wa Uislamu, mtu asiye muumini hawezi kuwa mrithi wa baba yake muumini. Kusipokuwepo imani, basi mahusiano ya kidunia, kimfumo na ya kimbari hukosa umuhimu wake.
Mtume wa Allah (s.a.w), ambaye amesema, “Hakuna muumini wa kweli isipokuwa humpendelea nduguye anachokipenda kwa ajili yake mwenyewe”, anatuelekeza jinsi aya hii ilivyo na mwangaza katika amali zetu na msisimko.
Nini kifanyike pindi chuki na uadui unapotokea kati ya waumini ilhali walitakiwa wapendane? Mwendelezo wa aya hiyo unaagiza yafuatayo: “fanyeni amani na mapatano baina ya ndugu wawili (wanaogombana).” Uhasama wao ugeuke kuwa urafiki, upendo na undugu.
Ndiyo, kwa mujibu wa amri ya Qur’an, waumini wote ni ndugu kwa kila mmoja. Wao ni familia moja. Juu ya mstari mmoja. Watu wanaowatenganisha huchukuliwa kuwa wamewafanyia kazi maadui kwa kujua au kutokujua.

Fundisho la Allah kutoka katika surah Hud: katika tukio la gharika ya Nuh, pindi Nuh aliposema, “Ewe Allah! Mwanangu pia ni wa familia yangu. (Uzao wangu)” Ewe Nuh, yeye si wa familia (uzao) yako.” Hivyo mtoto kafiri na mwasi hahesabiki kuwa ni katika uzao wake. Kisha, kafiri kutoka katika mbari yake hawezi kuwa rafiki au ndugu yake. Hapa kunahusiana na aya kutoka kwa Allah ambako hakuna nafasi ya upotoshaji wa tafsiri kwa makusudi:
Enyi mlio amini! Msiwafanye baba zenu na ndugu zenu kuwa vipenzi vyenu ikiwa wanastahabu ukafiri kuliko Imani. Na katika nyinyi atakaye wafanya hao ndio vipenzi vyake, basi hao ndio madhaalimu.” (Surah at-Taubah, 23)
Aya hii pia inatoa maelezo ya aya, “Waumini ni ndugu mmoja” ambapo kuna ufahamu mzuri na wa kina.
Baba yako au kaka yako asiyeamini si rafiki yako.
Wale wanaofanya urafiki nao wanachukuliwa kuwa wamesaliti ukweli na wamedhulumu.
Anazingatiwa kuwa ametumia hisia yake ya upendo, aliyozawadiwa na Allah, katika sehemu isiyosahihi na amedhulumu …
Amejipeleka mwenyewe Motoni kwa maamuzi yake yasiyo sahihi. Ameidhulumu nafsi yake.
Kwa kufanya hivyo, kafiri anapata nafasi bora zaidi moyoni mwake kuliko muumini na anakuwa mkandamizaji kwa dhuluma yake kubwa. 

Allah ambaye ndiye “Malik Yawm ad-Din” (Mwenye Kumiliki Siku ya Malipo.anaeleza yafuatayo: Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana. Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi...” (Surah ash-Shuara, 88-89)
Je, uhusiano baina ya mwana na baba si hatua ya kwanza na ya kiwango cha juu cha ukaribu wa kimbari? Aya hii inatujulisha kuwa ukaribu huo hauna thamani kabisa katika Siku ya Hukumu. Kwa hivyo, ubaguzi wa kimbari una thamani gani katika nukta hii? Katika siku hiyo, si mali wala idadi ya watoto wa mtu yeyote watakaokuwa na thamani yoyote.
Katika siku hiyo, kitu pekee kitakachokuwa na thamani ni nafsi iliyojisalimisha. Moyo safi wa mtu uliojisalimisha na kuwa mtumwa wa amri za Muumbaji wake. Nafsi ambayo haikuathiriwa na chochote kingine isipokuwa Yeye. Nafsi hii ina thamani kubwa bila ya kujalisha mwenye kuimilki. Na Peponi ni mahali ambapo malipo yatatolewa kwa nafsi zilizojisalimisha. Kila muumini atapewa nafasi kulingana na ikhlas (unyoofu) yake, amali, maadili na lengo lake huko. Nafasi zote zilizo huko ni kulingana na thamani hizo. Huko hakuna nafasi tofauti kwa ajili ya mbari mbalimbali.
Maswali juuyau islamu

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU