Tawhid (Umoja wa Mwenyezi Mungu) ina maana gani?

Umoja wa Mwenyezi Mungu maana yake ni: kuamini kutokuwepo kwa mungu yoyote isipokuwa Allah , kwa “kusema maneno laailah illah - Hakuna Mola ila Allah.”
Papo hapo umoja unatukumbusha kuhusu tamko laaillah ilaallah . Hili huitwa neno la upwekesho na maana yake ni kwamba hakuna mola wa kweli wa kuabudiwa isipokuwa Allah.
Malinganisho kadhaa yamefanywa kuhusu uwepo wa ulimwengu huu. Moja kati ya hayo ni kasri la ulimwengu. Kwa hivyo, umoja ni kumjua mfalme wa kasri hili kwamba ni mmoja na kutomshirikisha na yoyote.
Juu na chini ya kasri ya ulimwengu hakuwezi kumilikiwa na dhati tofauti. Taa, na vitu vingine vya ndani ya kasri haviwezi vikawa vimeletwa kutoka dunia nyengine na kuwachwa hapa. Kila kitu katika kasri na muhimu kuliko vyote, kila mgeni, anazaliwa katika kasri hii. Hebu tuangalie ua: kutokea katika dunia hadi katika jua, kila kitu kina mchango ndani yake. Na hebu tuuangalie mwili wa mwanadamu sehemu zake ambazo ni mawe ya msingi katika kasri hili, yapo ndani yake pia.
Milima huanzishwa juu ya tambarare kama viti vya kuegemeza mikono, kwa kutoletwa kutoka sehemu nyengine, bali huchomoza kutokea sehemu tambarare. Matunda yameambatana na matawi, kwa kutotokea kutoka katika nchi nyengine, bali yamekuja kutoka katika mti.
Mtoto huwa juu ya mapaja ya mama yake, hakuletwa kutoka katika nchi nyengine anakuwa katika fuko lake la uzazi. Jua ni taa ya kasri hili; halikununuliwa kutoka sehemu nyengine bali limeumbwa pamoja na mbingu.
Katika dunia hii, viumbe visivyo hisabika huungana na baina yao mchanganyiko hutokea na dunia hii ya viumbe hupewa muundo wa kasri. Watu wanaoakisi njia hii husoma neno la umoja na kufahamu kwamba kasri hili ni mali na kiumbe cha Allah pekee.
Wakati neno la umoja likiwa na maana ya kwamba hakuna mola wa kweli wa kuabudiwa isipokuwa Allah, jina la Allah linakusanya majina yote ya kiungu kwa hivyo, hubeba maana kama hakuna anayetoa maisha isipokuwa Allah hakuna muumbaji isipokuwa Allah hakuna isipokuwa Allah. Na kama hivi ndani ya umoja kuna wingi wa umoja kwa idadi ya majina ya kiungu.
Baadhi ya wanachuoni huugawa umoja katika sehemu mbili umoja unaogemea katika elimu na umoja unaegemea katika matendo. Kwa mujibu wa mgawanyo huu, kujua kwamba Allah ni mmoja na kwamba vitu vyote vilivyokua katika hali ya umoja ulimwenguni vinaonesha umoja wake ni umoja unaoegemea katika elimu. Umoja unaoegemea katika matendo ni umiliki wa imani hii ya umoja kwa ukamilifu ndani ya ulimwengu wa matendo wa mwanadamu.
Aya, “Iyyaka na’budu wa iyyaka nastain” Wewe tu ndie tunakuabudu, na Wewe tu ndie tunayekuomba msaada. Ya sura al-fatiha inatufundisha umoja unaoegemea katika matendo. Tunaelekea upande ambao wewe unataka tunasimama kwa heshima ya uwepo wako tu; tunainama na kukusujudia Wewe tu. Tunafikiria kuhusu mambo unayoyaridhia na tunawapenda wale tu unaowaridhia.
Mtu anayemuabudu Allah pekee anakua amewekwa huru kutokana na udhalili wa kuabudia miungu wa uongo; mtu anayetafuta msaada wa Allah pekee huwa huru na kuabudia sababu na huwa huru pia na kua mtumwa wa matukio. Huomba msaada kutoka kwa mola hali ya kuwa akiwa na utegemezi kamili hii ni yote mawili furaha na nguvu ya ushindi.
Kwa kuongezea, njia ya kuwa muumini kamili ni kwa kupitia ukamilifu katika
umoja unaoegemea elimu na umoja unaoegemea matendo.
Umoja hauishii katika mambo hayo tu. Umoja wa sifa, majina na matendo pia upo. Aina hizo zinaweza kufupishwa kama ifuatavyo:
Umoja wa matendo: “Kujua kwamba sababu hazina taathira katika uumbaji wa vitu na katika kuviongoza”, “kuamini kwamba wa pekee ni Allah pekee.”
Umoja wa matendo: “Kufahamu kwamba sifa kama elimu, nguvu, utashi ambazo zinaambatana na viumbe nazo pia ni viumbe wa Allah na sio kuzipa dhati ya kujitegemea.
Umoja wa dhati: “Kufahamu kwamba viumbe vyote havina uwepo unapovilinganisha na dhati yake na uwepo wake.”
Kuhuisha na kufisha, kuponya, kuongoza katika njia sahihi, kutoa chakula kila moja ni kitendo tofauti. Matendo haya yasiyo na ukomo hutegemea sifa hizo hizo. Sifa hizo ni uhai, elimu, nguvu, kusikia, kuona utashi, kuongea na kuumba. Hivyo umoja wa matendo ni kufahamu kwamba matendo yote ya tangu ambayo yanafanya kazi katika ulimwengu wa uumbaji huja kutokana na sifa hizi za kiungu na kuzirejesha sifa hizi kwa dhati moja peke yake ni umoja wa dhati.
Maswali juuyau islamu

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU