Talaka

Licha ya kwamba talaka ni kitendo halali, ni kitendo kinacho chukiza na ni kibaya kuzidi vitendo vyote.
Imam Sadiq (a.s) alisema: “Oeni lakini msitalikiane, kwa sababu talaka inaweza kutetemesha Arsh ya Mwenyezi Mungu.”
Imam Sadiq (a.s) pia alisema: “Mwenyezi Mungu huipenda nyumba ambayo inakaliwa na wanandoa na huchukia nyumba ambayo wanandoa wametalikiana. Hakuna kitendo kinacho mchukiza Mwenyezi Mungu kuliko kutalikiana.”
Ndoa si kama kununua jozi ya viatu au soksi ambapo vitu hivi vikichujuka kwenye matamanio ya mmiliki wake, huvitupa na kununua jozi nyingine ya viatu. Ndoa ni makubaliano ya kiroho ambayo hufanywa na watu wawili kwa lengo la kuishi pamoja kama marafiki wa kuliwazana, na wapenzi hadi kifo chao. Makubaliano haya yameegemezwa kwenye matumaini haya hivyo kwamba msichana huwaacha wazazi wake na kuungana na mume wake.
Mwanaume hufanya jitihada na kufanya bidii kwa msingi wa makubaliano hayo ya kimungu. Hulipa gharama za harusi yake na hununua vitu muhimu kwa ajili ya maisha yake mapya na hufanya kazi kwa ajili ya faraja ya familia yake.
Ndoa si jambo la kukata kiu cha tamaa ya kimwili na wanandoa hawawezi kuiharibu kwa visingizio vidogo. Licha ya kwamba kutalikiana ni tendo halali, linachukiza sana na watu wanashauriwa kuepukana nalo kadiri iwezekanavyo.
Bahati mbaya, tendo hili ambalo linachukiza sana, limekuwa jambo la kawaida sana kwenye nchi za kiislamu na misingi ya familia imetikisika sana, hivyo kwamba kwa ujumla watu hawana imani tena kuhusu ndoa.
Kuvunja ndoa inaruhusiwa hapo tu ambapo hali si ya kawaida na inalazimu iwe hivyo.
Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) alisema: “Malaika Jibril aliniusia kuhusu wanawake sana hivyo kwamba nilifikiri kwamba wanamume wasiwataliki isipokuwa kama wanazini.”
Kesi nyingi za kutalikiana hazina sababu za msingi, isipokuwa visingizio visivyo komaa. Yaani, sababu za kesi nyingi zaidi za talaka ni hafifu na hazifai kuwaathiri na kuwatenganisha wanandoa. Mume au mke, kwa sababu ya ubinafsi, anaweza kukuza jambo dogo na kuamua kwamba maisha yao ya ndoa lazima yakome.
“Bibi fulani mwenye umri wa miaka ishirini na nne, alimwambia mumewe awaalike wazazi wake kwenye chakula cha jioni chenye gharama kubwa. Kwa kuwa hakutekelezewa ombi hilo, alidai talaka.”
“Mwanaume alimtaliki mke wake kwa sababu alikuwa anazaa watoto wanawake tu. Wanandoa hawa walikuwa na watoto wanawake watano.”
“Mwanamke aliomba talaka kwa sababu mume wake aliamini mafundisho ya kumfikiri Mungu kwa njia ya tafakuri na hakuonesha kupenda maisha.”
“Mwanamume alidai talaka kwa sababu alitaka kumuoa mwanamke tajiri.”
“Mwanamke aliomba talaka kwa sababu mume wake alikuwa na tabia ya kuficha fedha zake kwenye mikono ya shati.”
“Mwanaume alimtaliki mke wake kwa madai kwamba ana balaa tangu walipooana baba wa mume alifariki na ami yake alifilisika.”
Wanandoa ambao hawana heshima na busara, wanaweza wakanasa kwenye mtego wa mambo madogo kama hayo na kudai talaka.
Wanandoa wanaotaka kutengana, wasifanye haraka kutelekeza jambo hilo. Wanashauriwa wafikiri kwa uangalifu kuhusu athari na maisha yao ya baadaye kwa makini na halafu waamuwe. Hususan lazima watafakari kuhusu mambo mawili:
Jambo la kwanza: wanandoa wanaotaka kutalikiana kwa kawaida hutaka kuoa au kuolewa tena. Lakini lazima wakumbuke kwamba baada ya kutalikiana, watu wanaojulikana kama watalaka hawatakuwa na sifa nzuri kuhusu ndoa. Watu huwafikiria kuwa wenye ubinafsi na si waaminifu.
Baada ya kupata taarifa ya maisha ya ndoa ya siku za nyuma ya mwanamume na kutaliki, mwanamke anaweza kuwa na shaka kuhusu uaminifu wa mwanaume au tabia yake.
Mwanamke mtalaka ni nadra sana kupata fursa ya kuolewa tena. Kwa sababu wanaume kwa kawaida hawaoneshi kuvutiwa sana kuoa mwanamke mtalaka na hutilia shaka kuhusu uaminifu wake.
Kwa hiyo, mtalaka anawezekana akaishi peke yake kwa muda wote wa maisha yake na atateswa na upweke pia.
Kuwa mpweke ni hali ngumu sana na watu wengine wapweke hupendelea zaidi kifo kuliko maisha ya aina hiyo yasiyovumilika.
Mwanamke wa miaka ishirini na mbili ambaye aliachika, alijaribu kujiua mnamo usiku wa siku ya harusi ya dada yake. Alikuwa na mtoto mmoja.
Hata kama mwanaume anafaulu kuoa tena, haitajulikana kabisa kwamba maisha yake mapya yatakuwa mazuri zaidi kuliko ya mke wake wa mwanzo. Mke wake wa pili anaweza kuwa mbaya zaidi. Mwanaume wa aina hii hupendelea kumtaliki mke wa ndoa ya pili na kurudi kumuoa mke wa kwanza. Lakini kwa kawaida huwa wamechelewa sana.
Mwanaume wa miaka themanini alisema mahakamani; “Nilikuwa na maisha mazuri nilipomuoa mke wangu wa ndoa ya kwanza, takriban miaka sitini iliyopita. Lakini baada ya muda alianza kunifanyia ubaya kwa hiyo nikamtaliki. Nilioa wanawake wachache baada ya hapo lakini nilihisi kwamba mke wangu wa kwanza alikuwa mwaminifu zaidi miongoni mwao. Nilimuona na nikampa rai ya kurudiana naye. Yeye, ambaye pia alichoka maisha ya upweke alikubali na sasa tunataka kuoana tena.”
Mwanaume alimtaliki mke wake wa pili kwa sababu hakutaka kuwalea watoto wawili aliozaa kwenye ndoa yake ya kwanza. Halafu akaamua kumuoa tena mke wake wa kwanza ambaye alimtaliki miaka mitano ya nyuma.’ Jambo la pili: Wanandoa ambao wanataka kutengana lazima wafikirie pia suala la watoto wao. Faraja ya watoto imo kwenye familia yenye wazazi wote wanao ishi pamoja na wanawalea kwa pamoja.
Baada ya kuvunjika kwa maisha ya familia, watoto hufadhaika sana. Kama ni baba yao tu anaye watunza, hawatakuwa na maisha na mama yao wa kambo. Mama wa kambo si tu kwamba wanashindwa kutekeleza kama mama halisi, lakini wanaweza kufikiri watoto wa kambo ni mzigo. Mama wa kambo wengine huwanyanyasa watoto wa kambo na kuwafadhaisha kwa kukusudia na baba zao hunyamaza kimya.
Bibi harusi wa miaka kumi na nne ambaye alitaka kujiua alisema akiwa hospitalini. Wazazi wangu walitengana nilipokuwa na mwaka mmoja.
Baba yangu alioa tena baada ya mwaka mmoja na nusu na sasa tunaishi wote. Mama yangu wa kambo alikuwa na desturi ya kunipiga na hata alinichoma moto kwa chuma mara kadhaa. Baba yangu licha ya kuwa na uwezo wa kifedha alinikataza nisisome. Takriban mwezi mmoja uliopita baba yangu alinioza kwa mtu mwenye umri wa miaka arobaini na tano.
Msichana wa miaka kumi na tatu alijinyonga. Msichana huyu aliishi na kaka zake wawili. Mmojawapo wa hao kaka zake alisema; “Wazazi wetu walitengana miaka takriban mitatu iliyopita. Mama yangu aliolewa tena na mwanamume mwingine na baba alikufa miezi miwili iliyopita. Ilikuwa saa 12:30 jana jioni nilikuja nyumbani nikamkuta dada yangu amejinyonga.”
Pia, kama mama anachukua wajibu wa watoto wake, basi watakosa baba halisi ambaye angewatunza. baba wa kambo mara nyingi ndiye sababu ya kukosekana furaha kwa watoto wake wa kambo.
Mwanamke alimsaidia mume wake wa ndoa ya pili kumfunga mtoto wa kambo mwenye umri wa miaka nane kwenye kitanda. Halafu wakafunga mlango na wakaondoka kwenda matembezini. Waliporudi nyumbani,walikuta mtoto wao ameungua moto hadi kufa kwa sababu ya moto uliounguza nyumba.
Talaka huharibu familia na huwaacha watoto wanatangatanga hawana hifadhi. Watoto mara nyingi huteseka kwa sababu ya ubinafsi wa wazazi wao.
Watoto wanne wenye umri wa miaka kumi na mbili, tisa, sita na minne walikwenda kwenye kituo cha polisi. Mtoto mwanamme mwenye umri mkubwa zaidi alisema: “Wazazi wetu walitengana muda fulani uliopita. Wakati wote walikuwa wanabishana na walikuwa na tabia ya kugombana kila siku mchana na usiku. Sasa wametalikina, hapana mmojawao ambaye yupo tayari kutulea sisi.”
Watoto ambao hawana mlezi anayefaa na mazingira ya familia, mara nyingi hukengeuka. Kutokupata elimu ya kutosha na mtu mwenye huruma katika maisha yao, huwafanya wasumbuliwe na hisia za udhalili. Wanaweza hata kufanya uhalifu wa viwango mbali mbali, wakati wa utoto au utu uzima.
Mtu anaweza kutambua jambo hili na kusoma matukio kwenye magazeti kila siku.
Kwenye utafiti uliofanywa kwenye kituo cha kurekebisha vijana, ni wazi kwamba katika vijana wahalifu mia moja kumi na sita wa kituo hiki, watu themanini walithibitisha kwamba mama zao wa kambo waliwanyanyasa ndio sababu wakafanya uhalifu.”
Mpendwa bibi na bwana! Kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, kwa ajili ya watoto wako wasio na kosa, kuweni wasamehevu nyinyi kwa nyinyi wanandoa. Msikuze matatizo madogo na msipende kung’ang’ania ubishi. Msitafutane makosa nyinyi kwa nyinyi. Fikirieni mambo yenu ya siku zijazo na watoto wenu.
Kumbukeni watoto wenu wanawategemeeni nyinyi na wanatumaini kupata furaha yao kutoka kwenu. Wahurumieni na msiharibu maisha yao.
Kama mkidharau matamanio yao ya ndani na kama mkivunja nyoyo zao ndogo, hamtaweza kuepuka athari ya masikitiko yao. Kwa hiyo, hamtaweza kuwa na maisha yenye faraja pamoja.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU