SWALA YA JAMAA

Allah amewaarimsha wanaume kuswali swala tano katika jamaa. Imethibiti kuwa malipo yake ni makubwa. Mtume,swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Swala ya jamaa ni bora zaidi kuliko swala ya mtu peke yake kwa daraja ishirini na saba». (Bukhari, Hadithi Na. 619- Muslim, Hadithi Na. 650).
Uchache wa idadi ya watu kuswali jamaa ni imamu na maamuma. Kila jamaa inapokuwa na watu  wengi sana basi inapendeza zaidi kwa Allah.
Maswahaba walikuwa na bidii ya kuswali swala ya Jamaa kiasi kwamba walikuwa wakizingatia kwamba kudumu kuacha swala ya Jamaa ni tabia miongoni mwa tabia za unafiki. 

Maana ya kumfuata imamu

Ni maamuma mwenye kuswali kuifungamanisha swala yake na imamu wake. Amfuate katika kurukuu kwake, kusujudu kwake na asikilize kisomo chake. Hatakiwi kumtangulia au kutofautiana naye katika jambo lolote katika hayo. Anatakiwa kufanya jambo mara tu  baada ya imamu wake kulifanya.
Mtume,swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakuna vingine isipokuwa kwamba amewekwa imamu ili afuatwe. Akitoa Takbira basi nanyi toeni Takbira, na wala msitoe Takbira mpaka yeye atoe Takbira. Na atakapo rukuu nanyi rukuuni, na wala msirukuu mpaka yeye arukuu. Na akisema: Samia-llahu liman-hamidah, basi semeni Rabbanaa Walakal-hamdu. Na akisujudu basi sujuduni, na wala msisujudu mpaka yeye asujudu…».    (Bukhari, Hadithi Na. 701-  Muslim, Hadithi Na. 414-   Abuu daudi 603)

Nani anafaa kufanywa imamu?

Anatangulizwa kuwa imamu yule aliehifadhi zaidi Qur`ani, kisha anayefuatia, kisha anayefuatia, kama Mtume,swallalahu alayhi wasalam, alivyosema kuwa: «Awaongoze watu msomaji wao zaidi wa kitabu cha Allah. Ikiwa watakuwa sawa katika kusoma, aongoze mjuzi wao zaidi wa sunna..»  (Muslim, Hadithi Na. 673).

Imamu na maamuma wanasimamaje? 

Inatakiwa imamu awe mbele, na maamuma wajipange safu  nyuma yake, na wajaze safu moja baada ya nyingine.  Kama maamuma ni mmoja basi asimame upande wa kulia wa imamu.

Atakamilisha vipi kilicho mpita kwa imamu?

Yeyote atakaye unga swala kwa imamu huku akiwa amepitwa na kitu katika swala, basi atamfuata imamu mpaka atoe salamu, kisha akamilishe kilicho mpita katika swala yake.
Pale alipomkuta imamu huhesabiwa kuwa ndio mwanzo wa swala yake, na atakayo yafanya baada ya hapo huhesabiwa kuwa ndio mwisho wa swala yake.

Vipi rakaa huwahiwa?

Swala huhesabiwa kwa idadi ya rakaa, na mwenye kuwahi rukuu pamoja na imamu hakika ameiwahi rakaa ikiwa kamili. Mwenye kupitwa na rukuu basi ataungana na imamu, lakini yale matendo na maneno yaliyo baki ya rakaa hiyo  hayatahesabiwa katika rakaa zake (ameikosa rakaa).
Mifano ya maamuma ambaye amepitwa na kitu mwanzo wa Swala pamoja na imamu.
  • Mwenye kuwahi rakaa ya pili pamoja na imamu katika swala ya Alfajiri basi itamlazimu, baada ya salamu ya imamu, asimame na akamilishe rakaa iliyompita. Hatakiwi kutoa salamu mpaka aimalize rakaa hiyo, kwa sababu swala ya Alfajiri ina rakaa mbili, na yeye hakuwahi isipokuwa rakaa moja tu.
  • Mwenye kumuwahi imamu akiwa katika Tashahudi ya Mwisho katika swala ya Magharibi basi itamlazimu, baada ya salamu ya imamu, asali rakaa tatu zote, kwa sababu amemkuta imamu akiwa katika Tashahudi, na rakaa inawahiwa kwa kuwahi kurukuu pamoja na imamu.
  • akimkuta imamu akiwa katika rukuu ya rakaa ya tatu katika swala ya adhuhuri  atakuwa amewahi rakaa mbili pamoja na imamu ( hii ni Kutokana na maamuma kukosa rakaa mbili za mwanzo za swala ya adhuhuri) imamu atakapo toa salam itamlazimu(maamuma) kusimama na kukamilisha kilicho bakia, nazo ni rakaa mbili ya tatu na ya nne kwani adhuhuri ina rakaa nne.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU