Samehe Makosa Ya Mke Wako ata kama kafanya hili
mwanadamu aliyekamilika na sote sisi hufanya makosa mengi. Kama mambo yalivyo, hii ni kweli kwa wanamume na wanawake.
Kwa upande wa wanawake, anaweza kufanya makosa kwa kutokuwa na adabu kwa mume wake, kufanya kitu kinyume na matakwa yake kuwa mkali kwake, au kumwingiza kwenye hasara kiuchumi kwa sababu ya kuwa mzembe na kadhalika.
Kama mambo yalivyo, ni kweli kwamba wanandoa lazima waridhishane na waepuke kabisa kuudhiana wao kwa wao: Hata hivyo, hutokea mara chache kwamba mmoja wapo au wote watashindwa kukwepa kipengele hiki.
Baadhi ya wanaume hudhani kwamba wanatakiwa kuwa wakali kwa makosa ya wake zao kwa kuwa wanaamini hii kuwa ndio njia ya kuzuia kurudia kosa la aina hiyo.
Hata hivyo, uzoefu mara nyingi unaonesha matokeo kuwa kinyume chake kabisa. Mwanamke, ambaye mume wake ni mkali kwake, anaweza kuvumilia ukali wake kwa kipindi fulani, lakini hatimaye anaweza kuamua kujibu dhidi yake ikiwa kama matokeo ya kukatisha tamaa. Mke atazoea msimamo wake polepole hadi hapo atakapokuwa sugu.
Mume ambaye hatakuwa msamehevu kuhusu makosa ya mke wake, ni kwamba anamhamasisha mke wake kuwa jeuri na kukosa nidhamu. Anaweza kutaka kuendelea na msimamo huu ambapo kwa hakika atakabiliana na ugomvi mwingi wa mke wake. Wote wataishi katika hali ya uchungu kwa maisha yao yote.
Au anaweza akamwacha mke alivyo na asijihusishe naye kwa ukamilifu. Katika mfano huu mke wake, ambaye atahisi ameshinda, atakuwa hajali ridhaa na matakwa ya mume wake. Hali hii inaweza kufika kiasi kwamba hata hapo mke anapofanya makosa makubwa ya kudhamiria, atanyamaza. Hapo tena ndoa yao itakuwa imepoteza uchangamfu na wanaweza kukimbilia kutalikiana.
Kumbuka kwamba talaka husababisha madhara pande zote mbili kwa sababu kuanza maisha mapya si rahisi. Itakuwa hakuna uhakika wa kuwepo furaha baada ya kutalikiana.
Kwa hiyo, ukali haufai kutumika kila wakati na mara nyingi husababisha matukio yasiopendeza ambayo mtu anaweza kuyasoma kwenye magazeti. Njia nzuri kuliko zote ni kuwa mwenye kiasi na kutenda kimantiki. Samehe makosa yote madogo na yasio ya kukusudia yanayofanywa na mke wao. Hakuna haja ya kupiga kelele kwa ajili ya kosa la mke wako ambalo limefanyika bila kukusudia.
Kama mambo yalivyo, mara kwa mara mtu anaweza kuwashauri wenzake ili kuwasaidia wasirudie tena kosa la aina hiyo.
Watu hufanya makosa mengi kwa kutokujua, kwa hiyo ni vizuri zaidi kuwa shauri kwa uvumilivu kusahihisha matendo au maoni yao yaliyopotovu.
Kwa hiyo, mke wako hawezi kulazimishwa kurekebisha makosa yake; lakini badala yake unatakiwa kumpa maelezo kuhusu kosa, ili aweze kufanya uchaguzi, yeye mwenyewe asirudie tena kosa hilo.
Hivyo, si tu kwamba uelewano na kuheshimiana unabakia kama zamani, lakini pia kosa hilo litazuiwa na halitafanywa tena.
Ni busara kwa mwanamume kumzuia kimantiki mke wake asifanye makosa, lakini kama ataendelea kufanya makosa, basi kwa mara nyingine amsamehe na asijali makosa yake. Si rahisi kwa mume kuendelea kumpa adhabu mke wake au kujaribu kuonesha hatia yake ili amweke katika hali ya kuomba msamaha. Hii ni kwa sababu wanawake ni wajeuri kwa kawaida; na ukali usio stahili huwafanya watoe majibu zaidi kuliko ya hapo mwanzo. Hii inaweza kufatiwa na matukio yasiyopendeza na ya kuhofisha, kama vile kuachana au mauaji.
Uislamu umelielewa jambo hili nyeti, ambapo wanamume wamepewa wajibu kwa wanawake zao.
Imamu Ali (a.s) alisema: “Wavumilieni wanawake katika hali zote na semeni nao vizuri; na kwa kufanya hivyo wanaweza kurekebisha matendo yao”
Imamu Sajjad (a.s) alisema: “Ni haki ya mke wako kwamba unamtendea wema, kwa sababu yupo chini ya dhamana yako na unatakiwa kumlisha na kuvesha na unasamehe makosa yake ya kijinga.”
Imamu Sadiq (a.s) aliulizwa: “Mwanamke anazo haki gani kwa mume wake, ambazo kama akizitimiza ipasavyo, ataonekana kuwa mtu mwenye matendo mema?” Imamu alijibu: “Lazima ampe chakula na nguo na amsamehe makosa yake aliyoyafanya bila kukusudia.”
Imamu Sadiq (a.s) pia alisema; “Yeyote anaye waadhibu wale walioko chini yake, asitarajie kuheshimiwa au kupata cheo cha juu.”
Mojawapo ya sababu za ugomvi miongoni mwa wanamume na wanawake ni kwamba mama wakwe huingilia mambo ya familia zao.
Mama kabla ya kumuoza binti yake kwa mume, hudhani ya kwamba mkwilima wake kuwa mkamilifu na humthibitisha kwa binti yake kwamba ndiye atakaye mfanya awe na furaha. Atamheshimu na kumfanyia wema kwa matumaini ya kuwa na uwezo wa kurekebisha dosari zake ndogo ndogo baadaye.
Wakati mwingine mama mkwe humuona mkwilima wake hufuata matarajio yake na wakati mwingine hafuati. Katika mfano wa mwisho, anayo nia ya kumtengeneza mkwilima wake hadi hapo atakapo kubalika naye na katika utekelezaji wa hili hutumia kila njia zinazo wezekana kama vile za kwake mwenyewe na za uzoefu wa wengine na huanza kupanga namna ya kuwendea.
Wakati mwingine mama mkwe hujifanya mwenye huruma na wakati mwingine mkali. Anaweza akafanya mambo kama vile yeye ni mlezi na mfawidhi au anaweza akalalamika. Hata hivyo, chaguo zuri zaidi ni lile la kufanikisha lengo lake kwa kumvuta binti yake kwa kumfanya asifuate matakwa ya mume wake.
Huanza kumtumia binti yake na kwa hiyo humuamuru afanye tofauti nyakati mbali mbali. Kwa hiyo mwanaume humuona mke wake humlaumu leo na kesho kumuomba afanye kitu fulani.
Mwanamke mwenye uzoefu atafikiria kwamba mama angekuwa na huruma kuhusu ndoa yake na angefuata ushauri wake.
Hivyo kama mume wake hatafuata matakwa ya mama mkwe wake, ugomvi utaanza baina ya wanandoa na matokeo yake yanaweza kuwa kutalikiana au hata mauaji.
Hii ndio sababu wanamume wengi hawaelewani na mama wakwe zao. Huwalaumu kwa utovu wa adabu wa wake zao na huamini kwamba mama wakwe zao huwafundisha mabinti zao tabia mbaya.
Haitakuwa wazo mbaya kama mtu anajifunza kuhusu malalamiko ya wakwilima wachache.
Bwana M. Javda ameandika: “Mama mkwe wangu ni pepo mbaya, zimwi na joka la vichwa viwili. Mungu na amwepushe asiliwe na mbwa mwitu. Ameyafanya maisha yangu kuwa machungu sana hivyo kwamba ninapata wendawazimu na ninahisi kama vile nikimbie niende milimani na majangwani. Si mimi tu, ambaye nimechoshwa na hali hii. Huu ni mfano wa kawaida na ninadhani asilimia tisini na tano ya wanamume wana athiriwa na hawa mama wakwe na asilimia tano nyingine labda hawana mama wakwe.” Bwana F. Mohammed ameandika: “Mama mkwe wangu kila mara huingilia maisha yangu. Husababisha maudhi bila ya sababu ya maana. kila wakati husema maneno ya kashfa kuhusu familia yangu.
Wakati wowote ninaponunua kitu chochote kwa ajili ya mke wangu, mama mkwe wangu, huanza kuonesha dosari kuhusu kitu hicho. Hukosoa rangi yake au mtindo na hujaribu kuthibitisha kwamba kitu hakina thamani kwa mke wangu.” Bwana K. Parvis amendika: Mama mkwe wangu amenitendea kwa njia ambayo kwamba nimebakia kidogo nimtaliki mke wangu mara tatu. Huuma kama nge. Humfundisha mke wangu kuwa jeuri kwangu, kuacha kazi za nyumbani au kutarajia kisichowezekana kutoka kwangu. Wakati wowote anapokuja kututembelea, nyumba yetu hugeuka kuwa jahanamu. Kwa kweli sipendi hata kumuona.”
Wanaume wengi hujaribu kukabiliana na mvuto wa wakwe zao kwa wake zao kwa kuwekea mipaka uhusiano wao. Huwakataza wake zao wasiende kwa wazazi wao. Kwa ufupi, wanaume hawaelewani kabisa na mama wakwe zao na huonesha kutokupenda kwao kwa kila namna iwezekanayo.
Hata hivyo, mtazamo huu licha ya kwamba ni wa kawaida, si wenye mantiki na busara. Hii ni kwa sababu uhusiano wa mama na binti yake una nguvu sana na wa kimaumbile ambao hauwezi kuvunjwa kwa urahisi.
Inawezekanaje mwanaume kutarajia mke wake, kuwaacha wazazi wake ambao walitumia miaka mingi kumlea?
Matumanini haya hayatekelezeki na hata kama inatokea itakuwa kwa muda mfupi tu, kama ilivyo kwamba tendo lolote lisilo la kawaida halidumu muda wote.
Zaidi ya hayo kama mwanamke anahisi kwamba mume wake hawapendi wazazi wake, anaweza kuchukua msimamo kama huo kuhusu familia ya mume wake. Anaweza akawa hamtii, hamheshimu na kadhalika.
Juu ya hayo, msimamo huu wa mwanaume hutoa mwanya wa kisingizio kwa mama mkwe wake huingilia ndoa yake kwa ukali zaidi. Kwa ufupi, msimamo huu unaweza kusababisha matokeo mabaya na huenda yakawaelekeza wanandoa kutalikiana.
Kwa vyovyote vile kwa nini mwanaume ambaye anaweza kufaidika kutokana na kuelewana na wazazi wa mke wake, akimbilie hatua ya aina hiyo ambayo inaweza kumdhuru yeye na familia yake?
Mamlaka ya polisi wa India yalitoa taarifa kwamba mnamo mwaka 1971, sababu kubwa ya idadi ya matukio 146 ya watu kujiua wenyewe katika jiji la New Delhi ilikuwa uhusiano mbaya baina ya waume na mama wakwe zao.”
Mwanaume ambaye alikatishwa tamaa na mama mkwe wake kwa sababu ya kujiingiza kwake, alimtupa nje ya teksi.”
Mwanaume alivunja fuu la mama mkwe wake kwa nyundo. halafu kaka wa huyo mtu akakasirika na baada ya kumjeruhi kwa kisu akatoroka na kupotea.”
“Bwana…ambaye alikasirishwa na mama mkwe wake, alimwagia supu ya moto kichwani. Mama mkwe alipiga kelele na kupoteza fahamu. Alipelekwa hospitalini baada ya kupona akasema kwamba binti yake amemwambia mume wake kwamba anataka talaka na hakutaka kuishi naye zaidi ya hapo.”
Mwanaume ambaye alichoshwa na mama mkwe wake, alijiua mwenyewe.
Labda inafaa kutaja mambo mawili hapa: Ni dhahiri kwamba mama mkwe si tu ni adui kwa mkwilima wake, lakini ni kawaida yeye kumpenda mkwilima wake kama ilivyo jionesha mwanzoni mwa ndoa. Zaidi yake ni kwamba mama mkwe anajikuta yupo karibu na mkwilima wake kwa sababu ya kutaka kuona binti yake anafurahi. Kwa hiyo, mama mkwe anapoingilia maisha ya ndoa ya binti yake, haiwezekani kumaanisha kuwa kitu chochote isipokuwa kiwe na nia njema. Anamaanisha kuwa na huruma lakini wakati mwingine kwa sababu ya ujinga, huchukua hatua zisizo sahihi au hutoa ushawishi wenye madhara. Kwa hiyo, mtu asiwakosoe sana wake wa aina hii.
Uhusiano wa mama na mtoto ni wa asili ya maumbile ambao hauwezi kuvunjwa kwa urahisi, na yeyote anayefanya bidii ili kufanikisha hilo, kwa hakika atashindwa. Juhudi za aina hiyo ni kinyume cha kanuni za maumbile na haziwezi kuhalalishwa kwa vyovyote vile.
Kama vile mtu mwanaume anavyo wapenda wazazi wake, ndivyo ilivyo kwa mwanamke. Kwa hiyo, ni vizuri zaidi kuwa na uhusiano na wazazi wa wanandoa ambao unanufaisha pande zote mbili. Hii inawezekana tu kama mtu anaonesha heshima na wema. Mwanaume anaweza kwa kutumia busara, heshima, utiifu na kadhalika kuwa na uhusiano mzuri na wazazi wa mke wake. Lazima aoneshe mapenzi yake kwa mtoto wao. Asimlaumu mke wake mbele ya wazazi wake. Aombe ushauri na msaada wa kiroho kutoka kwao. Inapotokea wanatoa ushauri au kukosea kitu fulani, mkwilima anatakiwa kuonesha hilo kwa upole na kimantiki kwamba hapo wamekosea. Asiseme nao kwa ukali.
Mwanaume aliyeoa anatakiwa kuona uhusiano mzuri baina yake na wazazi wa mke wake kama wajibu wake na siri ya mafanikio ya ndoa yao. Matokeo yake ni kwamba matatizo mengi ya kifamilia yanazuiwa yasitokee na mengine mengi zaidi hupatiwa ufumbuzi. Kwa ufupi, si kila mara mama mkwe ndiye anayekuwa na hatia lakini wanamume wanatakiwa kuwa na busara ya kutosha na kuwa fanya kuwa na marafiki.
Wapo wanaume wengi ambao hufurahia uhusiano mzuri na mama wakwe zao.
Bwana Munuchehr ameandika: “mama mkwe wangu ni malaika au hata huzidi. Ninampenda zaidi ya ninavyompenda mama yangu mzazi, kwa sababu ni mwema na muelewa. Kila mara hutusaidia kutatua matatizo yetu. Kuwepo kwake ni dhamana na furaha ya familia yangu na ustawi wetu.”
Hata kama mtu anaye mama mkwe ambaye ni jeuri, mjinga na haiwezekani kuelewana naye, asimfanyie ukali. Wanawake wa aina hii wanaweza kufanya maisha ya mtu kuwa magumu, lakini ni vizuri kila mara kutoa majibu kwa upole dhidi ya tabia yao isiyofaa. Hii ni kwa sababu, kwa kuwa mwema kwao, mtu anaweza akapunguza hatari inayoweza kutokea kwenye ndoa yake.
Wakati huo huo, mwanaume anatakiwa kuwa karibu na mke wake na amfanye mke amwamini yeye. Lazima azungumze naye kuhusu matendo mabaya ya mama yake na kuthibitisha kimantiki kwake matokeo yasiyopendeza yanayoweza kusababishwa na tabia ya mama mkwe wake.
Ikiwa mtu anaweza kutengeneza maelewano ya kina na mke wake, basi matatizo mengi ikiwa ni pamoja na lile la mama mkwe wake litatatuliwa.
Kwa hiyo usidharau tabia njema, uwe na busara na uifanyie wema familia ya mke wako ili mpate kufuzu katika ndoa yenu.
Imamu Ali (a.s) alisema; “Kukuza urafiki ni nusu ya busara.”
Imamu Ali (a.s) pia alisema; Kujumuika na watu na kuwafanyia tabia njema humzuia mtu asifanye matendo mabaya na fitina.”
Imamu Ali (a.s) alisema; Jumuikeni na mfanye wema. Jiepusheni na kununa na kufarakana.”
Uwe Msikivu
Mwanamke ni kiumbe mwenye hisia kubwa ambazo hutawala mantiki yake. Mwanamke ni mjinga na mwepesi kuhisi kuliko mwanamume. Mwanamke anaweza kudanganywa kwa urahisi zaidi na hawezi kudhibiti matashi ya hisia zake. Hawezi kuamua kwa busara pindi anapotibuliwa. Anaweza kufurahishwa au kutibuliwa kwa urahisi sana.
Hivyo kama mwanaume ana usimamizi wa tabia na matendo ya mke wake, hatari za watu wengi zingeepukwa.
Ndio sababu dini tukufu ya Uislamu imemteua mwanamume kuwa kama mlezi wa familia yao na hufanya kuwa na wajibu kwa mambo ya familia.
Mwenyezi Mungu anasema kwenye Qurani Tukufu:
الرِّجَالُ قَوَّامُونَ عَلَى النِّسَاءِ بِمَا فَضَّلَ اللَّهُ بَعْضَهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ وَبِمَا أَنْفَقُوا مِنْ أَمْوَالِهِمْ ۚ فَالصَّالِحَاتُ قَانِتَاتٌ حَافِظَاتٌ لِلْغَيْبِ بِمَا حَفِظَ اللَّهُ ۚ
{34}
“Wanamume ni wasimamizi wa wanawake kwa kufadhiliwa na Mwenyezi Mungu baadhi yao juu ya baadhi, na kwa mali yao wanayo yatoa. Basi wanawake wema ni wale wenye kutii na wanao jitihada hata katika siri kwa kuwa Mwenyezi Mungu ameamrisha wajilinde.”
(Quran 4:34).
Kwa hiyo mwanaume anayeonekana kama mlinzi wa familia yake, asifanye uzembe kuhusu matendo ya mke wake. Kila mara lazima afawidhi mambo ya mke wake na kufuatilia matendo yake. Lazima mume ahakikishe kwamba mke wake hapotoki au kujumuika na aina ya watu wabaya.
(Quran 4:34).
Kwa hiyo mwanaume anayeonekana kama mlinzi wa familia yake, asifanye uzembe kuhusu matendo ya mke wake. Kila mara lazima afawidhi mambo ya mke wake na kufuatilia matendo yake. Lazima mume ahakikishe kwamba mke wake hapotoki au kujumuika na aina ya watu wabaya.
Mume lazima amweleze mke wake kimantiki kuhusu madhara ya rafiki mbaya. Asimruhusu kuondoka nyumbani akiwa amevaa nguo zisizofaa au zile zinazosababisha ashiki ya kijinsia. Asimruhusu mke wake ashiriki kwenye shughuli ovu au kuhudhuria mikutano isiyofaa.
Ni kweli kwamba kama mwanamke akiachwa peke yake katika matendo yake na kuchanganyikana na watu, inawezekana akanasa kwenye mtego wa watu wenye akili potovu na huishia kwenye upotovu.
Wanaume wanashauriwa kuangalia idadi ya wanawake ambao kwa sababu ya uzembe wa waume wao wamenasa kwenye mtego wa uovu. Wapo wanawake wengi ambao wamedanganywa kwenye karamu za usiku. Familia nyingi zimevunjika na watoto wengi wamepoteza familia zao. Kwa sababu ya mikusanyiko hiyo.
Mwanaume anaye mruhusu mke wake kuondoka nyumbani akiwa amevaa nguo zisizofaa, kuwa na marafiki wabaya na hamzuii kuhudhuria mikusanyiko yenye uharibifu, kwa kweli atakuwa anafanya kosa kubwa sana la uhaini kwake, kwa mke wake na kwa watoto wake.
Msimamo huu ungemwelekeza mke wake kwenye mamia ya sehemu za hatari ambamo hawezi kujinasua kwa urahisi. Petroli hushika moto kwa urahisi sana, kwa hiyo ni tendo la kipumbavu kuacha petroli karibu na moto na kudhani kwamba haitashika moto.
Ujinga ulioje wa watu ambao huwaruhusu wake zao au mabinti zao kujionesha mitaani huku wakiwa wanavaa nguo zisizofaa na wakati huo huo hawapendi nadhari au kutupiwa macho na wanaume kwa sababu ya mavazi yao!
Uhuru usio sahihi wa aina hii unayo matokeo mabaya sana. Kama mwanamke amefaulu kumshinda mume wake kuhusu matamanio yake yasiyo halali, ataongeza matakwa hayo hadi kwenye kiwango ambacho atafanya mambo yake kwa uhuru bila kumjali mume wake. Hii itasababisha matukio ya uovu kwenye familia.
Ndio maana Mtume (s.a.w.w) alisema: “Mwanaume ni mlezi wa familia yake na mlezi yeyote anao wajibu kwa wale walio chini kuwatimizia mahitaji yao.”
Mtume (s.a.w.w) pia alisema: “Waamrisheni wanawake kufanya mema kabla hawajakufanyieni ninyi uovu.”
Kwa nyongeza Mtume alisema: “yeyote anaye mtii mke wake, Mwenyezi Mungu atamtupa kwenye moto akitanguliza uso wake.”
Mtume aliulizwa: “Aina gani ya utiifu unaomaanishwa hapa?” Mtume
(s.a.w.w) alijibu: “Ni hapo ambapo mume humruhusu mwanamke ambaye humwomba mume wake ruhusa ya kwenda kwenye hamamu ya nje, watu kuhudhuria harusi, sherehe na mikusanyiko ya kutoa rambi rambi akiwa amevaa nguo za kumfedhehesha.”
Imamu Sadiq (a.s) alisema: “Furaha kamili ya mwanaume ni kwamba awe mfawidhi na kiongozi wa familia yake.”
Mtume (s.a.w.w) wa Uislamu alisema: “Mtu yeyote anayemruhusu mke wake ambaye amejipamba, kuondoka nyumbani kwake ni mtu mwenye roho ya kikatili na yeyote atakaye mwita hivyo, atakuwa hakufanya dhambi.
Na mwanamke yeyote ambaye mume wake humruhusu kutoka nyumbani kwake akiwa amejipamba na kujipulizia manukato, kila hatua atakayo tembea, Mwenyezi Mungu atamjengea nyumba mume wake huyo katika Jahannamu.”
mwisho ninawakumbusha kuhusu mambo mawili: Ni sahihi kwamba mwanaume anatakiwa kuwa na hadhari kwa mke wake lakini zoezi hili linatakiwa kufanywa kwa uangalifu na busara. Mume hatakiwi kukimbilia kukasirika au matumizi ya nguvu. Asimwoneshe mke wake kwamba anaamuriwa au vinginevyo atatoa jibu kwa njia isiyopendeza. Njia iliyo nzuri kabisa, kwa mwanaume ni kuwa na huruma na uelewa. Lazima atekeleze zoezi hili kama mwenza mwenye upole na amwambie mke wake kuhusu madhara ya matendo maovu. Lazima atengenezewe mazingira ya kuchagua njia iliyo nyooka yeye mwenyewe kwa shauku na hamu.
Mwanaume anatakiwa kuwa na wastani, ni kwamba wala asiwe mkali sana na kiherehere ama asiwe mzembe.
Mwanamke, kama alivyo mwanaume, anahitaji uhuru na anatakiwa apewe uwezo wa kujiamulia la kufanya kwenye makundi yake kwa usawa unatakiwa.
Lazima mwanamke awe huru awe huru kuwasiliana na wazazi wake, kaka zake na dada zake, na lazima aruhusiwe kuwa na watu wa aina inayofaa.
Kwa ufupi, ipo mifano isiyo ya kawaida ambapo mwanamke ananyang’anywa utashi wake. Lakini hata kwenye mifano kama hiyo mtu hatakiwi kuvuka mpaka uliowekwa na kuwa mkali sana. Ukali wa kupita kiasi unayo madhara. Huharibu mazingira ya urafiki na husababisha maudhi. Mwanamke anaweza akajibu kwa ukali zaidi kutokana na ukali wa mume wake. Mke anaweza hata kuomba talaka.
Mwanamke kijana, mke wa… alimwambia mwandishi wa habari mahakamani: “Niliolewa na Bwana….Miaka mitano iliyopita. Tunao watoto wawili; mmoja wa kiume na mwingine wa kike. Wakati fulani mume wangu amekuwa anamchukulia kila mtu kwa namna ya ubeuzi. Haniruhusu mimi kushirikiana na mtu yeyote. Hata hufunga milango ya nyumba anapoondoka nyumbani. Sisi ni wafungwa ndani ya nyumba yake. Sasa, siwezi hata kwenda kwa wazazi wangu.
Watu wa familia yangu hawatutembelei, kwa sababu yake. Sijui nifanye nini! Kwa upande mmoja ni kwamba siwezi kuishi naye, na kwa upande mwingine, nina wasi wasi kuhusu hatima ya watoto. Kwa hiyo, niliamua kuleta shauri langu kwenye mahakama hii; labda wanaweza wakapitisha uamuzi fulani.”
Wanaume kama mume wa huyu mwanamke, kwa bahati mbaya ni wakali sana na si watu wa kawaida hivyo kwamba wake zao, licha ya kutaka kuishi pamoja na waume zao, huomba talaka. Wake zao huudhika sana, licha ya kuwa na watoto, wapo tayari kutengana nao.
Kwa nini mwanaume amkatae mke wake asishirikiane na ndugu zake wa karibu? Kwani haelewi kwamba ukali ukizidi kiasi, hutayarisha uwanja kwa baadhi ya wanawake kukengeuka? Kwani hajasikia au hajaona familia zilizosambaratika kutokana na tabia ya aina hii?
Hata kama mke wa mtu atavumilia ukali wa mtu, patakuwepo upungufu wa huba inayo changamsha mazingira ya familia ndani ya nyumba. Inawezekanaje mtu kutarajia mke aliyeko kifungoni kuwa mwema kwa mume wake na watoto au kufuatilia kazi za nyumbani kwa hamu?
Comments
Post a Comment