RC Makonda awapa siku tano wakandarasi Watakaokaidi Kukiona
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda, amewapa siku tano kuanzia jana Wakandarasi ambao miradi yao imekuwa ikisuasua kuhakikisha wanaanza kazi mara moja na kubainisha kuwa wakandarasi watakaokaidi agizo hilo Watakamatwa na Vyombo vya dola na mikataba yao kuvunjwa.
Miongoni mwa Miradi ambayo RC Makonda amesema imekuwa ikisuasua ni Ujenzi wa Mto Ng'ombe, Mfereji wa Buguruni Kisiwani, Tabata Roman Catholic, Barabara ya Kivule na Barabara ya Kawe.
Aidha RC Makonda amezionya Bodi za Manunuzi zitakazobainika kutoa tenda kwa wakandarasi kwa rushwa bila kuangalia uwezo wa Kampuni kuwa watachukuliwa hatua.

Comments
Post a Comment