Prof. Kabudi ataja changamoto zinazoikabili Dunia


Mabadiliko ya tabia nchi sambamba na matukio ya hali ya kiusalama ikiwemo masuala ya ugaidi na vita ni kati ya changamoto mbalimbali ambazo zimekua zikiikumba Dunia katika utekelezaji wa malengo endelevu.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof.Paramagamba Kabudi ameyasema hayo jana, Jijini Dodoma wakati wa maadhimisho ya miaka 74 ya Umoja wa Mataifa (UN) yaliyofanyika katika eneo la Nyerere Square.

Amesema baadhi ya Mataifa yamekuwa na matukio mbalimbali kama vile ugaidi, vita pamoja na migogoro mbalimbali ambayo inatakiwa kutatuliwa ili kuweza kurejesha amani kwa baadhi ya mataifa ambayo yamekuwa yakikumbwa na migogoro ya mara kwa mara.


“Tunapoadhimisha mikaa 74 ya Umoja wa Mataifa Dunia inakabiliwa na changamoto mbaimbali za matukio ya kiusalama kama vile ugaidi, vita, migororo mbalimbali pamoja na mabadiliko tabia nchi, na hii inarudisha nyuma utelekezaji wa maendeleo,” amesema Prof. Kabudi.

Amesema katika kukabiliana na changamoto hizo Tanzania inaupongeza Umoja wa Mataifa kwa kuwa mstari wa mbele kuzitafutia ufumbuzi changamoto hizo ili kuifanya Dunia kuwa sehemu salama na bora ya kuishi kwa wananchi na vizazi vijavyo.

Jumatano Oktoba 23, 2019 Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Mnyepe alisema maadhimisho ya miaka 74 ya Umoja wa Mataifa (UN), yafanyika hii leo huku Serikali ikiwa imepiga hatua katika suala la usawa wa jinsia kwa kutoa kipaumbele cha nafasi za uongozi kwa wanawake.


“Maadhimisho haya yana kauli mbiu isemayo Wanawake na Wasichana kuwa kipaumbele kufikia malengo ya Dunia ambapo tayari tumepiga hatua katika usawa wa kijinsia na maadhimisho haya Kitaifa yatafanyika hapa Jijini Dodoma,” alifafanua Dkt. Mnyepe.

Aidha Dkt. Mnyepe alisema wanawashukuru Umoja wa Mataifa (UN) kwa ushirikiano waliowapatia hasa katika kutoa elimu juu ya nafasi ya mwanamke katika uongozi na kuwashukuru wananachi kwa kujitokeza katika viwanja vya Nyerere Square kushuhudia maadhimisho hayo yanayofanyika kwa mara ya kwanza Dodoma.

“Kama Taifa tumekua mstari wa mbele kupigania haki ya mtoto wa kike na wanawake kwa ujumla hivyo tunaamini katika usawa na nitoe rai kwa watanzania kuendelea kuwaamini wanawake katika mambo mbalimbali kielimu, kisiasa, kitamaduni na kiuchumi,” aliongeza Dkt. Mnyepe.


Akizungumza kwa niaba ya Mratibu wa Umoja wa Mataifa nchini Balozi Michael Dunford amesema sherehe hizo zimelenga kuhimiza usawa wa kijinsia huku akiipongeza Tanzania kwa kupiga hatua katika utekelezaji wa lengo namba 5 la malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) ambalo linazunguzia usawa wa kijinsia.

Amesema wanaamini kama nchi itafanikiwa katika lengo la usawa wa kijinsia maendeleo endelevu yatapiga hatua kutokana na upande wa Tanzania kufanikiwa katika sekta mbalimbali zikiwemo za elimu na afya na kwamba UN Itashirikiana na serikali katika kufanikisha malengo kusudiwa.

Umoja wa Mataifa umekua ukifanya maadhimisho haya kila ifikapo Oktoba 24 kila mwaka ambapo limefanyika gwaride maalumu la Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na bendera ya UN kupandishwa kwa mara ya kwanza Dodoma ikiwa ni Makao Makuu ya Nchi.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU