Nini maana ya Allah kuwa huru na mbali kutokana na wakati na sehemu? Je, unaweza kuelezea kupitia mifano?

Dhati ya Allah na sifa zake ni za tangu… dhati na sifa zetu ziliumbwa baadaye… bila ya shaka, hatuwezi kujua dhati yake au sifa zake vya kutosha; hatuwezi kufahamu kuwa kwake wa tangu na kuwa kwake huru kutokana na wakati… Vipi tutaweza kufahamu hayo? Hatuwezi hata kufahamu wakati ni kitu gani!..
Wakati ni nini? Ni kitu cha aina gani? Kitu chenye kutembea katika mto mmoja katika wakati mmoja, lakini kwa nini unaathiri vitu kwa tofauti? Huwafanya watoto wawe viana, watu wa makamo kuwa vizee na vizee kuelekea katika umauti. Je, mto huu unatembea kuelekea chini au juu?
Shairi lina uliza kwa uadilifu:
Wakati ni nini, ni nini?
Ni maji au ndege?
Wakati ni nini, ni nini?
Chini ya mlima au juu ya mlima?
Tumewekewa mpaka na wakati. Tuna jana na kesho. Ni awamu za muda wote wa maisha. Hata hivyo, awamu zote hizo ni zenye mahusiano; zimepewa majina kwa uhusiano. Leo iliitwa jana masaa ishirini au thelathini yaliyopita. Asubuhi, tutaiita jana. Muda uliyopita na ujao hauna tofauti na jana na leo. Kila siku, kila saa, hata kila wakati ni dunia yenye kujitegemea… Yote yanayojiri katika ulimwengu katika wakati fulani huleta michoro tofauti ukilinganisha na wakati mmoja kabla yake na wakati mmoja baada yake. Hivyo, mchoro tofauti unadhihirishwa katika dunia hii kila wakati.
Wakati unasomwa kupitia michoro hiyo iliyopangiliwa katika mistari, au michoro hiyo imezamishwa ndani ya wakati. Maneno mengi yamesemwa kuhusu wakati. Bila ya kujali asili yake halisi ni kitu gani, wakati, ambapo ni dhana inayohusiana na vitendo, harakati, kutulia na kuondoka kwa viumbe, hauwezi kuwa tendaji kwa Mola na Muumba wa limwengu zote. Anajua kila kitu ambacho kiliumbwa na kitakachoumbwa kupitia elimu yake ya azali.
Aya ifuatayo inaeleza vizuri sana:
Asijue aliye umba, naye ndiye Mjua siri, Mwenye khabari? (al-Mulk, 14 )
Mtu anayetazama kitabu lazima afikiri kwamba kila neno, mstari, na herufi ndani ya kitabu hiki imeandikwa. Hivyo, yule aliyeandika hayo lazima atakuwa tofauti na maandiko na kuwa huru na kufanana na herufi na maneno!..
Ulimwengu, wanadamu wote, wanyama, mimea wanatiririka katika mto wa wakati kwa kuendelea… wanaelekea upande wa umauti na akhera. Anayefanya mto huo utiririke bila ya shaka yupo huru na wakati. Hiyo ni kusema, hajafungwa au kudhibitiwa na wakati. Na hakuna kati ya hao wanaotiririka katika mto huo awezaye kufahamu kuwa huru kutokana na wakati vya kutosha.
Allah yupo huru na mbali kutokana na sehemu, pia. Tunaweza kutoa mwanga wa jua kama mfano: Upo katika vitu vyote vyenye kung’ara ulimwenguni kupitia rangi zake saba; Lipo na linaonekana katika kila kitu kwenye mfumo wa mwanga, joto na rangi saba, ambazo ni kama sifa zake; hata hivyo, halipo lenyewe dhati yake katika kila kitu linachokimulika na kukiangazia. Hiyo ni, jua lipo katika vitu vyote vyenye kung’ara ulimwenguni kupitia sifa zake lakini halipo katika kitu chochote kiupande wa ukubwa na umbo lake.
Sifa na asili ya Allah ambaye analipa jua sifa hizi, ni kamilifu sana kufahamika na akili zetu. Allah amekizunguka kila kitu kupitia sifa zake, hiyo ni kusema, kupitia nguvu zake, elimu na utashi. Hata hivyo, hayupo katika kitu chochote kwa dhati yake. Hiyo ni kusema, Yeye yupo kila mahali kwa sifa zake. Na hayupo sehemu yoyote kwa dhati yake. Kwakuwa Yeye ndiye aliyeumba sehemu; hahitajii sehemu.
Maswali juuyau islamu

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU