Ni zipi sababu (hekima) za tasattur (kujitanda ushungi, kujisitiri)? Kwanini tasattur ni lazima?

Dear Brother / Sister,
Kanuni kuwa jina hubadili
sha kitu kulingana na maana yake hudhihirika katika ukweli kuwa tasattur humbadilisha mwanamke inayembadilisha na kuwa kito cha thamani. Thamani ya kito hicho huzidi kadiri mwanamke anavyojihifadhi na kujificha.
Muunganiko uliowekwa na vitu hufanya vitu viwe na thamani au kukosa thamani kutegemeana na mahali vinakotumika. Jina tunalovipa vitu kuhusu sifa za vitu hivyo. Kila sifa ambayo kitu kinaipata huamua nafasi yake.
As-Sattar, ambalo ni mojawapo kati ya majina mazuri ya Allah Mtukufu, kilugha linamaanisha mwenye kuficha, anayesitiri na kuficha makosa na madhambi. Neno tasattur maana yake kujisitiri
Tasattur, ambalo limezingatiwa kama ni ishara ya kuheshimika mpaka sasa, halimaanishi hivyo kwa watu walioondokana na hali yao ya kimaumbile.
Kwa mujibu wa tunayoweza kuyaona pindi tunapochunguza historia ya jumuia mbalimbali ni ukweli kuwa kilicho cha kawaida, kilichoenea na muhimu ni tasattur. Katika mataifa mengine, tasattur huzingatiwa kuwa ni kiashirio kinachoamua kiwango cha heshima. Kwa upande mwingine, kukaa uchi kulizingatiwa kama alama ya fedheha na dharau na imeshutumiwa na takribani kila taifa katika historia yote.
Quran inatuambia “Hivyo (tasattur ) ni karibu zaidi kuweza kutambulikana wasiudhiwe." (al-Ahzab, 59)
Mola wetu Mlezi, aliyetuumba wanadamu na kufafanua neno mwanadamu, aliyetufahamisha maumbile yetu, aliyetuumba Waislamu na akafafanua neno Muislamu, aliyetufundisha maana ya Uislamu, aliyetuumba tukiwa utupu, aliyetutilia unyoofu na heshima, aliyetusitiri makosa yetu, anawataka wanawake waumini wajulikane na akafafanua kuwa wamesitirika.
Ili mtu ajulikane kuwa yuko katika tasattur haimaanishi kujulikana mbele za watu tu bali pia mbele ya viumbe wote; kutokuudhiwa hakumaanishi kuonewa na watu tu bali kutendewa vyema na viumbe wote.
Kuwa katika  tasattur kunalingana na mtu kujizingatia kuwa yupo katika ummah wa Muhammad (s.a.w).
Sababu nyingine ya tasattur ni kuwa mwanamke hujitazama kuwa amehifadhika na anawawezesha wengine kumbainisha kuwa ni mtu aliyehifadhika.

Nia hiyo hubainisha tabia  na sifa ya tabia hiyo. Kinachohitajika kuhifadhiwa hakiwezi kuwa ni ngao wakati huo huo. Mwanamke anahitajika kukubali kuhifadhiwa kama kito cha thamani kwa kuwa ni mwenye unyoofu na heshima; kwa hivyo, anahitajika azingatie unyoofu wake na heshima yake kama kito chake cha thamani.
Hali hiyo, ya kuafikiana na maumbile yake, ikifanikishwa, watu watakaomhifadhi mwanamke na watakaokuwa ngao yake watakuwepo kwa ajili yake. Atakuwa amehifadhiwa kama mwanamke wa kabila la Bani Qaynuqa ambaye alitukana na akahifadhiwa.
Mwanamke husifika vyema kama atakuwa amesitirika. Sifa hiyo inawahakikishia watu wajue maana ya kuwa mwanamke, na hifadhi ya hisia ya haya na unyoofu katika maumbile ya mwanamke hubainishwa na sifa hiyo: mwanamke ni yule aliyesitirika.
Maswali juuyau islamu

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU