Ni vipi vigezo vya ibada kukubaliwa na Allah?

Kuna sharti moja tu la ibada kukubaliwa na Allah. Ambalo ni Ikhlasi.
Uaminifu ni kama roho ya ibada inayofanywa. Ibada bila uaminifu/udhati ni sawa na kwamba haina roho. Haina thamani mbele ya Allah.
Uaminifu/Udhati kwenye ibada maana yake ni kuabudu kwasababu tu ni agizo kutoka kwa Allah na ndio njia ya kupata radhi za Allah. Mwanachuoni Badiuzzaman Said Nursi amelielezea jambo hili kama ifuatavyo:
Ibada na kumtumikia Allah hulenga (utekelezaji) wa agizo la kiungu, na radhi ya kiungu. Lengo la ibada ni kutekeleza agizo la kiungu, na tija yake ni radhi ya kiungu. Matunda na faida zake hulenga maisha ya akhera.
Ikiwa uaminifu utatumika kwa matakwa na faida ya kidunia, uaminifu utatoweka na hivyo ibada haitokuwa sahihi; maana yake ni kwamba, haitokubaliwa na Allah.
Katika hadithi, Mtume (rehma na Amani ziwe juu yake) ameelezea nafasi ya uaminifu katika matendo na ibada kama ifuatavyo:
“Bila shaka yoyote, Allah huyakubali baadhi ya matendo na ibada ambazo hufanywa kwa uaminifu kwa ajili yake na kutafuta radhi zake.”
Maswali juuyau islamu

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU

Kisa Cha Nabii Ibraahiym عليه السلام - Sehemu Ya 1