Ni nini maana ya Ibada? Kwanini tunaabudu?
Ibada maana yake ni kutekeleza maamrisho ya Allah, kujitenga na makatazo Yake, na kutenda kutokana na ridhaa Yake. Ama kuhusu kwanini tunaabudu:
* Awali ya yote, tunaabudu kwasababu ndio lengo la kuumbwa kwetu kwasababu Allah alituumba, sisi wanadamu, ili tumjue, tumuamini na kumuabudu Yeye.
Jambo hili linaelezwa kama ifuatavyo katika Qur’an:
“Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.” (adh-Dhariyat, 56)
Kama waumini, tunatenda kwa mujibu wa lengo la kuumbwa kwetu lililotajwa katika aya na kujaribu kukalimisha wajibu wetu wa kumuabudu Muumba wetu.
* Vile vile, tunamuambudu Allah kama sehemu ya kupeleka shukurani zetu Kwake kwa neema nyingi anazotupa.
Tunamshukuru mtu ambae hutupa zawadi ndogo kabisa mara kadhaa; ikiwa hatutomshukuru Allah ambae anatupa neema nyingi na zawadi nyingi, kupitia kumuabudu, tutakuwa ni watovu wa shukurani. Tunajaribu kukamilisha majukumu yetu ya kuabudu kwa usahihi kabisa kuepuka utovu wa shukurani.
Allah ametuumba kutokana na si kitu, akatupa hisia na viungo kwa maelfu, akaumba kila kitu ambacho hisia na viungo hivyo vinahitajia na ametupa ubinadamu, Imani na muongozo wa maisha.
Inaelezwa katika Qur’an kwamba neema za Allah hazina mwisho na haiwezekani katu kuzihesabu kama ifuatavyo:
“Na mkizihisabu neema za Mwenyezi Mungu, hamwezi kuzimaliza. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye maghfira, Mwenye kurehemu.” (an-Nahl, 18)
Ambacho tunatakiwa kufanya kutokana na neema ambazo hazina ukomo ni kumjua na kumpenda Allah Mtukufu, ambae ndie mmiliki wa neema hizo, kuonesha kwamba tunampenda kupitia kuabudu na kumuonesha shukurani na heshima zetu Kwake kama mrejesho wa neema anazotupa.
Kwakweli, ibada na shukrani zetu hazitoshi kwa neema anazotupa Allah katika ulimwengu huu. Kwa kweli, Allah ametuandalia neema kubwa Peponi ikiwa tutamuamini na kumuamini na ametuahidi neema zisizokwisha Peponi. Kwa hali hiyo, neema ambazo Allah ametuahidi kutupa siku ya Qiama ni upendeleo wake maalumu, huruma na malipo. Si kwamba tunapewa kama malipo halisi kupitia ibada na shukurani zetu.
Mtume (rehma na Amani ziwe juu yake) amelielezea jambo hili kama ifuatavyo:
“Matendo yenu hayawezi kuwapeleka peponi. Vile vile matendo yangu hayawezi kunipeleka peponi.Hili linawezekana tu kupitia huruma za Allah.”

Comments
Post a Comment