Ni nini faida za ibada kwa mtu mmoja mmoja na kwa jamii?

1. Moja kati ya faida za ibada ni kwamba, ibada huweka hukumu zinazohusiana na itikadi na imani kutulia katika moyo na nafsi na kutengamaa.
Kama inavyojulikana, elimu huongezeka, hukua na kumakinika kutokana na matendo na uzoefu. Ni vigumu kuihifadhi elimu ambayo haifanyiwi kazi na kutumiwa; haitokuwa na maana yoyote kwa mwanadamu. Jambo hilo ni sahihi pia kwa elimu na hukumu za Imani na itikadi. Hutulia katika moyo wa mwanadamu tu kupitia ibada, kwa sababu ibada, ambayo maana yake ni kutekeleza maamrisho ya Allah na kuacha makatazo yake, ni kama kutenda na kuifanyia kazi Imani.  
Kuacha ibada husababisha taathira chanya ya Imani katika tabia ya mwanadamu kudhoofika na kufutika kabisa kwa kadri muda unavyoenda. Kwa kadri ambavyo taathira chanya ya tabia ya mwanadamu hudhoofika tabia mbaya na matamanio yenye madhara hutawala katika ulimwengu wake wa hisia na kumsukuma mwanadamu kutenda madhambi mbalimbali na matendo maovu. Kwa mantiki hiyo, Imani na ibada vina uhusiano wa karibu sana. Kama tutaifananisha Imani na taa, basi ibada ni kama glasi ya taa hiyo ambayo huizuia kuharibiwa na upepo na hivyo kuongeza mwanga wake. Katika kuonesha kazi ya ibada kuilinda Imani, Mtume (rehma na amani ziwe juu yake) amesema, “Imani ni mwili ulio uchi; nguo yake ni ucha Mungu.” Kama inavyojulikana, ucha Mungu ni kuacha makatazo ya Allah na kujitenga mbali sana na mambo yote ya haramu na dhambi; tuliyoyaorodhesha juu ndio maana ya ibada.
2. Ibada hufanya kazi muhimu ya kupangilia mfumo wa maisha wa mtu kwasababu ibada hugeuza fikra zote kwa Allah Mtukufu na kuuweka utukufu na ukubwa wa Allah katika akili za watu. Jambo hili humfanya mtu kufukiria kupata radhi za Allah katika kila jambo analofanya na kutii maagizo ya Kiungu na kuacha makatazo yote.
Hivyo, maisha ya mtu binafsi yanapangiliwa kwa kufuata maelekezo ya dini na huwekwa katika nidhamu maalumu kivitu na kiroho.
3. Ibada hufanya kazi muhimu sana ya kuunganisha watu na kuhakikisha Amani na upendo katika jamii vile vile. Kuabudu kwa kuelekea Qibla kimoja huanzisha uaminifu usiovunjika na uhusiano usio na ukomo baina ya Waislamu. Uaminifu na uhusiano huu huleta umoja imara, mapenzi ya dhati na urafiki wa kweli.
Hivyo, maisha kwenye jamii yanakuwa ya Amani na upendo; maendeleo ya vitu na kiroho hudumishwa.
4. Kwa ajili ya kuleta athari za ibada kwenye ulimwengu wa kitabia na kiroho wa mwanadamu:  
Muumini anaetekeleza ibada zake hupata Amani na utulivu. Huwa madhubuti kiroho. Huishi kwenye amani na furaha kwenye maisha yake yote pamoja na utulivu wa kisaikolojia wa mtu anaetekeleza majukumu yake.
Hatohisi kuchanganyikiwa, kuchoshwa au kukata tamaa. Hatohisi huzuni na kukosa matumaini wakati anapokabiliwa na changamoto, mazito na yasiyowezekana; hatopoteza msimamo na kujiamini kwake. Ulimwengu wa ndani wa mtu anaetekeleza ibada huwa na utulivu uliotengamaa. Kimbunga cha kisaikolojia, mikanganyiko na migogoro haitochukua nafasi katika maisha yake.
5. Ibada ndio njia kubwa kufikia ukamilifu wa mtu na kufikia ukomavu.
Kama inavyojulikana, mwanadamu ni kiumbe kidogo na dhaifu kwa kiwiliwili chake. Ingawa, anamiliki nafsi madhubuti na vipawa vikubwa vya akili. Fikra zake na matakwa yake hayana ukomo; fikra zake hazikuwekewa mipaka wakati alipoumbwa. 
Kitu kinachonyanyua na kukuza nafsi ya mwanadamu, ambae atakuwa na asili hiyo, ni ibada.
Kitu kinachokuza uwezo wake na akili zake ni ibada.
Kitu kinachonyanyua hisia na matamanio ni ibada. 
Kitu kinachomtambulisha malengo yake na kuyafanya upya matumaini yake ni ibada.
Kitu kinachohakikisha mawazo sahihi na hoja za msingi kwa kuziwekea kanuni za nidhamu fikra zake ni ibada.
Kitu kinachodhibiti hisia na mihemko, ambacho kinamlinda mtu asivuke mipaka na kuvuka kiwango katika utendaji wa mambo ni ibada.
Kwa ujumla, ibada ni kitu kinachomfanya mwanadamu kupata ukamilifu, Ukomavu wa kitabia na kiroho.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU