NI MALI ZIPI AMBAZO INAWAJIBIKA KUZITOLEA ZAKA?

Zaka sio wajibu katika vitu ambavyo Muislamu anavimiliki ili kufaidika navyo moja kwa moja yeye mwenyewe, kama vile nyumba yake anayoishi hata kama itakuwa na thamani kubwa kiasi gani, wala gari lake analotumia  hata kama ni la kifahari kiasi gani. Hivyo hivyo nguo zake, chakula chake na vinywaji vyake.

Allah amewajibisha zaka katika aina fulani ya mali ambazo zina sifa ya kwamba hazipo katika mahitaji ya matumizi yake ya lazima, na ambazo kwa kawaida ya mali hizo zinakuwa na kuongezeka, kama hizi zifuatazo:
  1. Dhahabu na Fedha ambazo hazitumiki katika mavazi na mapambo:
Zaka sio wajibu katika vitu hivyo isipokuwa tu vikifikia kiwango cha kisheria, na vikazungukiwa na mwaka mzima wa mwezi muandamo ambao hisabu yake ni  siku 354.
Kiwango cha zaka katika Dhahabu na Fedha ni kama ifuatavyo: 
Dhahabu ni takriban gramu 85, na Fedha gramu 595. 
Ikiwa Muislamu anamiliki kiwango hiki na kikazungukiwa na mwaka, atatoa zaka ya asilimia 2.5%.
  1. Hela na sarafu kwa aina zake zote, sawa ziwe ziko mkononi mwake au zimehifadhiwa benki.
Utoaji wa zaka yake: Kiwango cha hela na sarafu kinahesabiwa kwa thamani ya dhahabu. Kama hela au sarafu inalingana na kiwango cha dhahabu au kinazidi kiwango cha dhahabu ambacho ni takriban gramu 85 katika wakati wa kulazimika kutoa zaka, na ikawa umepita mwaka wa mwezi muandamo huku hela hiyo ikiwa bado ni mali yake, basi atatoa zaka ya asilimia 2.5%.
Mfano: Thamani ya dhahabu inabadilika. Kama tukichukulia  kwamba thamani ya dhahabu wakati wa kulazimika kutoa zaka ni sawa na Dola 25, basi kiwango cha hela kitakuwa kama ifuatavyo: 
25 (Thamani ya gramu ya dhahabu ambayo inabadilika badilika) x85 (idadi ya gramu ambayo haibadiliki) = Dola 2,125. Hicho ndicho kiwango cha hela.
  1. Bidhaa za biashara:
Maana yake: Ni kila kitu kilicho andaliwa kwa ajili ya biashara, ikiwa ni pamoja na mali isiyo hamishika kama vile viwanja, nyumba na majengo mengine, au bidhaa kama vile vyakula na bidhaa nyingine zitumiwazo.
Namna ya kutoa zaka yake: Mtu anatakiwa kuhesabu thamani ya vitu vyote alivyoviweka kwa ajili ya biashara, pale utakapopita mwaka mzima. Tathmini itakuwa kwa bei ya soko kwa siku hiyo anayotaka kutoa zaka.  Thamani ya bidhaa hizo ikifika kiwango cha zaka ya hela, ataitolea zaka ya robo ya asilimia kumi (2.5%).
  1. Mazao, matunda na nafaka zitokazo ardhini:
Allah  amesema kuwa: «Enyi mlioamini, toeni katika vile vizuri mlivyo vichuma na katika vile tulivyo kutoleeni ardhini». (Sura Albaqara, aya 267).
Zaka ni wajibu katika aina maalumu za mazao, na sio katika mazao yote, kwa sharti la kufikia kiwango maalumu cha kisheria.
Na kunakuwa na tofauti kati ya mazao yanayolimwa kwa kutumia mvua na yanayolimwa kwa kutumia gharama. Imeangaliwa katika kiwango cha lazima cha kutoa zaka kwa kuangalia hali za watu. 
Masharti ya kulazimika kwa zaka ya mazao na matunda:
  1. Mazao yafikie kiwango:
Mtume, swallalahu alayhi wasalam, ameainisha kiwango ambacho zaka inakuwa wajibu katika kiwango hicho, na haiwi wajibu katika kiwango ambacho ni  chini ya hapo. Amesema: «Chini ya wakia tano za tende hakuna zaka». (Bukhari, Hadithi Na. 1447. Muslim, Hadithi Na. 979).
Hicho ni kipimo cha ujazo. Lakini kwa kipimo cha uzito, kwa zao la ngano na mchele inakisiwa kuwa kati ya kilogramu 580 na kilogramu 600.  Chini ya kiwango hicho hakuna zaka.
  1. Mazao yawe katika yale yanayo takiwa kutolewa zaka: 
Zaka sio wajibu isipokuwa tu katika mazao ambayo yanaweza kuwa chakula ambacho, kwa kawaida, kinamfanya mwanadamu aishi, na ambacho inawezekana kukihifadhi kwa muda mrefu bila ya kuharibika, kama vile ngano, shairi, zabibu, tende, mchele na mahindi. Ama jamii ya matunda na mbogamboga ambazo haiwezekani kuzihifadhi kwa muda mrefu na kuzitegemea kama chakula, zaka sio wajibu katika mazao hayo. Mfano ni kama tikitimaji, komamanga, saladi, viazi, karoti, karanga, korosho na mfano wake.
  1. Kufika kwa muda wake wa kuvunwa:
Zaka inakuwa wajibu katika mazao na matunda yatakapokuwa yamevunwa, na wala hayafungamanishwi na kupita kwa mwaka. Kama mazao yanavunwa mara mbili kwa mwaka, zaka itakuwa wajibu katika kila mavuno (atatoa zaka mara mbili). Kama mtu kayatolea zaka mazao yake, kisha akayahifadhi kwa miaka kadhaa, hakuna zaka katika miaka hiyo. 
  1. Mifugo
Makusudio ya mifugo ni wanyama wa kufuga ambao  binadamu anafaidika nao, hasa hasa ni: Ngamia, Ng`ombe, Mbuzi na Kondoo tu.
Allah amejisifu kwa waja wake kwamba amewapa neema ya kuwaumbia wanyama hao ili wanadamu wale nyama zao, wavae nguo zitokanazo na manyoya yao na kuwabebea mizigo yao katika kusafiri. Allah amesema kuwa: «Na amekuumbieni wanyama wa kufuga ambao wana (kupeni vazi linalokupeni vuguvugu la) joto na manufaa mengine, na wengine mnakula. Na wanakupeni mandhari nzuri (ya kukufurahisheni) mnapowapeleka malishoni asubuhi na mnapowarudisha jioni. Na wanabeba mizigo yenu na kuifikisha katika miji ambayo msingeweza kuifikia isipokuwa kwa tabu sana. Hakika, Mola wenu ni Mpole sana na Mwenye rehema». (Sura An-nahli, aya 5-7).
Masharti muhimu ya zaka ya mifugo
  1. Wanyama wafikie kiwango cha kisheria; kwa sababu  zaka sio wajibu isipokuwa kwa matajiri tu. Ama wenye kumiliki idadi ndogo ya wanyama kwa mahitaji yao binafsi, hakuna zaka katika wanyama hao. Kiwango cha ngamia ni watano, mbuzi na kondoo ni arubaini na ng`ombe ni thalathini. Chini ya kiwango hicho hakuna zaka.
  2. Mifugo iwe imefika mwaka kamili wa mwezi muandamo ikiwa kwa mmiliki kwake.
  3. Wanyama wawe wanakwenda malishoni. Hawa ni wanyama ambao wanakula majani machungani, na wala mfugaji wake habebi mzigo wa gharama za chakula cha mifugo yake kipindi kikubwa cha mwaka.
  4. Wasiwe wanafanyishwa kazi. Wafanywishao kazi  ni wanyama ambao mmiliki wake anawatumia katika kulima au kubebea mizigo na bidhaa. Hakuna zaka katika wanyama hao.
Allah amewajibisha zaka katika ngamia, n’gombe, mbuzi na kondoo iwapo wanachunga na kula majani na mmiliki wake haingii gharama ya kuwalisha.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU