Ni ipi hali ya watu wa fatrah (kipindi baina ya mitume miwili) ambao hawakujua kuhusu Uislamu? Jee watakwenda motoni kwa vile walikufa bila ya Imani?

Fatrah maana yake ni kusimama na kupitiwa na muda ndani ya kipindi fulani. Kama neno la kidini, linamaanisha kipindi (muda) baina ya mitume wawili.
Katika hadithi iliyosimuliwa na Bukhari, fatrah maana yake ni kipindi (muda) baina ya mtume Issa na mtume Muhammad (rehma na Amani ziwe juu yao). (1)
Inafahamika katika baadhi ya aya kwamba Waarabu kabla ya Uislamu walikuwa na ufahamu mdogo juu ya mitume waliotumwa kwa watu. Katika Qur’an, imetajwa kwamba Waarabu waabudu masanamu walisema: “…Lau angelitaka Mola wetu mlezi (Kututumia mitume kutuonya) bila ya shaka angeli wateremsha malaika”. (2) na hivyo basi inaelezwa jinsi gani walivyokuwa na uelewa mdogo kuhusu Utume na pia kuhusu dini za haki.
Ingawa Waarabu walijua kuwa Mtume Ibarahim alikuwa ni mtume, walijua kuwa utume wake uliishia katika wakati wake, Kutokana na kipindi kirefu cha miaka elfu tatu (3000) baina ya Mtume Ibrahim na Mtume Muhammad (rehma na Amani ziwe juu yao), si wengi waliojua usafi (Hanif) wa dini aliyokuja nayo Mtume Ibrahim.
Wasomi wa Kiislamu wanawajadili watu wa fatrah (wale walioishi kwenye nyakati baina ya mitume wawili) kwa kuwagawa kwenye makundi matatu:
1. Wale waliojiridhisha na kukubali uwepo na umoja wa Allah kwa msaada wa hoja na uwezo wa akili zao kama vile Qus bin Saida na Zayd bin Amr, baba wa Said bin Zayd ambaye alibashiriwa pepo, n.k.
2. Wale walioingilia kwa kuiharibu na wakaibadili Imani ya Mungu mmoja, wakakubali ibada za masanamu pamoja na wale waliovumbua dini kwa matashi yao na wakawakusanya watu waliowazunguka kuwashawishi: akiwemo Amr bin Luhay, ambaye alianzisha ibada za masanamu kwa Waarabu na waabudu masanamu wengine, n.k.
3. Wale ambao hawakujiingiza ima kwenye Imani sahihi au Imani potofu, ambao hawakuwa waumini wala hawakuwa waabudu masanamu, na ambao waliyapitisha maisha yao kwenye ujinga, na ambao hawakuwahi kufikiri kuhusu mambo haya. Kwenye kipindi cha ujinga (kipindi cha ujinga kabla ya ujio wa Mtume) kulikuwa na watu wa aina hiyo pia.
Katika makundi haya matatu, kundi la pili litakwenda motoni kwasababu walikuwa waabudu masanamu. Wale wanaoangukia katika kundi la tatu hawatoingia motoni kwasababu ndio hasa watu wa kipindi cha fatrah. Hii ni kwasababu mtume ambaye angewalingania kwenye dini sahihi na ya kweli hakuwafikia na hawakuonesha ishara za kutokuamini; na kwa hiyo walikuwa miongoni mwa waliosalimika. Wanazuoni wote wa sunnah (Ahl As-Sunnah - kundi lenye wafuasi wengi) wamekubaliana kwenye hili. (3)
Qus bin Saida na Zayd bin Amr waliotajwa kwenye kundi la kwanza, kwa upande mwengine, watafufuliwa na Allah siku ya Kiama kama ni ummah tofauti (jamii), kwa vile wao waliamini uwepo na umoja wa Allah kati ya maelfu ya watu waliokuwepo kipindi hicho, na hawakuwa watu wa mtume yoyote kwasababu hakukuwa na mtume aliyetumwa kwao, na hawakufika kipindi cha Mtume Muhammad (rehma na amani ziwe juu yake). Wao ni watu walionusurukia na wakaokoa maisha yao ya milele kwasababu ya Imani zao. Watakapofufuliwa, watakuwepo uwanja wa makusanyo siku ya hukumu kama “jamii ya mtu mmoja”. Watu hawa ni “wa kipekee”  watafunikwa na rehma na huruma za Allah.
Ni Dhahiri kwamba watu wa fatrah hawahusiki na ibada pamoja na amri za kidini. Ingawa, kuna mgongano kati ya madhehebu mawili ya watu wa Sunnah (Ahl as-Sunnah), Maturidi na Ash’ari, kwamba jee walipaswa kuamini au laa. Kwa mujibu wa Imani ya dhehebu la Maturidi, watu hao walipaswa kutumia hoja na uwezo wa akili walioruzukiwa na Allah ili uwafikishe katika kufahamu uwepo wa Allah kwa kutathmini umbile la mbingu na ardhi na kila kilichomo. Kwa mujibu wa Ash’ari, kwa upande mwengine, watu wa fatrah hawalazimishwi kumuamini Allah. Na hii ni kutokana na hali ya kutokuletewa mtume. Allah anasema katika Qur’an: “…Wala Sisi hatuadhibu (mtu au jamii kwa makosa waliyofanya) mpaka tumpeleke Mtume.” (4) Hivyo basi, hawastahili kuadhibiwa kwasababu hawakupelekewa mtume.
Badiuzzaman, mwanachuoni wa Kiislamu ambaye aliishi na kuchapisha kazi kadhaa karne ya ishirini (20), anaileta aya iliyotajwa kama ushahidi na anasema:
“Watu walioishi kipindi baina ya mitume wawili ni miongoni mwa waliosalimika. Imetajwa kwamba hawatoadhibiwa kwa makosa yao kwenye mambo ambayo si ya msingi. Kwa mujibu wa Imam Shafi'i na Imam Ash'ari, wanasema kwamba hata kama si waumini na hawakuamini misingi ya Imani, bado watakuwa ni wenye kusalimika. Wajibu mbele ya Allah huwepo pale anapopeleka mitume, na mitume wakishaletwa, kuwajibika huanza kupitia elimu ya ujumbe wao. Kwavile kutokujali na kupita kwa muda mrefu kuliwafanya wasijue misingi ya dini ya mitume waliotangulia hawakuweza kutoa ushahidi kwa watu wa kipindi hicho. Kama watatii mfumo wa maisha uliotangulia, watapata malipo; na kama hawakufuata, hawatoadhibiwa. Na kwa msingi huo basi, kwa vile mfumo wa maisha ulifichika, hauwezi kuwa uthibitisho.” (5) 
Imam Ghazali, Mwanachuoni wa Kiislamu muhimu, anawagawa watu baada u utume wa Mtume Muhammad (rehma na amani ziwe juu yake) katika makundi matatu makubwa:
1. Wale ambao hawakusikia kuhusu ujumbe wa Mtume na hawakupata taarifa kuhusu Mtume. Wale watakaoangukia kwenye kundi hili ni watu waliosalimika na wataingia peopni.
2. Wale ambao walisikia kuhusu ujumbe wa Mtume, na miujiza aliyokuja nayo, tabia zake zilizotukuka, lakini hawakumuamini Mtume. Kundi hili bila shaka yoyote litaangamia na litapata adhabu iumizayo.
3. Wale ambao walilisikia jina la Mtume, lakini hawakusikia chochote zaidi ya propaganda chafu, na hakuna yoyote aliyewaeleza ukweli na kuwatia moyo kwenye Imani thabiti; kwa sababu hizi, wanabaki katikati. Na natumai kwamba nao watakuwa miongoni mwa watu waliosalimika na hivyo basi wataingia peponi.
Mwanachuoni Badiuzzaman, ambaye anaeleza kwamba mwisho wa zama, watatokea pia watu wa fatrah, na anaelezea kwamba aina hiyo ya watu wasio na hatia ambao hufa katika vita vya dunia nao pia watakuwa watu waliosalimika. Badiuzzaman anasema:
“Katika zama za mwisho (akhir zaman), kutaibuka dini na dini ya Muhammad (rehma na Amani ziwe juu yake) itakuwa kama joho fulani tofauti litakalo akisi aina fulani ya fatrah, na katika zama za mwisho kabisa dini sahihi ya Nabii Issa (Yesu) itatawala na kuwa bega kwa bega na Uislamu. Kwa sababu zote hizi, bila shaka majanga waliyoyapata Wakristo ambao walimfuata Nabii Issa (Yesu) ni aina ya mateso kwao.” (6) 
Marejeleo
1. Bukhari, Manaqibu'l-Ansar: 53.
2. Qur’an, Fussilat , 14.
3. Tajrid-i Sarih trns, 4:544.
4. Qur’an, Isra, 15.
5. Barua za (Mektubat), 360-361.
6. Kastamonu Lahikası, p. 77.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU