Msaidie Mume Wako Kupata Maendeleo

Msaidie Mume Wako Kupata Maendeleo

Wanadamu kiasili wanazo nguvu zisizo dhihirika za kuwawezesha kupata maendeleo. Kupenda kupata ubora ni hali ambayo kila mmoja wetu anayo; na tumeumbwa ili tuweze kufanikisha ubora.
Kila mmoja, ambaye anayo kazi yoyote katika umri wowote na katika hali yoyote anaweza kuendelea na kukomaa. Mtu hatakiwi kutosheka na hali ya yeye kuwepo tu na asisahau makusudio ya kuumbwa. Mtu lazima ajaribu kupata ubora katika kipindi cha uhai wake.
Licha ya kwamba kila mtu anafuatilia maendeleo, si wote wanaofanikiwa kupata maendeleo yanayohitaji malengo ya juu na juhudi kubwa ya kufanya kazi. Mtu lazima atayarishe uwanja na kuondosha vigingi na baada ya hapo anachukua hatua muhimu za kuelekea kwenye mkondo wa maendeleo. Umashuhuri wa mwanaume unategemea sana utashi wa mke wake. Mwanamke anaweza kumsaidia mume wake kupata maendeleo kama vile ambavyo pia anaweza kuwa mwenye kusababisha hasara kuhusu maendeleo ya mume wake.
Mpendwa Bibi! Wakati ambapo unafikiria uwezekano, fikiria hadhi ya juu zaidi ya mume wako na umtie moyo wa kufanikiwa. Kama bado anataka kuendelea na masomo yake au kama anataka kuongeza ujuzi wake kwa njia ya kusoma na utafiti, basi usimsitishe. Mpe moyo wa kufanikisha matakwa yake Panga maisha yako kwa namna ambayo hayatakuwa kipingamizi cha maendeleo yake.
Jaribu kumsaidia ili apate maendeleo kwa kutengeneza mazingira ya kuburudisha na kuliwaza ndani ya nyumba yenu. Kama mumeo hakusoma, mshawishi kwa unyenyekevu, mwambie aanze masomo yake ya usiku.
Kama mumeo ni msomi, mtie moyo wa kuongeza ujuzi wake kwa kusoma zaidi.Kama mume wako ni daktari wa tiba, mhamasishe asome majarida ya tiba na makala zingine zinazohusiana na tiba.
Kama mumeo ni mwalimu, mhandisi au jaji, basi mwambie awe anasoma vitabu na makala mbali mbali zinazohusiana na utaalamu wake. Unatakiwa kukumbuka kwamba katika kazi yoyote ambayo anafanya mumeo, ipo fursa ya kuendelea.
Usimruhusu mume wako aache mkondo ambao umewekwa na mpangilio kwenye muumbo. Mtumainishe asome vitabu. Usiruhusu umashuhuri wake usiendelee kuongezeka.
Kama hana muda wa kununua au kupata vitabu basi kwa kutumia ufawidhi wake wa rafiki yake, pata vitabu anavyo vipenda yeye. Mpe vitabu hivyo na mpe matumaini ya kusoma. Wewe pia unatakiwa kusoma vitabu na majarida yenye manufaa. Kama katika kusoma kwako unasoma makala ambayo ina manufaa kwa mume wako, basi mtaarifu. Kitendo hiki kina manufaa kadhaa:
Kwa kufanya hivi mara kwa mara, mume wako atakuwa mtu mwenye kuelimika ambaye atakujengea heshima wewe na yeye. Aidha, atakuwa bingwa mzuri sana ambaye huduma zake zita mnufaisha yeye na jamii yake.
Kwa kuwa amekubaliana na sheria za muumbo, kupitia kwenye masomo na utafiti wake, hapatakuwepo na uwezekano yeye kupata maradhi ya akili na kuchanganyikiwa.
kwa kuwa yupo kwenye mkondo wa kuelekea kwenye maendeleo na anaonesha kupendelea kusoma, basi ataambatana zaidi na wewe na watoto, hatavutiwa kwenye uovu na hatanasa kwenye mtego wa mazoea ya hatari.

Kuwa Mwangalifu Mume Wako Asipotoshwe

Wanaume wanatakiwa kuwa na uhuru wao na ushirikiano wao katika shughuli ili waweze kufanya kazi na kuendelea kwa namna inayowafaa. Kama wanaume watawekewa masharti katika shughuli zao, basi, hawatakuwa na furaha. Mke mwenye busara hawezi kuingilia mambo ya mume wake.
Mke hatakiwi kufuatilia nyendo za mume wake; kwa sababu lazima atambue kwamba kwa kumnyima mume wake uhuru anaouhitaji na kujaribu kumdhibiti katika shughuli zake anaweza kujibu kwa ukali sana.
Wanaume wenye busara na uzoefu hawahitaji kudhibitiwa.Wanaume kama hao kila mara kufanya mambo yao kwa busara; si rahisi kuwa danganya; wao wanawajua marafiki zao na maadui zao. Hata hivyo, wapo watu ambao ni wa kawaida; watu hawa wanaweza kudanganywa kwa urahisi na kuvutiwa kwa urahisi na watu wengine.
Wapo watu ambao ni laghai na wanangoja kuwadanganya watu wa kawaida. Mtu laghai, licha ya kujifanya kuwa mwema, humtega na kumnasa mtu mwingine na kumwelekeza kwenye uovu. Jamii iliyojaa uovu na tabia ya binadamu isiyokubali kushindwa haisaidii kurekebisha hali. Mtu wa kawaida anaweza asijue hali yake kwa kipindi fulani, lakini siku moja anashtuka na kujikuta yupo kwenye kina cha mtego na hawezi kujinasua.
Ukiangalia kila mahali pale ulipo, utaona watu wengi wa aina hiyo wenye bahati mbaya. labda hakuna hata mmojawao aliye nuia kuanguka kwenye mtego au kuwa mwovu. Lakini kupitia kwa urahisi wao, ujinga na uamuzi wa pupa sasa wamekuwa mawindo ya waovu katika jamii.
Kwa sababu hii, watu wepesi wanatakiwa kusimamiwa. Kwa kufuatilia shughuli zao, watu wenye busara na wenye kuwatakia mema wenzao watakuwa wamewafanyia huduma kubwa.
Watu wazuri sana kwa kazi hii, hata hivyo, ni wake wa wanaume hawa. Mke mwenye busara na mwerevu anaweza kufanikiwa kazi kubwa sana kuhusu mume wake, kwa msimamo wa kumsaidia na busara.
Wanawake wa aina hii, hata hivyo, lazima wakumbuke kwamba hawatakiwi kuingilia moja kwa moja mambo ya waume zao, au kuwaambia “Wafanye hivi” na “wasifanye vile”. Sababu yake ni kwamba wanaume mara nyingi hawataki kabisa kutumiwa kama kitendea kazi mikononi mwa wengine vinginevyo watajibu kwa ukali. Lakini mwanamke mwenye hekima angefuatilia shughuli za mumewe na kuwaangalia washirika wake bila kudhihirika, na mume asitambue.
Pia hutokea kwamba baadhi ya wanamume, wakati mwingine huchelewa kurudi nyumbani isivyo kawaida. Endapo jambo hili linatokea na idadi ya siku anazochelewa kurudi nyumbani imo katika kiwango kinacho kubalika, basi hapana haja ya kuwa na wasi wasi, kwa sababu upo wakati ambapo wanaume hujikuta wanajaribu kushughulikia mambo ambayo hawakuyategemea baada ya kazi zao. Hata hivyo, endapo idadi ya siku anazochelewa kurudi nyumbani inazidi kiwango kisicho kubalika, basi, mke wake atalazimika kufanya upelelezi. Lakini, upelelezi si jambo rahisi, unahitaji uvumilivu na busara, mtu lazima aepuke hasara na malalamiko.
Kwanza kabisa, mke anatakiwa azungumze na mume wake kwa upole na wema: Mke amuulize mume wake kwa nini alirudi nyumbani kwa kuchelewa kuliko jana yake na alikuwa wapi. Mke anatakiwa kufuatitilia jambo hili kwa busara na uvumilivu katika nyakati mbali mbali na fursa tofauti. Kama atagundua kwamba mumewe huchelewa kurudi nyumbani kwa sababu ya kazi yake au kuhudhuria mkutano wa kisayansi, kidini na kimaadili, basi amwache aendelee hivyo. Kama mke anahisi kwamba mume wake amepata rafiki mpya, anatakiwa ajue rafiki huyoni nani. Kama rafiki yake mpya ni mtu mwenye tabia njema na mwenendo safi, basi, asiwe na wasi wasi, kwa sababu rafiki mzuri ni neema kubwa.
Ukihisi kwamba mume wako anaingia kwenye upotofu au ameshirikiana na watu waovu na wasiofaa, basi unatakiwa umsitishe haraka sana. Katika hali kama hii, mwanamke anao wajibu mkubwa sana.
Kosa dogo tu katika kushughulikia jambo hili, kwa kufanya uzembe, linaweza kuharibu maisha ya familia yao.
Hii ni hali ambapo busara na werevu wa baadhi ya wanawake hutumika na kudhihiri. Mtu lazima akumbuke kwamba ugomvi na ubishi si suluhu na huweza kusababisha kinyume chake. Mwanamke nayepitia kwenye tukio hili anazo kazi mbili za kufanikisha: kwanza anatakiwa kutathmini hali ya nyumbani; na ajipime yeye mwenyewe na msimamo wake. Lazima agundue sababu ya tabia ya mume wake.
Lazima afanye uamuzi usio na upendeleo kwa nini haoneshi uchangamfu kwa familia yake na kuelekea kwenye upotofu. Mke anaweza akang’amua kwamba msimamo wake mwenyewe ndio umekuwa sababu; au labda alikuwa ndio sababu; au labda alikuwa hajali vyakula anavyo vipenda mumewe, jinsi anavyoonekana au mambo ya nyumbani. Mambo kama haya huwafanya wanaume wafarakane na familia. Wanaweza wakafuatilia mambo ya upotofu ya nje ili wasahau matatizo yao. Mke anaweza kumuuliza mume wake kuhusu matatizo yake na ajaribu kusaidia kuyatatua.
Kama mwanamke alijisahihisha na kuibadilisha nyumba kulingana na matakwa yake, basi, awe na matumaini kwamba mume wake atarudi tena kwenye familia yake na kwamba ataepuka sehemu zenye uovu.
Pili, mke lazima amwoneshe mume wake wema mwingi kadiri iwezekanavyo. Lazima amshauri mume wake na kumkumbusha matokeo mabaya na matendo yake. Anaweza hata kulia na kumwambia awaache marafiki zake wabaya. Lazima amwambie: Nina kupenda kwa dhati ya moyo wangu. Ninajivuna kuwa na wewe. Ninaona heri kuwa na wewe kuliko vitu vyote na nipo tayari kujitolea kwa ajili yako. Lakini nina huzunishwa na kitu kimoja; kwa nini mwanamume kama wewe, awe na marafiki kama, au ahudhurie dhifa ya aina hiyo? Matendo kama haya hayastahili kufanywa na wewe. Tafadhali acha kufanya mambo haya.
Mke lazima aendelee na msimamo huu hadi aushinde moyo wa mume wake. Inawezekana kwamba mume amezoea kuendekeza tabia zisizofaa na kwamba hawezi kuathiriwa kwa urahisi, lakini mke asikasirike. Lazima afuatilie lengo lake kwa juhudi na uvumilivu zaidi.
Wanawake wanao uwezo mkubwa kwa wanaume. Mwanamke anaweza kufanya lolote atakalo kama akili yake itamwelekeza kufanya hivyo. Kama mwanamke anaamua kumwokoa mume wake kutoka kwenye kinyaa cha maovu, anaweza kufanya hivyo. Upo uwezekano wa asili mia themanini kushinda, almuradi utekelezaji wake uwe wa busara. Kwa vyovyote vile, mke hatakiwi kutumia nguvu au msimamo wa ukali; isipokuwa tu kama haoni matokeo yoyote ya kuonesha wema na upole kwake. hata hivyo, hatakiwi agombane, aondoke nyumbani au atumie njia nyingine yoyote ile ya upole kadiri iwezekanavyo na si kulipize kisasi.
Ndio, kutunza mume ni kazi ya kila mke. Ni kazi ngumu na ndio maana Mtume (s.a.w) alisema: “Jihadi ya mwanamke ni kumtunza mume ipasavyo.”

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU