Kwanini wanawake katika Uislamu wana nusu ya haki ya wanaume katika kutoa ushahidi?

Dear Brother / Sister,
Mambo ya lazima yanayounda misingi ya sheria ya Kiislamu yanategemea ufunuo (wa Allah). Yameorodheshwa katika Qur’an. Kwa maneno mengine, mambo ya lazima yamewekwa na kuamrishwa na Muumbaji wa Ulimwengu. Zama, angahewa na mazingira yoyote mtu anamoishi, mambo hayo ya muhimu ndio chanzo cha amani na njia ya kupata faraja. Hii ni kwa sababu ya amri hizo ndio zenye kufaa zaidi kwa uumbwaji wa mwanadamu. Amri na mamlaka za kisheria katika Qur’an zinapotafitiwa, nukta inayosalia nki kwamba kuwepo kwa mwanadamu kimwili na kiroho huzingatiwa.
Katika mambo ya kutoa ushahidi, inawezekana kuliangalia hilo, pia. Tafsiri ya aya inayohusu kutoa ushahidi ni kama ifuatavyo:
“…Na mshuhudishe mashahidi wawili katika wanaume wenu. Ikiwa hapana wanaume wawili, basi mwanamume mmoja na wanawake wawili katika mnao waridhia kuwa mashahidi. Ili ikiwa mmoja wao akipotea, mmoja wao amkumbushe mwengine…” (1)
Kwa hivyo, hapa, jambo la msingi linahusiana moja kwa moja na uumbwaji wa wanawake. Hili ni sharti la sura yao ya kisaikolojia. Msingi wa silika ya mwanamke ni kusisimka na yeye anaishi kwa misisimko yake. Kwa hiyo, dhana hujikita moyoni mwake zaidi kuliko akilini mwake na kuleta athari kwa njia hiyo. Kwa hakika hawezi kutokuwa na upendeleo mbele ya matukio. Yeye huliendea jambo akiwa na welewa unaoendana na jinsi inavyotawala dhamiri na huruma yake.
Kwa sababu ya sifa yao hiyo, Qur’an inasema: “Wanawake wanaweza kusahau, kwa hiyo wanatakiwa wapewe wasaidizi katika ushahidi.” Hayo yamesemwa na Allah aliyemuumba mwanamke. Kwa hivyo, ni kanuni isiyobadilika. Je hakuna wanawake wasiosahau kirahisi na wenye kumbukumbu kali kuliko wanaume? Ndiyo, wapo, lakini kwa ujumla, hali hiyo ya kisaikolojia (kusahau) huonekana mara nyingi zaidi kwa wanawake. Ni jambo la kimaumbie tu kwamba hawezi kutunza kumbukumbu kwa muda mrefu.
Kwa upande mwingine, mwanamke ni mndani sana. Ana dunia ya kwake mwenyewe. Yeye ameshughulishwa sana na kazi za nyumbani kutwa nzima. Anawatunza watoto na kuwalea. Wanawake wachache sana huvutiwa na kazi, biashara, na siasa. Mwanamke ambaye yuko mbali sana na dunia ya nje anawezaje kujua matukio yanayotokea huko, atayajuaje na kuyahifadhi akilini mwake na kwa kiasi gani ataweza kutoa ushahidi?
Kwa kupokea ushahidi wa wanawake wawili sawa na wa mwanamume mmoja, na kwa hivyo kutokumtwisha mzigo mwanamke kwa kumpa wajibu ule wa mwanamume katika mambo ya kuutoa ushahidi, Uislamu hauharibu haki yake, kinyume chake, unamuhifadhi na kumzuia asitende dhambi. Hayo ni kwa sababu kutoa ushahidi ni jukumu zito lenye majukumu makubwa.
Katika aya ya Qur’an, yanaelezwa yafuatayo:
“…Wala msifiche ushahidi. Na atakaye ficha basi hakika moyo wake ni wenye kutenda dhambi. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa mnayo yatenda.” (2)
Katika hadithi (maneno ya Mtume) yameonesha kuwa kutoa ushahidi kuna majukumu makubwa na kuwa ushahidi wa uongo unahesabiwa ni miongoni mwa madhambi makubwa mno.
Kwa hakika, Uislamu unamhifadhi mwanamke dhidi ya madhambi makubwa na kumzuia kutenda dhambi ya ushahidi wa uongo, kwa kuhadaiwa na baadhi ya udhaifu wake kupitia msisimko au kupitia hali ya kuwa na jazba. Uislamu umechukua tahadhari dhidi ya hilo kwa kumteulia mwanamke msaidizi kando yake. Kwa sababu hii tu, katika baadhi ya mambo ya ushahidi, wanawake wawili huchukua nafasi ya mwanamume mmoja.
Wakati mwingine wanawake wanaweza kuwa na wivu katika mambo watakayoyatolea ushahidi na hisia za ushindani zinaweza kutawala. Kwa hiyo, wanaweza kuwa na dosari ya kutambua haki kwa kuficha baadhi ya vipengele vya jambo hilo. Hata hivyo, ikiwa wanawake wawili watatoa ushahidi, mashaka yatafutwa pale mmoja wao atakapofafanua nukta atakayoificha mwingine.
Kwa upande mwingine, kuwa ushahidi wa wanawake wawili huchukulika kuwa sawa na ushahidi wa mwanamume mmoja hakuna namna ya kumaanisha kuwa mwanamke ana thamani ya nusu ya mwanamume. Hili ni dalili tu kuwa umuhimu mkubwa kwa kuwepo namna zote za uhakikisho katika ushahidi. Katika madai yapi mwanamke hutoa ushahidi, ni katika madai gani hayumo, na katika yapi ushahidi wake ni nusu ya ule wa mwanamume?
Sheria ya Kiislamu imemtoa mwanamke katika ushahidi wa makosa yanayohukumiwa adhabu inayoitwa ‘had’ kama vile uzinifu, pombe na wizi na katika adhabu za ‘qisas’ (kisasi) na ushahidi wake katika hayo haupokelewi. Katika madai hayo, adhabu ya uzinifu inahitaji ushahidi wa wanaume wanne na hayo mengine ni wanaume wawili. Katika madai yanayohusiana na mambo kama ya biashara, kuuza na kununua, ndoa na talaka, yaliyomo katika kundi la mahusiano na miamala, ikiwa hakuna wanaume wawili, basi ushahidi wa mwanamume mmoja na wanawake wawili hutakiwa. Hata hivyo, katika mambo ambayo wanaume si mahiri kama vile kujua ubikira, hali za wakati wa uzazi kuhusu mama na mwana, na kuanzisha undugu wa kunyonya, ushahidi wa mwanamke mmoja unatosha. Zaidi ya hayo, Umar Ibn Al-Khattab (Allah awe radhi naye) aliona ushahidi wa mwanamke mmoja kuwa unatosha hata katika mambo ya talaka. Hayo ni kwa sababu kusudio halisi katika ushahidi ni kuhifadhi haki mbalimbali, kuendeleza haki na kuutambua ukweli. Hekima mojawapo ya kutokutumia ushahidi wa mwanamke katika adhabu za ‘had’ na katika qisas (kisasi) ni kiwango cha hisi ili kuzuia shaka hata ndogo sana katika mambo hayo. Hayo ni kwasababu katika madai ya qisas kwa kauli zisizo kamilifu, haki ingeweza kukiukwa au mtu angeweza kulipiziwa kisasi kimakosa. Mwelekeo kama vile wa usahaulivu na kuelemewa na jazba kuhusu wanawake kunaweza kulitoa jambo hilo maanani.
(1) Al-Baqarah, 282.
(2) Al-Baqarah, 283.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU